Mwanamke anavyovaa ni kwa influence ya nani?

Mwanamke anavyovaa ni kwa influence ya nani?

Maamuzi yao binafsi na wako hivyo linapokuja swala la mavazi kwa wengi wao, hebu chunguza siku moja kama uko sehemu mfano kuna wanawake wengi au kwenye shughuli/sherehe lazima watoleane macho wewe ukiangalia unaona kabisa hapa kuna kawivu fulani.

Na si mavazi tu hata nywele zao za bandia sijui ndio niseme za kubandika hali ni hiyo hiyo kutoleana macho
 
Which thing shows that women are weak ,And how about men do you think MEN are not weak.For me a want to know the one who post this thread he or she knows what FEMINISM IS? For me i think i can not wear because of aguy coz does a guy wear because of me? So dont live life of wind right?
 
Katika kitu ambacho Mungu kanisaidia kukiepuka na influence ya mtu yani always huwa nabaki kwenye msimamo wangu

nakubaliana na wewe. ni vizuri kufanya kitu ambacho upo comfortable nacho, na sio kwasababu ya kumfurahisha mtu mwingine.
 
Ni matumaini yangu kuwa nyote mnaendelea kupumua.Kuna dhana imejengeka sana miongoni mwa jamii zetu nyingi. Dhana yenyewe ni kuwa mwanamke ni kiumbe dhaifu sana katika nyanja mbalimbali za maisha. Kutokana na huu mtazamo, wengi wanaamini kuwa ni vigumu sana kwa mwanamke kufanya maamuzi ya aina yoyote ktk maisha ya kila siku.Tuje kwa upande wa mavazi hasa kwa wadada zetu ambao wengi hudiriki hata kutembea nusu uchi wakidai ni fashion. swali linakuja, kwamba; wanavovaa vile ni maamuzi yao au kuna mtu/watu wenye maamuzi aghalabu wanaume wanaowasababisha au kupenda wao wavae vile?? Tupe mtazamo wako.Naweka mjadala mezani.
wanawake gani hao ambao hawawezi kufanya maamuzi yao wenyewe? hao wanawake bado wapo kweli kwenye kizazi hiki
 
Wanawake wanavaa nguo kwa ajiri ya wanaume. Kama unakukubali kakataa au kataa kukubali shauri yako
 
ila tupende tusipende, tukubali, tusikubali jinsi dunia inavyobadilika ndivyo watu tabia, mazingira ndivyo yatakavyobadilika...Hata watu wapige kelele vipi...km nchi za magharibi hazijakubali kubadilika kwanza wao nchi hizi zinazoendelea hazitobadilika ila zitaendelea tuu kuwaiga kila wakifanyacho....Labda taifa la kiarabu likuwe kiuchumi liwe la kwanza kiuchumi duniani ndipo watu watabadilika...

Dunia inavyobadilika kimazingira, kimaendeleo na tabia za watu lazima zibadilike...hatuwezi kurudi nyumba au kubakia na tabia zile zile....Maovu, uchafuzi mazingira, nk.
 
Back
Top Bottom