Mwanangu Mwanauba, jifya moja haliinjiki chungu

Mwanangu Mwanauba, jifya moja haliinjiki chungu

SUZANE

JF-Expert Member
Joined
Oct 26, 2010
Posts
740
Reaction score
502
Nawapenda wote!!
Ni juzi tu nilialikwa kwenye kitchen party ya jirani yangu Mwanauba, nilijuta kwanini nilikwenda maana nilijikuta nikipoteza raha yangu yote.....

Mama mmoja ambaye alialikwa kumfunda Mwanauba alikuwa akiongea maneno ambayo yalikuwa yakiniuzi kila alipoendelea kuongea, nilitembeza macho yangu huku na huku kutizama wenzangu kama walipokeaje yale mahusia ya kungwi kwa bibi harusi Yule mtarajiwa, chakushangaza watu walikuwa na furaha ya ajabu, hasa wanawake waliokwenye ndoa wa pale mtaani, walishangilia na kupiga vigelegele za shangwe!!

Moyoni sikuona kama huo ndio ulikuwa wakati muafaka wakusemea maneno yale pale ukumbini, nilidhani mambo ya ndani watakua wameshamwambia Mwanauba na pale ukumbini ni kuserebuka tu Utamu wa Yesu!!

Alianza hivi, “Mwanangu Mwanauba ukibeba ndoo ubebe na kidumu mkononi, kuna bahati mbaya mwanangu waweza jikwaa ndoo ikaanguka na maji yakamwagika ukabaki na kidumu kikakufaa kuoshea vyombo, kumbuka siku zote chombo hakiendi ila kwa nyenzo mwanangu, Mwanauba mkono mmoja hauchinji ng'ombe hata siku moja kaa ukijua hilo mwanangu, hakika Mwanauba…tendegu moja halisimamishi kitanda tumia akili!!

Watu walipiga kelele za furaha wakati kungwi Yule akimalizia na kusema hivi, mwanangu Mwanauba namalizia na kusema hivi, “jifya moja haliinjiki chungu, sharti matatu ili chungu kikae vema jikoni” asante MC asante sana!!!

Mie nilibaki hoi nikijiuliza hawa makungwi wanatufundisha nini?? Wanaifundisha nini jamii?? Je Mwanauba jirani yangu amejifunza kitu gani pale!! Mbona wakina mama nanihii walikuwa wakishangilia sana na kupiga vigelegele kwa kuonyesha waliambiwa kitu ambacho wanakifanya au walitamani kukifanya hivyo walikosa mshauri tu!!

Baada ya sherehe nilijirudia zangu nyumbani kwangu kama shomoro alienyeshewa na mvua!!

Nawatakia wakati mwema rafiki zangu!!
 
Ndo wawafundishe na kondomu, vinginevyo tutazikana sana!
 
Ndo wawafundishe na kondomu, vinginevyo tutazikana sana!
mtu katoka huko kutafuta utamu wa pipi ,atakubali kula hiyo pipi na maganda yake sasa?
dunia hii..kuna moja nilienda ,,mmmh wanafundishwa jinsi ya kupika k bibi? nikasema hizi cancer za vizazi hizi ndo maana zinaongezeka? toka lini k ikaungwa kama pilau? eti iwe tamu fyooooooo!
 
mtu katoka huko kutafuta utamu wa pipi ,atakubali kula hiyo pipi na maganda yake sasa?
dunia hii..kuna moja nilienda ,,mmmh wanafundishwa jinsi ya kupika k bibi? nikasema hizi cancer za vizazi hizi ndo maana zinaongezeka? toka lini k ikaungwa kama pilau? eti iwe tamu fyooooooo!
unaijua na ile yakufokonyeza asali k inawaka moto ,babu akija anaishia kulia tu usishangae hayo maasali wanayofokomeza yamechanganywa na mafuta ya breki au ya transfoma ukilipuka kisa unatengeneza joto ya k kwiwkwiwkwiwkwiwkwiwwkwiwkwiwkwi Smile leka na na ulana lu monomao
 
Last edited by a moderator:
K yenyewe unahangaika kumpikia Marioo?

Kazi kweli kweli

mtu katoka huko kutafuta utamu wa pipi ,atakubali kula hiyo pipi na maganda yake sasa?
dunia hii..kuna moja nilienda ,,mmmh wanafundishwa jinsi ya kupika k bibi? nikasema hizi cancer za vizazi hizi ndo maana zinaongezeka? toka lini k ikaungwa kama pilau? eti iwe tamu fyooooooo!
 
unaijua na ile yakufokonyeza asali k inawaka moto ,babu akija anaishia kulia tu usishangae hayo maasali wanayofokomeza yamechanganywa na mafuta ya breki au ya transfoma ukilipuka kisa unatengeneza joto ya k kwiwkwiwkwiwkwiwkwiwwkwiwkwiwkwi Smile leka na na ulana lu monomao
kwiii kumbe na wewe ulishasikia eeh ,ujue ndo maana wanawake wengi hata mirija ya uzazi inaziba ..kuingiza ingiza mavitu huko ....... siwezi hata chumvi mie asietaka na asile
 
Haya ndo matatizo ya hizo kitchen party wanashauri ufanye wanayofanya wao kwenye ndoa/maisha yao..yafaa kila mtu aishi maisha ya ndoa anayoyataka yeye mwenewe ni shida kubwa watu kulazimisha ndoa zao zifanane na za wengine.
 
Ungefanya tathmini fupi lau ya rika la waliokuwa wakishangilia ungepata jibu kwani kuna watua ambao ndoa kwao ni sawa na suala rahisi na la kawaida sana
 
Haya ndo matatizo ya hizo kitchen party wanashauri ufanye wanayofanya wao kwenye ndoa/maisha yao..yafaa kila mtu aishi maisha ya ndoa anayoyataka yeye mwenewe ni shida kubwa watu kulazimisha ndoa zao zifanane na za wengine.

nadhani, nahisi, nafikiri kuna kitu ama jambo zaidi ya hiliunaloliwaza wewe!! we subiria tu utaona badae hapa hapa, wana ong'wa kulwa!!!
 
Haya ndo matatizo ya hizo kitchen party wanashauri ufanye wanayofanya wao kwenye ndoa/maisha yao..yafaa kila mtu aishi maisha ya ndoa anayoyataka yeye mwenewe ni shida kubwa watu kulazimisha ndoa zao zifanane na za wengine.

nadhani, nahisi, nafikiri kuna kitu ama jambo zaidi ya hiliunaloliwaza wewe!! we subiria tu utaona badae hapa hapa, wana ong'wa kulwa!!!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom