Mwenyekiti atishia kwenda kwa Rais mbele ya Waziri Lukuvi

Mzee Abuu akili zake haziko sawa aisee kuna siku Waziri atakula banzi kama mnaweka watu wa aina hii karibu yao. Huyu mzee ana cheti cha ugonjwa wa akili, kaulize pale Kamanga kwa madalali au Villa Park (sijui kama ilifunguliwa tena)

Huyu mzee ni wale walioshiriki kuiua Toto Africans, ni zee lia lia la Yanga huwa Simba ikiingia Mwanza linahaha hadi ifungwe

Kwa mnaokumbuka mwaka jana kwenye kampeni ndo yule mzee alilia Star TV akisema vijana wanataka kuchezea amani ya nchi. Nati zimelegea Mwanza mjini wanamjua vizuri sana
 
Mimi naona waziri yupo sahihi kwasababu huyo mzee ameanza kuweka title ya mzee wake ili asikilizwe, badala ya kuweka taarifa zinazoonesha anastahili hiyo ardhi.....

kwanini aanze mimi ni mtoto wa muasisi wa Tanu?....Waziri ameogopa kuonekana anaoendelea watu ambao ni waasisi wa nchi......

waziri yupo sahihi japo kuna sehemu amekosea anaelekezwa anakuwa kama hataki kusikiliza hiyo inatokana na jamaa kuwa kama amemdharau
Tatizo clip haijaanza mwanzo kabisa, Ila Kuna watu hawawezi kuzungumza bila kufoka, inawezekana ndivyo alivyo, yote kwa yote Kama Kiongozi inapaswa kuwa mwenye hekima Ili uweze kuendana na watu wote
 
Huyu mwananchi amemdharau sana Lukuvi, na kaongea kishari shari sana.

Haya ndiyo matatizo ya dikteta kuhodhi madaraka yote. Wananchi wanaanza kuwaona mawaziri kama takataka tu.

Mitano tena!




Waziri kakosea ilipaswa amsikilize mlipa kodi.Kuonyesha dharau na majivuno ya kuvimbiwa kodi zetu sio uungwana.
 
Waziri hakutakiwa kujibu kwa kejeli "nenda kamuone Rais", hii lugha haijakaa vyema, hata kama ni mna urafiki bado atabaki kuwa Rais.
 
Lakini kwa nini Lukuvi hakutaka kumsikiliza? Usanii umegonga mwamba. Halafu lukuvi anasema "nenda kamuone Rais" ... hasira imemponza
Anamwambia mwananchi kuwa hamuogopi Rais, alitaka aende ila yeye hamsikilizi
 
Ukiitizama hii video kwa makini ukiwa neutral kabisa utagundua huyo mwananchi ana changamoto kidogo ktk akili yake,hana utulivu kabisa.
Ndg Lukuvi alipaswa kuwa mtulivu kwa kuliona hilo angeahirisha kumsikiliza kwa kumuambia tu kwa utulivu wewe jambo lako ni zito tuonane pale ofisini.

Akija ofisini unachukua mabarua yake hayo unamuambia kaa hapo kunywa chai usizungumze,unazisoma ukielewa unatoa uamuzi.
Uongozi ni pamoja na uvumilivu wa kumudu personality za Watu.
 
Kwa wadhifa wake, viwanja na mashamba hapati bila kuwatumia maafisa ardhi. Kama ni hivyo, atawezake kuwakemea wanapokuwa wamekosea? Ndo maana matatizo hayaishi!! Waziri ana viwanja Mwanza, Iringa, Arusha, Dar, etc. Lengo ni nini? HAta kama ni haki yake kama raia, ni vibaya kumiliki rasrimali kwa urafi kiasi hicho! Waziri ukishakuwa mrafi, nani akuamini? Ndo maana kila mtu anatamani kumuona rais. Hawa wasaidizi wake ni urafi uliokithili!

Huu ndio kweli wenyewe, hawa viongozi wakiwa mawaziri,wakuu wa mikoa na wakuu wa wilaya wanawatumia hawa maofisa wa Ardhi kupata viwanja na mashamaba sehemu wanakoongoza!! Inakuwa vigumu sana kuwathibiti maofisa ardhi pale wanapokiuka taratibu na kuwadhulumu wananchi!! Lukuvi is no exception; ana viwanja Mwanza, Arusha ,Dar, Dodoma na mashamba Kilosa!!!! Kwa mtindo huo anatupiga dongo la macho tu pale anapokuwa kwenye TV akiwakaripia maofisa ardhi!!!
 
Ukiitizama hii video kwa makini ukiwa neutral kabisa utagundua huyo mwananchi ana changamoto kidogo ktk akili yake,hana utulivu kabisa.
Ndg Lukuvi alipaswa kuwa mtulivu kwa kuliona hilo angeahirisha kumsikiliza kwa kumuambia tu kwa utulivu wewe jambo lako ni zito tuonane pale ofisini.

Akija ofisini unachukua mabarua yake hayo unamuambia kaa hapo kunywa chai usizungumze,unazisoma ukielewa unatoa uamuzi.
Uongozi ni pamoja na uvumilivu wa kumudu personality za Watu.
LOoo, nimekukubali.

Lakini wewe haya umeyapata kwa msaada wa 'afterthought/hindsight'. Lukuvi hakuwa navyo.

Pengine hata Lukuvi mwenyewe sasa hivi anatamani angefanya hivi unavyopendekeza.
 
Back
Top Bottom