Mwanza yarindima mabomu kwenye kesi ya Wenje

Mwanza yarindima mabomu kwenye kesi ya Wenje

Tarehe ya huu waraka kama imekosewa vile, leo ni 14th March, 2016. Hiyo tarehe ya waraka hatujaifikia.
 
Kesi ya kupinga ushindi wa STANSLAUS MABULA iliyofunguliwa na Mh. E. Z. WENJE imeendelea leo.

Upande wa wajibu mashtaka waliweka pingamizi kwenye HATI YA KIAPO ya Shahidi namba Tatu ambaye ni Mh. E. Z. WENJE hivyo kuiomba Mahakama iwape masaa mawili ya kuitolea ufafanuzi.

Baada ya hilo kujitokeza Mahakama ilihairishwa kwa masaa mawili yaliyoombwa, saa Nane mchana Mahakama iliketi upya na kupokea hoja bishwaniwa juu ya HATI KIAPO.

Baada ya pande zote mbili kutoa hoja zake, Mh. Jaji alihairisha kesi hiyo mpaka trh 16 March, 2016 saa tatu asubuhi ambapo aliweka wazi Mahakama kuwa suala hilo haliondoi uhalali wa Mh. E. Z. WENJE kutoa ushahidi wake.

Hivyo inatarajiwa trh 16 March, 2016 Shahidi namba tatu Mh. E. Z. WENJE atatoa ushahidi wake.

Nje ya mahakama wafuasi na wapenzi wa CDM walikuwa wengi sana waliokuja kusikiliza kesi hiyo, hivyo kulazimika Mwanasheria ERICK MUTTA kutoa ufafanuzi wa kilochoendelea mahakamani na kuwaomba wafuasi na wapenzi hao wa CDM kutawanyika kwa AMANI.

Katika hali ya kushangaza Askari wa Jeshi la Polisi waliziba njia nakuanza kuwashambulia kwa virungu na mbwa hata kupelekea majeraha makubwa kwa baadhi ya wafuasi hao, Hali iliyopelekea Mh. E. Z. WENJE Kuingilia kati na mabishano makubwa kuzuka, ilikuwa ni dhahama kubwa na mpaka hivi sasa Mwanachama mmoja ambaye jina Lake halijapatikana amekimbizwa Hospitali kwa Gharama za Mh. E. Z. WENJE.

TUKUTANE TENA MAHAKAMANI JUMATANO trh 16 March, 2016 saa tatu asubuhi.


ERICK MUTTA.
MWANASHERIA,
Bavicha Nyamagana.
MWANZA
16 Marchi, 2016.
Wenje ataendelea kuwatumia kwa kesi ambayo majibu yake anayajua.
 
Ila hapo sina uhakika kama haki itendeka kwasababu naona mr Hapa kazi amekuja lasmi kwaajili ya kuupoteza upinzani.
Siasa ni pesa, na upinzani wameshapata mgodi wa pesa (kwa ongezeko kubwa la wabunge) hivyo upinzani kufa sahau kwasasa.
 
.............anayestaili hofu apewe hofu.........lema
 
......kuna haja gani ya kuwa na mbunge ambaye hata wananchi hawataki kumuona akipita ......mimi huwa najiuliza huyu mabula huwa haoni aibu.....
 
Serikali sikivu na jeshi la polis sikivu kwa ccm nimekosea hakuna jeshi linalojihusisha na siasa hao ni wafuas wa ccm waliovaa nguo za polis kwa kod za umma kutekeleza matakwa ya mtawala wao hawako kwa ajili ya haki wao ni wabomoaj wa haki

unawaone polisi, wanapokea amri na kuzitekeleza bas ndo kazi yao na ndo wanapopatia mkate wao
 
Kaka tushapambana sana kuhakikisha ccm inatoka madarakani lakini tatizo walituzidi kwa tikitaka

Mimi ni moja ya watu ambae Kura yangu haijaenda ccm
Kuanzia mbunge diwani rais hadi serikali ya mtaa Leo sio siri zote
Nilizichapa kwa viongozi wa ukawa
Mkuu hongera sana mimi mwenyewe nilipiga Hat trick ya UKAWA namshukuru Mungu nikashinda kwa kumpata Msigwa na diwani toka Ukawa nimepoteza ile ya mauzauza tu na huu mwendo ni miaka yote hawa ccm hawatopata kura yangu kamwe.
 
Hivi kama Mungu angetulaani na chadema kushinda, mngetumia wapi?? Au red brigade??
Hivi kama Mungu angetulaani na chadema kushinda, mngetumia wapi?? Au red brigade??
Kununua magari 779 ya kuwakabili wananchi ili kulazimisha kutawala tena na kuwaacha wamama wajawazito vijijini wakifa na pia wanafunzi wakikaa chini kwa kukosa madawati ipi ni LAANA?
Laanakhum nyie!
 
Back
Top Bottom