Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar yalifanyika Januari 1964, na ndipo likaundwa Baraza la Mapinduzi, na kuundwa kwa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, ambapo rais wa Zanzibar ndio Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi!.
Uchaguzi Mkuu wa kwanza wa Zanzibar baada ya Mapinduzi ulifanyika mwaka 1975, kuanzia hapo, Zanzibar ilitawaliwa na seikali ya kidemokrasia ili jina la Serikali ya Mapinduzi, lilibaki kama jina tuu, na Baraza la Mawaziri la Zanzibar, liliendelea kuitwa Baraza la Mapinduzi jina tuu, ambao rais za Zanzibar, aliendelea kuitwa Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi jina tuu!.
Hivyo mpaka leo mpaka kesho, serikali yoyote iliyoko madarakani Zanzibar ni jina lake ni Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, hata bila SUK, kama CUF ingeshinda, then ingeunda Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, na Maalim Seif ndio angekuwa Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi. Hata sasa ndani ya SUK, wajumbe wa CUF walioko ndani ya Baraza la Mawaziri la Zanzibar ni wajumbe wa Baraza la Mapinduzi. Hivyo kama Maalim Seif ameshinda uchaguzi uliofutwa, yeye ndiye atakuwa Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi. Hakuna kipengele chochote kinachozungumzia asili ya Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, kuwa eti kwa kuwa waliopinduliwa ni Waarabu, then Mtu mwenye asili ya Mwarabu, haruhusiwi kuwa Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi!, hata CCM ikimsimamisha mtu mwenye asili ya Kihindi kama Harun Suleiman, then Harun Suleiman ndie angekuwa Mwenyekiti wa BLM!.
Ubaguzi wa aina yoyote, haukubaliki Tanzania, ambapo pia haikubaliki Zanzibar ambayo ni sehemu ya JMT!.
Happy New Year!.
Pasco