Daudi Mchambuzi
JF-Expert Member
- Nov 25, 2010
- 62,190
- 128,240
Imeipenda UDA wenyewe na tulishauri tangu mwanzo.
Kweli kabisa hiyo ya kuchekechwa ipo sananiliwahi kusikia mtu akisema kuwa madereva hufanya vile ili kuwachekecha watu watoshe vizuri haswa wale wagumu wa kusogea mbele
Kwanza abiria wanakata tiketi, kisha wanasubiri gari zaidi ya saa moja.
Kinachosikitisha ni kuwa baadhi ya vituo havina viti vya kupumzika abiria wala vyoo.
Yaani abiria wa mwendokasi wamekuwa kama watumwa kwani ukisha ingia kituoni huwezi kutoka kwenda kujisaidia nje ya kituo kisha urudi na kuendelea na safari yako.
Endapo ukifanya hivyo lazima ukate tena tiketi, sasa jamani mnategemea watu wajisaidie wapi ilihali wanasubiri magari muda mrefu?
Hawawezi kupanda humo watakosa pumzi sie wenyewe tunapanda kwa vile hatuna usafiri mwingine, yaani wachukue hatua haraka hali sio nzuri kabisa hata maambukizi ya maradhi ni rahisi.Bado tupo nyuma sana, hii yote inatokana na nafasi nyeti za uongozi kushikwa na watu wasio na ubunifu, kwa hali ya kawaida ilipaswa viongozi nao wawe wanasafiri kwa usafiri huo ili kuonja kero zake na kisha kuzifanyia kazi badala ya kusikilizia adha za usafiri huo jamvini
Hawawezi kupanda humo watakosa pumzi sie wenyewe tunapanda kwa vile hatuna usafiri mwingine, yaani wachukue hatua haraka hali sio nzuri kabisa hata maambukizi ya maradhi ni rahisi.
Kwanza abiria wanakata tiketi, kisha wanasubiri gari zaidi ya saa moja.
Kinachosikitisha ni kuwa baadhi ya vituo havina viti vya kupumzika abiria wala vyoo.
Yaani abiria wa mwendokasi wamekuwa kama watumwa kwani ukisha ingia kituoni huwezi kutoka kwenda kujisaidia nje ya kituo kisha urudi na kuendelea na safari yako.
Endapo ukifanya hivyo lazima ukate tena tiketi, sasa jamani mnategemea watu wajisaidie wapi ilihali wanasubiri magari muda mrefu?
Mkuu umenichekesha sana japo havichekeshi.Tukiachana na sauti ya yule dada anayetaja vituo, hakuna kingine cha maana kwenye hayo magari.