naomba kuiliza hivi mwanaume kwa nini anaenda nje ya ndoa na siyo na mwanamke mmoja wengi tu,na mke anampa kila kitu (starehe) na kumridhisha na kumpenda kwa dhati lakini mwanaume ndo hatulii y y y ?
Duh!Anyway nina majibu binafsi lakini ngoja nisubiri walioko kwenye ndoa waje waseme shida inayowapelekea wafanye hayo!
naomba kuiliza hivi mwanaume kwa nini anaenda nje ya ndoa na siyo na mwanamke mmoja wengi tu,na mke anampa kila kitu (starehe) na kumridhisha na kumpenda kwa dhati lakini mwanaume ndo hatulii y y y ?
Hapo tu ndio huwa kunakuwa na utata hasa bibiye akishakuwa VETERAN ndani ya nyumba. Yaani akisha kuwa ndani ya nyumba kwa miaka mitano na kuendelea. Kinamama wengi wanaanza kutoa dozi za ile shughuli yetu kama wanavyotoa dozi za dawa ya minyoo kwa watoto. Wengine wakiombwa huduma ndio kabisa wanajifanya kushangaa kwa nini mzee ana hamu na shughuli utadhani hawajui wajibu wao ndani ay nyumba.
jamani achaneni na huyo kiumbe anayeitwa mwanaume, hawaeleweki utampa huduma zote anazostahili, na wakati mwingine wewe ndio unamuomba mfanye lakini bado anahangaika tu. ni ushenzi tu walionao ndio maana ukimwi hauishi. mnauthi kweli nyie wanaume.
jamani achaneni na huyo kiumbe anayeitwa mwanaume, hawaeleweki utampa huduma zote anazostahili, na wakati mwingine wewe ndio unamuomba mfanye lakini bado anahangaika tu. ni ushenzi tu walionao ndio maana ukimwi hauishi. mnauthi kweli nyie wanaume.
Acha jazba na matusi hayasaidii. Hii kitu ipo kwenye damu. Wewe unadhani tatizo kupewa? La hasha... Alianza Babu yako... akaja Baba yako Sasa unamshangaa nini mumeo?
kwa hiyo hata wewe inaonekana una mwanamke nje ndio maana unaitete, muogopeni mungu nyie viumbe.
Yaani wanaohangaika kutafuta wanawake /kutongozatongoza ni waume za watu why?
Asa da mkubwa mi si mwanaume ninayejua walichofanya babu zangu na baba zangu? mi nikiwaigilizia nimekosa nin?
aaha kumbe leseni yao ni kwa wote eeh?tayari wana leseni za kudrive na ni experienced bebii!
mhh! mtatuua kwa mapresha ya kutuletea mitoto ya nje.