Mwanaume unakaa na mkeo kila saa kama jiwe la honge

Mwanaume unakaa na mkeo kila saa kama jiwe la honge

Mwabhleja

JF-Expert Member
Joined
Jan 27, 2016
Posts
1,369
Reaction score
2,105
Najua kila mmoja ana namna ya kuishi. Pamoja na hayo nimeona vema nikawakumbusha ndugu zangu waliofungwa na vifungo vigumu vya ndoa au uchumba.

Nimeamua kuandika huu uzi nikiamini kwamba rafiki yangu Bernard atapita huku na atajifunza kitu. Juzi tulikuwa kona fulani hivi tukila mbuzi katoliki maeneo ya California, Nyegezi jijini Mwanza huku tulivuta taswira ya mazingira ya Fiesta.

Mshikaji nilimpigia toka alhamisi kwamba nitakuwa Mwanza. Sasa ile jioni mishale ya saa kumi na moja nikampigia. Jamaa akaomba excuse eti hawezi kutoka home maeneo ya Pepsi maana mkewe hatomruhusu maana hajamzoesha kutoka mida hiyo.

Nikasema Fresh kama Fareed Kubanda.
Ile kuendelea na michapo Mara meseji mshikaji anadai sorry mwanangu natamani sana tuonane maana huu mwaka wa tano tangu tuachane chuo. Nikaona huyu siyo mchizi kama Mox, nikabadilisha line kuendeleza stori Tatu tofauti kama J Mo.

Nilichogundua ni kwamba wanaume wengine siyo Mashine kama alivyo Msaga Sumu ila wanaibiwa kama Rayvanny.

Wewe ni wa kuamka na kwenda kazini, ukirudi nyumbani tu.
Hunywi pombe, huchezi bao, huchezi draft, huchezi pool table, si mshabiki wa mpira n.k

Wewe unajitafutia ugonjwa mbaya sana kuliko hata ubaya wa Baba ubaya.
Yaani wewe ukifukuzwa kazi gafla utakufa mapema kama funza maana huna stamina kama za mchwa kwa kuwa unajitenga na wadau.
Suala LA kujumuika ni kikatiba. Hivi kila SAA wewe na mkeo mnaongea nini?
Kutana na kina mhogo mchungu huku kwenye draft upigwe supa au umpige MTU force king wote mcheke akili iwe poa.

Ndiyo maana mnahangaika Mara nguvu kiume zimepungua, zitaachaje kwa mfano?

Isitoshe kinachopungua hapo siyo nguvu za kiume bali AKILI YA KIUME.
Miaka ile ulikuwa machachari, pita huku na kule tazama maua akili inafurahi ukikutana na mpango wa kando saaafi kama Kenya lakini sasa unashinda nyumbani kila SAA kama jiwe la Honge umerogwa?

Hata mwenza wako mpe muda hata kama anakung'ang'aniza kimbia fasta kama Babuu wa Kitaa ila usichelewe sana kurudi walau SAA mbili na nusu au Tatu rudi home.
Akizoea atakufurahia vinginevyo utalazimishwa kuangalia Picha za kihindi ukiaminishwa mwishoni Kali sana lakini Mara zote utaishia pahala steringi anafia kwenye maua kama nyuki wa kwenye mashamba ya Tumbaku kule Kaliua!
Zamani ushauri kama huu nilikuwa nauza 250/= Tzs lakini saizi ni bureeee. Siyo bure kama ya mtandao wa simu kwamba nunua vocha ya 1000 upate dakika 15 za bure mitandao yote msg 500 na mb 10.
Huu ushauri ni bure kweli kweli. Ukiona unakufaa uchukue mapema kama CCM lakini ukiona haukufai upotezee kama Masanja.

Alarmed!
 
Wew hujajua tu kuna kitu anakipata kwa mkewe kutokana na mpenz, sasa kama mtu anapata kila kitu ataenda kuzurura ili iweje
Mwanaume mashine hawezi pata kila kitu kwa mkewe.
Usione watu wanapack magari na kujumuika kwenye vijiwe vya bao,draft,bar au kahawa ukadhani wajinga.
Hili ni suala LA kisaikolojia na afya ya akili
 
Ujue hata wewe wanakushangaaa unaowashangaaa. Sio lazima kila kitu kiwe kama unavyotaka kila mmoja ana namna ya! Kujumuika, wengine huenda church kujumuika na sio lazima kwenye starehe. Mnapishana mitazamo hilo halikuweki kua sahihi mkuu.
 
Mwanaume mashine hawezi pata kila kitu kwa mkewe.
Usione watu wanapack magari na kujumuika kwenye vijiwe vya bao,draft,bar au kahawa ukadhani wajinga.
Hili ni suala LA kisaikolojia na afya ya akili
Aiseeeeeeee
 
Ukikaa sana mkeo ndo unakuta jamaa anaanza kujifunza tabia za umbeya umbeya, mwishowe anaambiwa na mkewe akune nazi.
[emoji134] [emoji134] [emoji134] [emoji134]
 
Nilianza kuusoma uzi kwa makini mpaka nilipofikia sehemu ya kitimoto, nikasema anhaa kumbe huyu ni katika waleeee, ......Basi sawa
 
Mwanaume asiye penda kutoka lazima atakuwa na hobby yake, wengine wanapenda video/computer games, kusoma vitabu, kuangalia mpira nk. Si kuwa kila saa wanaongea na wake zao.

Mwanamke jukumu lake ni kuweka mazingira ya nyumbani yawe masafi na yaliyotulia. Wanaume wengine wana kuwa kwenye utaratibu huu hata kuanza kuaga anatoka mkewe anashangaa.
 
Kuna kitu cha kujifunza hapa,ngoja nufuatilie,
kila kitu ni kamali siku hizi na dini zetu haziruhusu.
 
Back
Top Bottom