DOKEZO Mwanangu ameuawa kwa kupigwa na Mwalimu lakini kesi inazungushwa

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
Tukisoma taarifa ya Jeshi la Polisi kipenge cha 3, tutaona kwa uwazi hatua zote. Kuwa uchunguzi umefanyika hospitali gani na watuhumiwa 5 wako ndani na upelelezi unaendelea. Na kwamba, tukio lilitokea 28 Feb 2024 taarifa ikatolewa 11 Machi, 2024. Hapa Pana maswali ngazi ya wazazi napo. Hivyo lazima upelelezi ufanyike chini ya wizara ya mambo ya ndani Jeshi la Polisi, kisha mwendesha mashtaka (wizara ya Katiba na Sheria) aone itifaki yake kuhusu kwenda mahakamani.

Nadhani wananchi wengi hawajui hizi itifaki za kisheria, wao wanajua, ustawi akipokea taarifa mambo yote anamaliza yy. Siyo hivyo ndugu zangu wapendwa.

Kuna Sheria, taratibu na kanuni za vyombo vya taasisi za wizara mbalimbali kwa mujibu wa Sheria kuu yaani Katiba ya nchi yetu. Mbarikiwe.

Sent from my CPH2207 using JamiiForums mobile app
Uzi ufungwe Sasa kweli katika mawaziri nchi hii wewe Mama upo active kwenye sector yako

Ubarikiwe sana Mheshimiwa
 
Uzuri ni kuwa, hakukuwa na mazungumzo kati yangu na yy kama ilivyoandikwa hapo juu. Sijui haya katunga nani
Mheshimiwa don't use that words, inasikitiaha sana kuuliwa kwa binadamu kizembe hata kama hukuzungumza ila tukio limetokea na maisha yametoweshwa.

Hapo ni mtu/watu wawajibishwe no excuse tupo kwenye Ramadhan tutende haki hata kwa wasio na uwezo kujisimamia, waweze kusimama.
 
Mheshimiwa don't use that words, inasikitiaha sana kuuliwa kwa binadamu kizembe hata kama hukuzungumza ila tukio limetokea na maisha yametoweshwa.

Hapo ni mtu/watu wawajibishwe no excuse tupo kwenye Ramadhan tutende haki hata kwa wasio na uwezo kujisimamia, waweze kusimama.
Si ndiyo taarifa imetolewa kuhusu maendeleo ya shauri ndugu yangu? Mm nilichokanusha ni kuwa sijaongea kwa simu na kutoa hayo maelekezo kama ilivyosemwa. Kisha nikatoa na update ya hatua zilizochukuliwam kumbe tena ndugu yangu sijafanya vema? Niwie radhi basi tusonge mbele.
 
Si ndiyo taarifa imetolewa kuhusu maendeleo ya shauri ndugu yangu? Mm nilichokanusha ni kuwa sijaongea kwa simu na kutoa hayo maelekezo kama ilivyosemwa. Kisha nikatoa na update ya hatua zilizochukuliwam kumbe tena ndugu yangu sijafanya vema? Niwie radhi basi tusonge mbele.
Achana nae
 
Inaumiza sana kwa kweli,mara nyingi mauaji ya visasi huanzia katika Hali Kama hizo hususan haki inapopindishwa na ndugu wakabaki na majeraha ya moyo.

Huyu mama asaidiwe
 
Ubarikiwe, Kila la heri. Ndiyo Dunia ilivyo, Hadi vitabu vimeandika, kumbukumbu nzuri hutolewa ukisha fumba macho na mdomo. Ndiyo kanuni ya Dunia. Kwa kuwa tunaishi kimwili na kiroho, tuimarishe zaidi misuli ya Imani, ndiyo faraja yetu....

Sent from my CPH2207 using JamiiForums mobile app
Nakupenda Waziri wangu, miongoni mwa wachache walio tayari kujibu hoja za watu wa hali zote. Be blessed.
 
Umemchapa mtoto, kafa lazima ujieleze kilichotokea sio unafichwa fichwa kama mwali. Kama ulimchapa kwa weledi kwanini unafichwa fichwa? Unatetea ujinga ujinga tu.
Usipende kusikiliza upande mmoja na kujaji? Kwa Hiyo unataka kusema Mwl kampa Hela Daktari atoe ripoti feki, akampa waziri na mtu wa Dawati la jinsia wafiche ukweli? Hivi unadhan ni rahisi? Hivi unaijua case ya mauaji? Unajua namna serikali inamvalue mwanafunzi? Mwaka Jana nilipatwa na mkasa mmoja. Nilimuokota mwanafunz mmoja njiani akiwa amelala anatetemeka. Kwa maelezo yake, mwenzake amemchoma na pen kichwani baada ya ugomvi Watu wametawanyika ndio yeye hali ikabadilika. Kiutaratibu ilitakiwa nianzie police kupata form ya pf3 ila nikamuomba Daktari amsaidie tu maana anahitaji matibabu ya haraka. Bahati mbaya mtoto akafariki kesho yake. Nikashangaa police wananing'ang'ania Hata maelezo yangu hawayasikilizi. Badaye nikaona mkuu wa kituo anataka kuonekana ameshaanza kuchukua hatua na baadhi ya watu tayari wapo ndani. Nikamuomba mkuu wa kituo anisaidie kutoa pf3 na kuibackdate akasema haiwezekani Maana taarifa za Jana za kituo ameshatuma mbele na haiwepo hiyo taarifa. Hospital pia hawawezi kubadili taarifa maana pale wanajiendesha kidigitali taarifa zote zinatembea Kwa njia ya Mfumo wa computer. Niliteseka sana kuja kutoka. Na ilikua ni baada ya kumkamata mtoto aliyemchoma mwenzake na pen. Ninachotaka kukwambia hapa ogopa case ya kumuua mwanafunzi, mambo sio marahisi Kama mnavyodhani mtaani. Maana Daktari mkuu hataki kuharibu Kazi yake, police pia ni hivyo hivyo, Kila mtu anajiweka safe side. Maana case inaweza kufika Mbali na udanganyifu wowote unaweza kumkost mtu

turudi kwenye Mada Mimi nadhani ripoti ya Daktari ni ya Kweli, lakini mzazi hataki kuamini Hilo, anapeleka malalamiko Kwa waziri akiwa tayari na majibu yake, anataka Watu waadhibiwe tu Ili Moyo wake uridhike. Kilichotokea hapo ni matukio mawili yasiyo na mahusiano yametokea, mwalimu kuadhibu na mtoto kuonyesha dalili za cancer na Hilo ndio mzazi hataki kuamini hilo.

Inauma sana kumpoteza mtoto lakini inahitajika utulivu tu, ni Kweli mzazi anaham ya kumpigania mtoto angalau Mwl achukuliwe hatua Ili mtoto huko alipo ajue mzazi hakukaa kizembe kudai haki. Ila Ndugu mzazi jikaze, limeshatokea na haiwezekani kubadili Hilo na maisha lazima yaendelee
 

Naitwa Janeth Shayo, mkazi wa Uru, Moshi. Naomba unisaidie kupaza sauti mwanangu Jonathan Makanyaga (07) mwanafunzi wa darasa la kwanza shule ya msingi Mrupanga, ameuawa kwa kupigwa na Mwalimu lakini kesi inataka kupindishwa.

Tar.28/02/2024 mwanangu alienda shuleni akiwa mzima. Alipofika aliadhibiwa kwa kuchelewa "namba". Alipoingia darasani alianza kutokwa damu puani na mdomoni. Akarudishwa nyumbani. Nilipomkagua nikamkuta na majeraha yaliyovilia damu mgongoni, kwenye mbavu na mguuni.

Kesho yake nikaenda nae shuleni kutaka kuoneshwa mwalimu aliyemfanyia ukatili mwanangu. Lakini Mwalimu mkuu akaomba nibaki nje. Akaingia na mwanangu ofisi ya walimu na kumtaka amtambue Mwalimu aliyemuadhibu. Mwanangu akamtanbua. Mwalimu Mkuu akaniambia wameshamfahamu ni mwalimu wa "Field" hivyo atazungumza nae.

Wakanipa 20,000/= za matibabu. Nikampeleka mwanangu zahanati. Kesho yake akazidi kutoka damu, na kulalamikia maumivu sehemu za mbavu. Nikampeleka hospitali ya masista. Daktari akaniambia bandama imejeruhika ndio sababu ya kutoka damu mdomoni. Mtoto alidai pamoja na viboko alivyochapwa, Mwalimu pia alimpiga ngumi tumboni. Huenda ndiyo iliyopasua bandama.

Hali yake ilizidi kuwa mbaya tukapewa rufaa kwenda KCMC. Akatakiwa kufanyiwa upasuaji. Gharama 350,000/= lakini sikuwa nayo. Nikapiga simu shuleni wakasema tuombe afanyiwe halafu watalipa baadae. Hata hivyo kabla hajafanyiwa hali yake ikazidi kuzorota, akashindwa kupumua, akawekwa kwenye Oxygen. Akashindwa kula, akawekewa mpira wa chakula. Baada ya siku chache akafariki 😭.

Lakini ripoti ya hospitali inasema mwanangu amekufa kwa kansa ya damu. Kansa gani ya damu inayomuua mtoto kwa wiki mbili? Na kwanini hiyo kansa itokee baada ya kuadhibiwa shuleni? Kwanini Mwalimu aliyemuadhibu mwanangu anafichwa, na sipewi haki ya kumfahamu?

Nalazimishwa nichukue maiti nikazike lakini nimekataa. Nataka uchunguzi huru. Nimeenda dawati la jinsia kulalamika nikapuuzwa. Nimepiga simu kwa Waziri Dkt. Gwajima D akanipa namba ya mtu wa kunisaidia. Nilipopiga kumbe ni yuleyule Mkuu wa dawati la jinsia aliyenipuuza. Nikamrudia Gwajima akasema niwasiliane nae huyohuyo. Nimekosa pa kulilia haki ya mwanangu Jonathan

Pia, Soma: Madai ya Janeth Shayo, Mkazi wa Uru, Moshi, kutosikilizwa
Habari bado haija balance .....ni mbaya sana kuleta habari upande mmoja....inaharibu maana
 
Acha UJINGA. Wewe ndo huyo mwalimu? Mwalimu amekataa kuwa hakumpiga ngumi kama madai ya mzazi anavyosema? Huyo mwalimu yupo wapi aseme kuwa hakumpiga mangumi na mateke? Hapa hoja ni upatikanaji wa huyo mwalimu ambaye tukio la kifo limeanzia kwake. Ajieleze. Alimpiga mtoto kwa kiwango gani.
Unadhan mpaka waziri na mtu wa Dawati la jinsia kuanza kumpuuza mzazi hawakulifanyia Kazi Hilo? Lazima Mwl amehojiwa na Daktari amehojiwa. Lazima mkurugenzi amelifatilia analijua Hilo, lazima mkuu wa wilaya amelifatilia analijua Hilo, DSEO Lazma amelifatilia analijua Hilo, ocd lazma analijua hilo Maana waziri hawezi kwenda mwenyewe Ana vyanzo vyake vya habari na viongozi wa chini hujitahid sana kufatilia jambo na kulifahamu Kwa kina, asije kupigiwa Simu akampotosha waziri Au akajibu hajui Maana ni kuchezea kitumbua chake.
 
Dada pole sana
Yaweza kuwa fimbo zimekuw sababu ya kusogeza kfo chake karbu , lakn sasa mwanafunz/Mtoto (07) ata kama huyo.mwl ni wa field kweli amempga ngumu

Kwa maelekezo ya awali inaonyesha fimbo lakn inaonyesha changamoto ilipozd mkaja tafuta sababu zaid mkadai ni ngumi pia

Kawaid ulipofk hospital ya kwanza kuna report inaandikwa vle mgonjwa hali yake ilivyo iliandw kuhusu majeraha ya fimbo

(Pia tafuta wanafunz wanao soma na mwanao uliza ni kwa jins gan mtoto alipewa adhabu)
 
Duuu mkuu pole sana bila shaka Dkt. Gwajima D atakuja hapa kutoa majibu …aisee inauma sana sana yani mwalimu anampiga ngumi mtoto hapa hii haikubalika kabisa kabisa!

Nafikiri kwenye hili Mwl Mkuu anapaswa kuchukuliwa hatua kabisa na huyo mwalimu anapaswa kufikishwa kwenye vyombo vya kisheria hii ni hatari!

Halafu Dkt. Gwajima D unapaswa kutwambia huyo mtumishi wako wa dawati la jinsia anaye lalamikiwa kupuuza watu unapaswa kumuondoa pale hapamfai kabisa!
Don't jump to conclusions
 
Pole sana bi dada .siku za mja zikishatimia huwa sababu ni nyingi sana
Mtoto ndio ameshafariki mshukuru tu mungu
 
Back
Top Bottom