fimboyaasali
JF-Expert Member
- Jan 14, 2011
- 8,623
- 8,198
Ndio, wewe mwanamke ukiwa tayari kuolewa, toka nje umtafute mumeo, usikae ndani kumsubiri, mfate huko nje. Mumeo hutampata ndani, toka nenda kanisani kusali, nenda msikitikini, nenda kwenye mihadhara ya kila aina ya kidini, kisiasa, makongamano, kwenye michezo mbalimbali.
Ongea na rafiki zako wa kike kama wana makaka ambao wapo tayari kuoa, ongea na mapadri, wachungaji, mashehe kuwaambia kuwa unatafuta mchumba, jiandikishe kwenye dating sites.
Ukitoka vaa kwa staha ongea kwa adabu na ukifanya utafiti ukamuona kaka fulani akakuvutia na ukagundua kuwa hana mke, mkabili mwambie umempenda na upo tayari akuoe.
Chacharika kwa kila hali, usikae kusubiri mwanaume aje, toka umtafute huko nje.
Ongea na rafiki zako wa kike kama wana makaka ambao wapo tayari kuoa, ongea na mapadri, wachungaji, mashehe kuwaambia kuwa unatafuta mchumba, jiandikishe kwenye dating sites.
Ukitoka vaa kwa staha ongea kwa adabu na ukifanya utafiti ukamuona kaka fulani akakuvutia na ukagundua kuwa hana mke, mkabili mwambie umempenda na upo tayari akuoe.
Chacharika kwa kila hali, usikae kusubiri mwanaume aje, toka umtafute huko nje.