Habari Za Muda Wadau.
Naomba Msaada Wenu Mambo Yameniharibikia.
Nina Mchumba Aitwae Amina Ambae Tumeshatambulishana Kwa Wazazi Na Kwa Uweozo Wa Mwenyezi Mungu Nataraji Kumuoa Mapema Mwakani. Kabla Ya Kuwa Nae Takriban Mwaka Mmoja Ulopita, Tulikuwa Marafiki Wa Karibu Na Tulisaidiana Kwa Sihida Na Raha. Nilipo Mueleza Nia Yangu Mara Ya Kwanza Alikataa Na Akasema Hakuwa Tayari Na Hakutaka Kutoa Sababu Zaidi. Nilisikitika Sana Ila Sikuwa Na Namna. Urafiki Uliendele Japo Nilianza Kupunguza Mazoea Kwakuwa Nilitaka Kumtoa Moyo Mwangu.
Nikaanza Kuongeza Ukaribu Na Msichan Mwingine Aitwae Mariam Nilokuwa Na Mazoe Nae Ya Kawaida Kwa Lengo La Kumsahau Amina Na Ili Nimsome Huyo Mariam Kama Angenifaa Kuwa Mbadala Amina. Wakati nafanya hivyo, Amina Ndio kwanza Alizidisha Mazoe, Na Kwakuwa Tayari Nilikuwa Nina Mpenda Nami Nikajikuta Nazidisha Ukaribu Badala Ya Kupunguza. Nikajikuta Tayari Nipo Ndani Ya Sintofaham, Kwani Nilikuwa Na Mahusiano Ya Karibu Sana Na Amina na Mariam na Sikujua Hatima Yake.
Baada Ya Miezi Takriban 4 Tangu Nilipo Ongea nae Akakataa, Amina Alinitamkia Mweneyewe Kuwa Yuko Tayari Kuwa Nami Na Alikuwa Hajanifaham Vya Kutosha Ndiomana Awali Alikataa.
Kipindi Chote Cha Nyuma Kabla Hata Sijamueleza Haja Yangu, Amina Alikuwa Akimfaham Mariam Kama Ndugu Yangu, Ndivyo Nilivyomwambia Coz Sikutaka Ajue Kuwa Ni Rafiki Tuu Kwa Kuhofia Kuwa Angenitafsiri Vibaya Na Angeweza Kuakataa Ombi Langu Pindi Nitakapo Kuja Muelzamkwani tangu mwanzo nilimsoma Amina kuwa ana wivu sana.
Baada Tu Ya Kunieleza Kuwa Yuko Tayari Kuwa Nami, Tulianza Uhusiano Na Nikamueleza Ukweli Juu Ya Mariam Kuwa Si Ndugu Yangu Ila Alikuwa Ni Rafiki Tu. Sikumueleza Kwa Undani Kuwa Tulikuwa Na Ukaribu Mkubwa Na Wala Sikumwambia Kuwa Nilikuwa Na Mpango Wa Kuwa Nae (Mariam) Baada Ya Yeye Kunikataa Mara Ya Kwanza. Amina Alinishauri Nikate Mawasiliano na Mariam, Na Nilikubaliana Nae. Nilianza Kupunguza Mwasiliano Na Mariam Na Baadae Nikayakat Kabisa Na Mpaka Leo Hatuwasilani na huyu mchumba wangu analijua hilo.
Lengo La Kutomueleza Amina Ukweli Ilikuwa Ni Ktomuumiza kwasababu Ana Wivu Sana Na Sikuona Haja kwasababu Nilishakata Mawasiliano Na Mariam.
Sasa Balaa Limeibuka Leo, Kakuta Msg Tulizokuwa Tukiwasiliana Na Mariam Kwenye Computer Yangu Huwa Nafanya Backup Ya Simu Mara Kwa Mara. Nilisha Zifuta Msg Za Mariam Nyingi Ila Nadhani Nyingine Sikuziona. Hapa Nilipo Kashakata Mawasiliano Nami, Na Hataki Tuendelee Tena Na Uhusiano.
Nimechnganyikiwa sababu Nampenda Sana, Na Sikotayari Kumpoteza. Hapokei Cm, Hajibu Msg Japo Nimetuma Zaidi Ya Msg 30. Ni Takriban Wiki 2 Zimepita Tangu Nimtambulishe Nyumbani Na Niko Kwenye Maanadalizi Ya Kufunga Nae Ndoa Mapema Mwakani. Naombeni Msaada Wenu Wadau, Sijui Nifanyeje Anielewe.
Nimebebmbeleza Na Kujieleza Kwenye Msg, Nimeomba Msamaha Lakini Hakuna Kilichofanikiwa.
Niko Njia Panda Sijui Nifanyeje?
Wenye ujuzi wa haya mambo plzz nisaidiaeni.