Meridah Tough
Senior Member
- Nov 27, 2017
- 136
- 363
Habari wana jf?
Kwa kweli nianze kwa kutoa dukuduku langu kwa wanaume baadhi ambao hawana msimamo.
Sifa ya kwanza ya mwanaume kwangu mimi ni kuwa na msimamo. Ujue nini unataka. Ujue kufunga na zipu yako.
Yaani hapa kuna ex wangu mmojawapo hana msimamo kabisa. Anahitaji kuwa na mimi na hapohapo anahitaji kuwa na mwanamke mwingize, wawili zaidi yangu. Hata tukiachana leo, kesho mkakutana tu anaanza kutengeneza mazingira ya kurudiana.
Kutokuwa na msimamo kunawafanya wanaume wengi kushindwa kuwasaidia wapenzi wao wa dhati kwa kigezo kuwa hawajawaoa. Unakuta mwanaume ana wanawake 6, wote hao anawadanganya hovyohovyo tu, analipia guest, chakula, vinywaji nk. Unakuta pesa yote ambayo ungeweza kuhifadhi kwa ajili ya future yako au kumsupport mwenzako inaishia kwenye kula na kunywa na kulipia vyumba tu.
Kutokuwa na msimamo kunapelekea wanaume kuwapelekea wanawake wanaowapenda magonjwa hatarishi kama UKIMWI. Mwanaume hujielewi, mradi mwanamke amekuchekea basi unapita naye.
Mwaka jana kuna mdada alikuwa anafanya kazi saluni moja hivi. Bahati mbaya alikuwa muathirika. Kwa kuwa alijua hali yake, basi aliambukiza kwa makusudi. Ukienda saluni hapo na bae wako, huyo dada atajiongeza mwenyewe jinsi atakavyoonana na mwenzako mradi ameshamuona na kumjua. Atamtafuta na kumtega anavyoweza. Wale waliokosa misimamo wanaangukia pua.
Leo niishie hapa. Lakini wanaume mnapaswa kuwa na misimamo. Siku hizi hakuna wanaume wenye misimamo kabisa na kama wapo ni wachache sana.
Kwa kweli nianze kwa kutoa dukuduku langu kwa wanaume baadhi ambao hawana msimamo.
Sifa ya kwanza ya mwanaume kwangu mimi ni kuwa na msimamo. Ujue nini unataka. Ujue kufunga na zipu yako.
Yaani hapa kuna ex wangu mmojawapo hana msimamo kabisa. Anahitaji kuwa na mimi na hapohapo anahitaji kuwa na mwanamke mwingize, wawili zaidi yangu. Hata tukiachana leo, kesho mkakutana tu anaanza kutengeneza mazingira ya kurudiana.
Kutokuwa na msimamo kunawafanya wanaume wengi kushindwa kuwasaidia wapenzi wao wa dhati kwa kigezo kuwa hawajawaoa. Unakuta mwanaume ana wanawake 6, wote hao anawadanganya hovyohovyo tu, analipia guest, chakula, vinywaji nk. Unakuta pesa yote ambayo ungeweza kuhifadhi kwa ajili ya future yako au kumsupport mwenzako inaishia kwenye kula na kunywa na kulipia vyumba tu.
Kutokuwa na msimamo kunapelekea wanaume kuwapelekea wanawake wanaowapenda magonjwa hatarishi kama UKIMWI. Mwanaume hujielewi, mradi mwanamke amekuchekea basi unapita naye.
Mwaka jana kuna mdada alikuwa anafanya kazi saluni moja hivi. Bahati mbaya alikuwa muathirika. Kwa kuwa alijua hali yake, basi aliambukiza kwa makusudi. Ukienda saluni hapo na bae wako, huyo dada atajiongeza mwenyewe jinsi atakavyoonana na mwenzako mradi ameshamuona na kumjua. Atamtafuta na kumtega anavyoweza. Wale waliokosa misimamo wanaangukia pua.
Leo niishie hapa. Lakini wanaume mnapaswa kuwa na misimamo. Siku hizi hakuna wanaume wenye misimamo kabisa na kama wapo ni wachache sana.