Nimekupata mkuu... wewe endelea kutupa data/ushauri kadri unavyoweza. Nashukuru pia kwa namba ya simu... nitamtafuta kesho muda wa kazi.
Mkuu katika wilaya ya Mvomero Morogoro maeneo ya Turiani, kuna vijiji vinavyopakana na wilaya mpya ya kilindi, huko kuna maeneo makubwa sana ambayo ni potential kwa mazao mengi unayoya fahamu, jirani kuna mito kama mto mziha nk. Kwa ujumla kule ndiko viliko vyanzo vingi vya maji kutoka misitu ya tao la mashariki (Eastern Arc Mountain Forets). Hata hivyo ni vizuri kuwahi kwani watu wengi wanaanza kujanjaruka na hivyo yatakuwa bei kubwa zaidi siku za usoni.[/QUOTE
bei gani kwa acre moja?
Kama Isele ya Pawaga kuna maeneo yenye sifa anazotaka mjumbe ni vizuri ukimsaidia, lakini Isele ninayosema mimi ni ya Kilolo karibu na kijiji cha Lulanzi, ni majina tu, kama ilivyo Itimbo ya Kilolo na Itimbo ya Mfindi.
Hivi wewe Malila ni wapi usipopajua nchi hii,kila kijiji unakijua wewe? Tuwe waangalifu lakini wadau tusije tukawa madalali wa kuiuza nchi yetu kama viongozi wetu watukufu (simaanishi napinga wawekezaji) kama ni muwekezaji toka nje ya tz anapaswa kukodishwa tu hiyo ardhi siku wajukuu wetu wakiihitaji wasiwe na haja ya kutafuta AK47 kuipata tena
Hapana mkuu,
Navijua vijiji vichache sana,na kwa sababu mimi ni mkulima inanibidi nivijue ili niweze kulima vizuri. Ukiniuliza biashara nyingine mimi ni mbumbumbu wa kutupwa. Halafu hata kama mimi nitakaa kimya,haiwafanyi jamaa wasiuze nchi yetu, mimi nalima tu mwenyewe. Taratibu zikifuatwa vizuri hakuna shida.
Upo sahihi mkuu Malila kila mtu na eneo lake la kujidai nimeona humu kuna watalaamu hadi wa kuuza vyura,soon ntahamia Mbeya ntawasiliana na wewe usisite kunisaidia kupata shamba la kulima maharage,nataka nijaribu maharage nasikia nayo yanalipa sana
kuna eka 800 morogoro, na eka 6500 mkoa wa Pwani wasiliana nami ktk iyennsemwa@gmail.com kama kuna interest maeneo hayo