Mwenyekiti wa CCM taifa anaua chama

Mwenyekiti wa CCM taifa anaua chama

Mbuzimtu

JF-Expert Member
Joined
Jul 25, 2013
Posts
355
Reaction score
178
Watu wengi walitegemea kutakaswa kwa chama hicho kupitia hotuba ya mwenyekiti Jana. Baada ya hotuba yake jana, ni dhahiri kuwa mtuhumiwa namba moja wa mauaji ya chama cha mapinduzi ni mwenyekiti wa chama hicho.

Wakati chama kikizidi kupoteza mvuto mbele ya macho ya watanzania, hakuna juhudi za makusudi kukinusuru chama hicho. Hotuba ya mwenyekit wa CCM kwa wazee wa Dar es salaam ilikuwa nafasi adimu na pekee ya kukiinua chama na kurejesha mvuto kwa watanzania. Kilichotokea jana, mwenyekiti, kuamua kupiga danadana kwa namna tofauti kwenye skendali ya Escrow. Kusema Mhongo anawekwa kiporo ni kukiangamiza chama. Kushindwa kumwajibisha Maswi moja kwa moja ni kukiua chama. Mbaya zaidi, ni pale alipomwajibisha Tibaijuka ambaye ni mnufaika wa mbali sana katika skendali hii.

CCM kama chama itasema nini mbele ya watanzania?. Kwanini chama kikose mvuto kwajili ya watu wawili?. Nani mwenye ujasiri wa kuinadi CCm mbele ya watanzania wa leo baada ya hotuba ya jana?.
 
Uchaguzi wa SM ulioshirikisha Wananchi Matokeo--
Ccm 47%
Ukawa 53%

Mapingamizi 33%

Ccm Halali ni 47% + 33% = 80%

Ukawa 53% - 33% ongezeko la Mapingamizi ccm = 20%.

Je kulipowekwa Vikwazo ccm wangeshinda kwa 100% kama wananchi wangepewa fursa?
 
acheni akiue si atakuwa anarahisisha kazi
 
Uchaguzi wa SM ulioshirikisha Wananchi Matokeo--
Ccm 47%
Ukawa 53%

Mapingamizi 33%

Ccm Halali ni 47% + 33% = 80%

Ukawa 53% - 33% ongezeko la Mapingamizi ccm = 20%.

Je kulipowekwa Vikwazo ccm wangeshinda kwa 100% kama wananchi wangepewa fursa?

Jumlisha na hayo mapingamizi hawajafikisha 80%, achana nao na data zao za uongo hao.
 
kama umekereka malizia hasira zako kwenye sanduku la kura 2015
~~~chagua UKAWA!!
 
Watu wengi walitegemea kutakaswa kwa chama hicho kupitia hotuba ya mwenyekiti Jana. Baada ya hotuba yake jana, ni dhahiri kuwa mtuhumiwa namba moja wa mauaji ya chama cha mapinduzi ni mwenyekiti wa chama hicho.

Wakati chama kikizidi kupoteza mvuto mbele ya macho ya watanzania, hakuna juhudi za makusudi kukinusuru chama hicho. Hotuba ya mwenyekit wa CCM kwa wazee wa Dar es salaam ilikuwa nafasi adimu na pekee ya kukiinua chama na kurejesha mvuto kwa watanzania. Kilichotokea jana, mwenyekiti, kuamua kupiga danadana kwa namna tofauti kwenye skendali ya Escrow. Kusema Mhongo anawekwa kiporo ni kukiangamiza chama. Kushindwa kumwajibisha Maswi moja kwa moja ni kukiua chama. Mbaya zaidi, ni pale alipomwajibisha Tibaijuka ambaye ni mnufaika wa mbali sana katika skendali hii.

CCM kama chama itasema nini mbele ya watanzania?. Kwanini chama kikose mvuto kwajili ya watu wawili?. Nani mwenye ujasiri wa kuinadi CCm mbele ya watanzania wa leo baada ya hotuba ya jana?.
wewe upo dunia ipi JK anataka kuiwa ccm mara ya ngapi wakati ccm imeshakufa siku nyingi sana tunasubiri kuizika 2015 rasmi ..upinzani tunamshukuru sana JK kwa kutusaidia kuiuwa ccm kiulani sana.
 
Katika watu wanaotia aibu wewe huwezi kukosekana jk kaongea mamno ya msingi na yenye mashiko na kuifungua jamii kwa kiasi kikubwa hasa kwa kutoa elimu ya uraia kwa wale ambao walikuwa hawajui undani wake.
 
ktk hili Kikwete unastahili pongezi kubwa. ukawa iko haja ya kumpatia zawadi profesa zawadi ya Xmas na ny
 
wewe upo dunia ipi JK anataka kuiwa ccm mara ya ngapi wakati ccm imeshakufa siku nyingi sana tunasubiri kuizika 2015 rasmi ..upinzani tunamshukuru sana JK kwa kutusaidia kuiuwa ccm kiulani sana.
Jipange vema kwa hayo mawazo yako utasubiri sana inawezekana ukapata ugojwa wa moyo juu ya jambo hili.
 
Kwa hotuba ya jana, ni ukweli usiopingika kuwa;
1. Ukawa ni mpango wa Mungu au,
2. Mwenyekiti wa CCM taifa ni ajenti wa Ukawa ndani ya CCM.
 
Huwa napenda kuwa upande wa upinzani kwahiyo mwakani lazima nijiandae kisaikolojia japo ni ngumu sana kuwa CCM kwasababu kitakuwa chama cha upinzani soon
 
Kikwete kupewa uraisi badala ya Salim Ahmed Salim na UJIO wa "mhehe" mwenzangu Harbinder Sigh Sethi ni MPANGO WA MUNGU. Wenye vichwa vigumu kuelewa wekeni kumbukumbu sawa tukutane January 2016 mtaelewa nachomaanisha
 
mwigulu ulizunguka baadhi ya mikoa unatuambia ni lazima wote waliohusika wachukuliwe hatua na umeona vicheko vya mkuu wa kaya sijui utatuambia nini siku ukipita kwetu tena au ndo haupiti tena?
 
Back
Top Bottom