nguvumali
JF-Expert Member
- Sep 3, 2009
- 4,923
- 1,325
Leo nilitembelea maeneo ya Tabata kwa mwanangu, wakati narudi kwangu kule Kigamboni , ghafla kufilka pale wanapoita Tabata reli Trafiki Police alisimamisha magari ya upande mmoja ilikuokoa jahazi la magari yanayotoka Buguruni, sasa Gari la mwanajeshi likawa limekumbwa na kizaazaa cha kusimamishwa, mwanajeshi yule ana cheo cha staff sajenti alimvaa Police kwa kejeli na matusi. Trafic akamjibu tuheshimiane lakini mjeshi akaendelea kumtusi askari yule mwenye cheo cha Copro, kama mzaa mwanajeshi akamkwida Uniform , hahahahaaaah Police hakukubali dharau ile, akampiga Mtama mwanajeshi yule, alipoinuka akapigwa Gumi la kuushoto, baada kama ya Dakika 5, MWANAJESHI HOI, ashukuru Mungu jamaa wenye mabucha na askari Police wengine walikuja kuingilia ugomvi ule.
Hakuna dereva wala konda wa daladala alietamani Ugomvi ule uishe, ila jambo lililosisimua na aina ya Ngumi za yuleTrafic dhidi ya Mwanajeshi yule.
Hakuna dereva wala konda wa daladala alietamani Ugomvi ule uishe, ila jambo lililosisimua na aina ya Ngumi za yuleTrafic dhidi ya Mwanajeshi yule.