DOKEZO Mwanangu ameuawa kwa kupigwa na Mwalimu lakini kesi inazungushwa

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
Changamoto ni yy mwenyewe mama huyu nimemuomba hiyo namba ya simu ya mtu ambaye waliongea naye Ili nimhoji, naisubiri tangu asubuhi.

Sent from my CPH2207 using JamiiForums mobile app
Ok Mkuu ngoja tumsubiri lakini hili jambo Mh Waziri unapaswa kulifatilia kwa ukaribu na kujua huyo aliyewasiliana nae ni nani na walio husika lazima wafikishwe kwenye vyombo vya usalama! Mtoto awezi kufa halafu tukanyamaza tuu na ikaisha tuu lazima kuna ukweli na kuna uongo maana najua kwa hali aliyo nayo ni kama kachanganyikiwa bila shaka wewe unaweza kufanya juhudi za kuhakikisha unapata mawasiliano yake na una ujua ukweli na ikiwezekana ukae uongee nae najua wajua fika uchungu wa kupoteza mtoto!
 
Halafu hakurudi kwangu, kwamba alipiga akaniambia nikasema Rudi tena huko, siyo kweli. Unaweza kusoma maelezo yangu tafadhali na baada ya mm kushangazwa na taarifa hizi nikamtafuta. Uzuri mm nawasiliana na wote kwa sms Ili kutunza Kumbukumbu zisaidie baadae.

Sent from my CPH2207 using JamiiForums mobile app
Mh Waziri nimekuelewa sana pengine kuna sehemu amekosea naomba usamehe na ujue kuwa ambacho unaweza msaidia ni yeye kupata haki yake ya kujua ukweli na kupata fursa ya kuongea nae na kumfariji maana kwa hali aliyonayo lazima kuna kuchanganyikiwa…Mtoto amefariki cha kumsaidia ni kuhakikisha anapata msaada na unaongea nae….! Tunaomba unsaidie wewe ni Mama na unajua mtoto anavyo uma wengi huvurugwq!
 
Kifupi sijaongea naye naye anashangaa. Nisaidie kumuuliza ameongea na nani maana mm nasubiri hiyo namba tangu asubuhi. Ukweli uko kwenye tamko la Polisi kuwa watuhumiwa wako ndani.

Sent from my CPH2207 using JamiiForums mobile app
Tunashukuru kwa kuja kujibu hapa chamsingi tunaomba ufatilie hili jambo hadi mwisho ujue limefikia wapi na ikiwezekana uonane na mfiwa ujue na umfariji! Kwenye hizi kazi kuna kusingiziwa kwa hiyo usichoke ndio kazi ya Umma! Tunaomba umsaidie
 
Vyote hivyo ni uongo. Kwa kuwa mm huwa siongei na simu daima, mm natumia sms tu. Muulize alimpigia nani Ili labda tukaombe kumbukumbu za sauti na ikionekana siyo mm iweje? Maana nimemuomba namba husika tangu asubuhi sijapewa. Ila ukweli ni kwamba, watuhumiwa wako ndani na yy amekiri anajua, na ameshangaa haya maneno yametoka wapi.

Sent from my CPH2207 using JamiiForums mobile app
Nilitaka kushangaa hizi tuhuma juu yako maana nakujua vizuri.Binafsi mwaka jana nilikuwa na shida nikakutumia sms usiku saa nne usiku nilishangaa kuona unanijibu.Upo vizuri sana kufatilia mambo yanayohusu wizara yako maana ni nadra sana kumuona Waziri anajibizana na wananchi tena kwa sms .Big up sana dada.
 

Naitwa Janeth Shayo, mkazi wa Uru, Moshi. Naomba unisaidie kupaza sauti mwanangu Jonathan Makanyaga (07) mwanafunzi wa darasa la kwanza shule ya msingi Mrupanga, ameuawa kwa kupigwa na Mwalimu lakini kesi inataka kupindishwa.

Tar.28/02/2024 mwanangu alienda shuleni akiwa mzima. Alipofika aliadhibiwa kwa kuchelewa "namba". Alipoingia darasani alianza kutokwa damu puani na mdomoni. Akarudishwa nyumbani. Nilipomkagua nikamkuta na majeraha yaliyovilia damu mgongoni, kwenye mbavu na mguuni.

Kesho yake nikaenda nae shuleni kutaka kuoneshwa mwalimu aliyemfanyia ukatili mwanangu. Lakini Mwalimu mkuu akaomba nibaki nje. Akaingia na mwanangu ofisi ya walimu na kumtaka amtambue Mwalimu aliyemuadhibu. Mwanangu akamtanbua. Mwalimu Mkuu akaniambia wameshamfahamu ni mwalimu wa "Field" hivyo atazungumza nae.

Wakanipa 20,000/= za matibabu. Nikampeleka mwanangu zahanati. Kesho yake akazidi kutoka damu, na kulalamikia maumivu sehemu za mbavu. Nikampeleka hospitali ya masista. Daktari akaniambia bandama imejeruhika ndio sababu ya kutoka damu mdomoni. Mtoto alidai pamoja na viboko alivyochapwa, Mwalimu pia alimpiga ngumi tumboni. Huenda ndiyo iliyopasua bandama.

Hali yake ilizidi kuwa mbaya tukapewa rufaa kwenda KCMC. Akatakiwa kufanyiwa upasuaji. Gharama 350,000/= lakini sikuwa nayo. Nikapiga simu shuleni wakasema tuombe afanyiwe halafu watalipa baadae. Hata hivyo kabla hajafanyiwa hali yake ikazidi kuzorota, akashindwa kupumua, akawekwa kwenye Oxygen. Akashindwa kula, akawekewa mpira wa chakula. Baada ya siku chache akafariki 😭.

Lakini ripoti ya hospitali inasema mwanangu amekufa kwa kansa ya damu. Kansa gani ya damu inayomuua mtoto kwa wiki mbili? Na kwanini hiyo kansa itokee baada ya kuadhibiwa shuleni? Kwanini Mwalimu aliyemuadhibu mwanangu anafichwa, na sipewi haki ya kumfahamu?

Nalazimishwa nichukue maiti nikazike lakini nimekataa. Nataka uchunguzi huru. Nimeenda dawati la jinsia kulalamika nikapuuzwa. Nimepiga simu kwa Waziri Dkt. Gwajima D akanipa namba ya mtu wa kunisaidia. Nilipopiga kumbe ni yuleyule Mkuu wa dawati la jinsia aliyenipuuza. Nikamrudia Gwajima akasema niwasiliane nae huyohuyo. Nimekosa pa kulilia haki ya mwanangu Jonathan
Toa ripoti hii kwenye vyombo vya juu; ni ukatili sanba kukatisha maisha ya mtoto wa miaka saba ambaye bado alikuwa na dunia yite mbele yake. \
 
Hapa ni shutuma za kutengenezwa kwa makusudi. Kwanza, sijawahi ongea naye, mawasiliano yangu ni sms , kwenye ukurasa wake hakuna maneno aina hiyo, naye anajua kuwa, watuhumiwa 5 wako ndani. Na baada ya kumpigia kuongea naye imekuwaje, naye anashangaa, nimeomba simu aliyopiga au kupigiwa anipe, tangu asubuhi hajanipa. Humu duniani, tuvumiliane tu...View attachment 2935524View attachment 2935525

Sent from my CPH2207 using JamiiForums mobile app
Shikamoo Dr. gwajima nimefarijika kumbe umekuwa mtu wa watu kiasi hiki hadi unachati na sisi huku..Naomba tu kubali salamu yangu najua inaenda kubadili ktu kwenye maisha yangu kitakacho acha alama🙏🙏
 
Huyo dokta na huyo mkuu wa dawati wote sasa hivi wanafaa waachie ngazi maana hakuna walichokifanya.

Dkt. Gwajima D unatakaiwa kuwajibika kwa kuachia ngazi maana kama mtumishi wako hafanyi kile kinachotakiwa, hata wewe bosi wake utakuwa ni sehemu yake. Hapo ulipo upo kwa kodi za wananchi na ushukuru kuwa tanzania hakuna utawala wa sheria maana kibarua, na ndani kungekuhusu katika nchi za wenye akili
Nafikiri kashatoa majibu kwenye post za nyuma na ametoa maelezo mengi tuu unapaswa kusoma na amesema ana fatilia na ana subiri majibu ya mtoa taarifa na atamtafuta!
 

Naitwa Janeth Shayo, mkazi wa Uru, Moshi. Naomba unisaidie kupaza sauti mwanangu Jonathan Makanyaga (07) mwanafunzi wa darasa la kwanza shule ya msingi Mrupanga, ameuawa kwa kupigwa na Mwalimu lakini kesi inataka kupindishwa.

Tar.28/02/2024 mwanangu alienda shuleni akiwa mzima. Alipofika aliadhibiwa kwa kuchelewa "namba". Alipoingia darasani alianza kutokwa damu puani na mdomoni. Akarudishwa nyumbani. Nilipomkagua nikamkuta na majeraha yaliyovilia damu mgongoni, kwenye mbavu na mguuni.

Kesho yake nikaenda nae shuleni kutaka kuoneshwa mwalimu aliyemfanyia ukatili mwanangu. Lakini Mwalimu mkuu akaomba nibaki nje. Akaingia na mwanangu ofisi ya walimu na kumtaka amtambue Mwalimu aliyemuadhibu. Mwanangu akamtanbua. Mwalimu Mkuu akaniambia wameshamfahamu ni mwalimu wa "Field" hivyo atazungumza nae.

Wakanipa 20,000/= za matibabu. Nikampeleka mwanangu zahanati. Kesho yake akazidi kutoka damu, na kulalamikia maumivu sehemu za mbavu. Nikampeleka hospitali ya masista. Daktari akaniambia bandama imejeruhika ndio sababu ya kutoka damu mdomoni. Mtoto alidai pamoja na viboko alivyochapwa, Mwalimu pia alimpiga ngumi tumboni. Huenda ndiyo iliyopasua bandama.

Hali yake ilizidi kuwa mbaya tukapewa rufaa kwenda KCMC. Akatakiwa kufanyiwa upasuaji. Gharama 350,000/= lakini sikuwa nayo. Nikapiga simu shuleni wakasema tuombe afanyiwe halafu watalipa baadae. Hata hivyo kabla hajafanyiwa hali yake ikazidi kuzorota, akashindwa kupumua, akawekwa kwenye Oxygen. Akashindwa kula, akawekewa mpira wa chakula. Baada ya siku chache akafariki 😭.

Lakini ripoti ya hospitali inasema mwanangu amekufa kwa kansa ya damu. Kansa gani ya damu inayomuua mtoto kwa wiki mbili? Na kwanini hiyo kansa itokee baada ya kuadhibiwa shuleni? Kwanini Mwalimu aliyemuadhibu mwanangu anafichwa, na sipewi haki ya kumfahamu?

Nalazimishwa nichukue maiti nikazike lakini nimekataa. Nataka uchunguzi huru. Nimeenda dawati la jinsia kulalamika nikapuuzwa. Nimepiga simu kwa Waziri Dkt. Gwajima D akanipa namba ya mtu wa kunisaidia. Nilipopiga kumbe ni yuleyule Mkuu wa dawati la jinsia aliyenipuuza. Nikamrudia Gwajima akasema niwasiliane nae huyohuyo. Nimekosa pa kulilia haki ya mwanangu Jonathan
Inasikitisha sana huyo mwalimu achukuliwe sheria.
 
Hakuna mwalimu anayeweza kumpiga mtoto ngumi tena mtoto wa darasa la kwanza, huyo mtoto labda alipigana na wenzake au alipata ajali, uchunguzi wa kina ufanyike. Kuchelewa namba hakuwezi kumfanya mwalim ampigie mtoto ngumi ya tumboni.

Nimulize kitu hapa.

Siku hiyo adhabu ilipotekelezwa na huyo mwalimu kwa marehemu je ni wanafunzi wangapi walikuwa wamechelewa namba?

Hiyo ngumi alipigwa huyo marehem tu au walipigwa wanafunzi zaid ya huyo marehemu?

Hiyo adhabu ilitolewa katika mazingira gani? ili ushahidi uwe wa kina zaidi

Zaidi ya yote niseme kwamba, poleni sana wazaz, ndugu, jamaa na wote tulioguswa na msiba huu. Mungu amrehemu marehemu! Amina.

Ficha ujinga wako basi.
 
Upo Bongo? Nikuambie. Mwaka 2018 nilikwenda shule fulani yenye chekechea kuulizia nafasi ili nimwandikishe mwanangu. Nilichokutana nacho kiliniacha mdomo wazi. Nilikuta mwalimu wa kike anampiga mtoto wa chekechea fimbo kama anaua nyoka. Take it from me. Nikaghairi na mama yake akampeleka shule nyingine. Nikawa nimesafiri kikazi. Nikiwa ugenini mke wangu akanijulisha kuwa mtoto analia sana kila asubuhi basi linapokuja kumchukua na hataki kwenda shule. Kisa? Kipigo. Ni mtoto wa chekechea ukumbuke. Nikamwambia afuatilie shuleni. Kwenda waalimu wakamwambia hii shule fimbo ni lazima. Hapa wazazi wanatusifu na wametupa ruhusu watoto wachapwe. Kama wewe hutaki wako achapwe, basi ondoka naye. Nilichoka kweli kweli. Nikamhamishia shule nzuri na nikatoa masharti kuwa sitaki apigwe. Wakanihakikishia kuwa wao hawapigi. Na kweli alisoma kwa amani. Tanzania yote hizi shule za Kayumba waalim wanaamini kuwa huwezi kumfundisha mtoto bila kiboko..... kuanzia chekechea.
Umeongea vizuri, ila kusema hutaki mwanao asipigwe nimebaki mdomo wazi. Basi wewe ni tofauti na mimi, mimi nina watoto wanasoma hizi kayumba zilizochangamka (English medium) tena ya dini . Wakati nampeleka wa kwanza wakaniambia kuna wazaz walisema hawataki watoto wao wachapwe. Mimi nilisema wa kwangu akikosea achapwe la sivyo ntamhamisha. Mimi sina imani ya kulea mtoto km mayayi. Muhimu "aadhibiwe siyo kupigwa". Mimi mwenyewe hata nyumbani wanakula makofi kila wakifanya upuuzi achilia mbali fimbo.

Ila ktk malezi kila mtu na style yake bwana hamuwezi kufanana wote. Ni sawa tu na kuendesha maisha ya ndo, kila mwanaume ana mfumo wake.
 
Ok Mkuu ngoja tumsubiri lakini hili jambo Mh Waziri unapaswa kulifatilia kwa ukaribu na kujua huyo aliyewasiliana nae ni nani na walio husika lazima wafikishwe kwenye vyombo vya usalama! Mtoto awezi kufa halafu tukanyamaza tuu na ikaisha tuu lazima kuna ukweli na kuna uongo maana najua kwa hali aliyo nayo ni kama kachanganyikiwa bila shaka wewe unaweza kufanya juhudi za kuhakikisha unapata mawasiliano yake na una ujua ukweli na ikiwezekana ukae uongee nae najua wajua fika uchungu wa kupoteza mtoto!
Tukisoma taarifa ya Jeshi la Polisi kipenge cha 3, tutaona kwa uwazi hatua zote. Kuwa uchunguzi umefanyika hospitali gani na watuhumiwa 5 wako ndani na upelelezi unaendelea. Na kwamba, tukio lilitokea 28 Feb 2024 taarifa ikatolewa 11 Machi, 2024. Hapa Pana maswali ngazi ya wazazi napo. Hivyo lazima upelelezi ufanyike chini ya wizara ya mambo ya ndani Jeshi la Polisi, kisha mwendesha mashtaka (wizara ya Katiba na Sheria) aone itifaki yake kuhusu kwenda mahakamani.

Nadhani wananchi wengi hawajui hizi itifaki za kisheria, wao wanajua, ustawi akipokea taarifa mambo yote anamaliza yy. Siyo hivyo ndugu zangu wapendwa.

Kuna Sheria, taratibu na kanuni za vyombo vya taasisi za wizara mbalimbali kwa mujibu wa Sheria kuu yaani Katiba ya nchi yetu. Mbarikiwe.

Sent from my CPH2207 using JamiiForums mobile app
 
Mh Waziri nimekuelewa sana pengine kuna sehemu amekosea naomba usamehe na ujue kuwa ambacho unaweza msaidia ni yeye kupata haki yake ya kujua ukweli na kupata fursa ya kuongea nae na kumfariji maana kwa hali aliyonayo lazima kuna kuchanganyikiwa…Mtoto amefariki cha kumsaidia ni kuhakikisha anapata msaada na unaongea nae….! Tunaomba unsaidie wewe ni Mama na unajua mtoto anavyo uma wengi huvurugwq!
Mimi sina neno na huyu mama wala. Na sitakiwi kuwa na neno lolote kama kiongozi. Hoja yangu ni hawa watoa habari wa kujitegemea akina unknown ambao, hawazingatii maadili na miiko ya habari, ama kwa kutojua au kujua yaani makusudi na kutumika kwa faida zao. Ili tu, kazi yote ninayofanya na wadau wazuri kwenye jamii kwa maslahi ya jamii ionekane ya hovyo.

Anyway, Mungu ana macho.

Sent from my CPH2207 using JamiiForums mobile app
 
Umeongea vizuri, ila kusema hutaki mwanao asipigwe nimebaki mdomo wazi. Basi wewe ni tofauti na mimi, mimi nina watoto wanasoma hizi kayumba zilizochangamka (English medium) tena ya dini . Wakati nampeleka wa kwanza wakaniambia kuna wazaz walisema hawataki watoto wao wachapwe. Mimi nilisema wa kwangu akikosea achapwe la sivyo ntamhamisha. Mimi sina imani ya kulea mtoto km mayayi. Muhimu "aadhibiwe siyo kupiga". Mimi mwenyewe hata nyumbani wanakula makofi kila wakifanya upuuzi achilia mbali fimbo.

Ila ktk malezi kila mtu na style yake bwana hamuwezi kufanana wote. Ni sawa tu na kuendesha maisha ya ndo, kila mwanaume ana mfumo wake.
Ukienda nchi zilizostaarabika kama za Ulaya utapata shida kweli kweli na watakunyang'anya watoto. Kupiga hakusaidii bali kunaharibu. Hii ni research siyo mimi. Unaweza kumfundisha mtoto bila kumchapa. Hata mimi nyumbani sikupigwa na wazazi wangu. Hivi unajua mtoto aliyekulia Ulaya ana tofauti kubwa na mtoto aliyekulia Tanzania? Unajiuliza ni kwa sababu gani?
 
Tunashukuru kwa kuja kujibu hapa chamsingi tunaomba ufatilie hili jambo hadi mwisho ujue limefikia wapi na ikiwezekana uonane na mfiwa ujue na umfariji! Kwenye hizi kazi kuna kusingiziwa kwa hiyo usichoke ndio kazi ya Umma! Tunaomba umsaidie
Kila kitu Kiko sawa, shauri linaendelea, soma taarifa ya Polisi, Moshi kuna serikali ya mkoa na wilaya pia, hapa kikubwa wala siyo huyu mama Bali watoa taarifa wasiozingatia weledi wa kubalance habari. Hawa ndiyo shida.

Sent from my CPH2207 using JamiiForums mobile app
 
Nilitaka kushangaa hizi tuhuma juu yako maana nakujua vizuri.Binafsi mwaka jana nilikuwa na shida nikakutumia sms usiku saa nne usiku nilishangaa kuona unanijibu.Upo vizuri sana kufatilia mambo yanayohusu wizara yako maana ni nadra sana kumuona Waziri anajibizana na wananchi tena kwa sms .Big up sana dada.
Hata mm nimeshangaa kuwa, inawezekanaje baadhi ya watu wakipokea taarifa tu wanaondoka nayo hata kusema kuwa, mbona haina upande wa pili? Yaani nashangaa kuwa zama hizi mtu anaweza kuibuka na habari mfano nime R...P, basi baadhi wakaanza kabisa kuchimba na ka...ri hata dea.... cert..... haipo

Wito wangu jamani, watoa taarifa watafute taarifa kwa bidii lakini wafanye balance, na wasomaji nao wasome kwa bidii ila wakumbuke kuangalia balance...

Kwenye mambo ya kijamii wote tunategemeana ..

Sent from my CPH2207 using JamiiForums mobile app
 
Shikamoo Dr. gwajima nimefarijika kumbe umekuwa mtu wa watu kiasi hiki hadi unachati na sisi huku..Naomba tu kubali salamu yangu najua inaenda kubadili ktu kwenye maisha yangu kitakacho acha alama
Ubarikiwe, Kila la heri. Ndiyo Dunia ilivyo, Hadi vitabu vimeandika, kumbukumbu nzuri hutolewa ukisha fumba macho na mdomo. Ndiyo kanuni ya Dunia. Kwa kuwa tunaishi kimwili na kiroho, tuimarishe zaidi misuli ya Imani, ndiyo faraja yetu....

Sent from my CPH2207 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom