MwanaHALISI laibukia MSETO...

MwanaHALISI laibukia MSETO...

VUTA-NKUVUTE

JF-Expert Member
Joined
Nov 25, 2010
Posts
6,140
Reaction score
18,004
Katika kile kinachoonekana ni kufuata ushauri wa JF katika kuhakikisha kuwa wananchi wanaendelea kupata habari zenye mshiko,leo Gazeti dada la MwanaHALISI la Mseto limebeba makala ya kisiasa tofauti na kawaida ya gazeti hilo kusheheni michezo.

Ukurasa wa mbele kabisa wa Mseto la leo kuna makala iliyoandikwa na Mhariri wa MwanaHALISI Comredi Jabir Idrissa yenye kichwa cha maneno 'Kilicholiponza MwanaHALISI ni hiki'.Katika makala hiyo,Idrissa anachambua kwakina makala zinazosemekana kuwa siliiudhi Serikali na kupelekea kufungiwa gazeti pendwa la MwanaHALISI.

Wakati huohuo,Gazeti la RaiaMwema linaloongozwa na Gwiji wa Uandishi, Jenerali Ulimwengu aka Mzee wa G55, nalo limejitokeza katika toleo la leo kupinga ubabe wa Serikali kufungiafungia magazeti ya kiuchunguzi. Aluta Continua...


Si kitu cha ajabu kwa gazeti la michezo kuta habari nyingine, na si kinyume cha sheria. Mara nyingi magazeti ya akina Shigongo huwa yanaandika habari za siasa, utadhani Uhuru.

isitoshe mwaka 1995 wakati akina Jenerali Ulimwengu walipoanzisha Dimba (la michezo) gazeti hilo lilikuwa linaandika habari za siasa, zakampeni za uchaguzi, hadi pale walipoanzisha Mtanzania, na baadaye RAI.

Lakini ninachohofia hapa ni kwamba katika serikali hizi za kihovyo hovyo inaweza pia kulifungia gazeti hilo kutimiza uchu wake wa kuwaziba wananchi wasijue jinsi serikali yao inavyofanya unyama kwa wananchi wake.

Halafu kitu zaidi kinachonishangaza ni kwamba serikali ilishindwa kabisa kuelezea kivipi Mwanahalisi kilisema uongo katika matoleo yake iliyotaja kukiuka maadili kuhusu sakata la Ulimboka.

Mimi nadhani imefika wakati sasa serikali iwaambie wananchi kuwa sakata la kutekwa ulimboka halikuwapo kabisa na kwamba daktari huyo huenda alipigwa na mke wake nyumbani.

Sijaona serikali kama hii. Lile gazeti la Rupert Murdoch la NEWS OF THE WORLD lilikowa linaandika habari za uongo za kupotosha umma na wahariri wake kudukuu simu za watu wengine hazlikufungwa na serikali ya huko Uingereza, mmiliki wake mwenyewe ndiyo aaliamua kulifunga kuondoa malalmiko.
 
...options zilivyokuwa nyingi siku hizi, sijui kama kufungia gazeti ni suluhu ya jambo!
...stamping hard on sh**t to cover will only spread it afar!! kalaghabao...
 
Uwezi kuziba uhuru wa habari kwakufungia vyombo vya habari.....huu ni udikiteta nijinsi gani washahuri wa habari wasivyokuwa makini wakidhani ukifungia chombo cha habari utakuwa umejiosha kwa umma wa watanzania!!Kumbe ndo kwanza unawafumbua akili wakitaka kujua nini kimefanyika mpaka gazeti linafungiwa!!
 
Serikali ikiua adui mmoja inazalisha wengine 100, kufungwa kwa mwanahalisi ni kufungua midomo ya magazeti mengine...
kwani anaeruhusu kuanzishwa magazeti mengine ni nani?au mtu yeyote anaweza amka asubuhi na kuanzisha gazeti?
 
Uwezi kuziba uhuru wa habari kwakufungia vyombo vya habari.....huu ni udikiteta nijinsi gani washahuri wa habari wasivyokuwa makini wakidhani ukifungia chombo cha habari utakuwa umejiosha kwa umma wa watanzania!!Kumbe ndo kwanza unawafumbua akili wakitaka kujua nini kimefanyika mpaka gazeti linafungiwa!!
hizi gumzo zinanikumbusha enzi ya magazeti kama motomoto,wakati ni huu,etc .

This is the way the cook crumble.HAKUNA JIPYA HAPA.
 
kwani anaeruhusu kuanzishwa magazeti mengine ni nani?au mtu yeyote anaweza amka asubuhi na kuanzisha gazeti?

Sio kuanzisha gazeti ila kuzalishwa kwa waandishi wa aina ya Kubenea na Jabir wenye haya haya magazeti tuliyonayo. Hii nchi iko ICU
 
Gazeti la Mwanahalisi leo limeibukia katika gazeti lake dada la michezo, Spoti Mseto. Limefafanua kwa kurasa tatu kilicholiponza hadi likafungiwa, na mambo kibao.
 

Attachments

  • Photo0025.jpg
    Photo0025.jpg
    44.7 KB · Views: 1,913
Katika kile kinachoonekana ni kufuata ushauri wa JF katika kuhakikisha kuwa wananchi wanaendelea kupata habari zenye mshiko,leo Gazeti dada la MwanaHALISI la Mseto limebeba makala ya kisiasa tofauti na kawaida ya gazeti hilo kusheheni michezo.

Ukurasa wa mbele kabisa wa Mseto la leo kuna makala iliyoandikwa na Mhariri wa MwanaHALISI Comredi Jabir Idrissa yenye kichwa cha maneno 'Kilicholiponza MwanaHALISI ni hiki'.Katika makala hiyo,Idrissa anachambua kwakina makala zinazosemekana kuwa siliiudhi Serikali na kupelekea kufungiwa gazeti pendwa la MwanaHALISI.

Wakati huohuo,Gazeti la RaiaMwema linaloongozwa na Gwiji wa Uandishi, Jenerali Ulimwengu aka Mzee wa G55, nalo limejitokeza katika toleo la leo kupinga ubabe wa Serikali kufungiafungia magazeti ya kiuchunguzi. Aluta Continua...
Ngoja nikalitafute...
 
Tunashukuru kwa taarifa. Ila tunakuomba ungeandika kwa ufupi sababu hizo kadhaa, ungetusaidia wana jamvi wengi. Wengine huku kijijini gazeti hili halifiki kabisa.
 
Kanisa la ufufuo pia lifungiwe!
 
nimeshalikosa pale kijiweni kwangu, nitumieni hata soft copy nitalipia bana, kwani buku kitu gani bana
 
The good thing is that TRUTH is devine, BUT falsehood is demonic; no matter how hard they try; TRUTH will preavail over falsehood, na laana ya unyama wao itawatafuna mmoja mmoja mpaka waishe. na hii ndio sala ya kila mzalendo wa nchi hii. hata wakifunga media houses zote na kuua kila anayezungumzia issue ya utekwaji na mateso ya Dr. ulli; ukweli uko wazi na utashinda tu.
 
Asante kwa kutujulisha kumbe kila j5 tutakuwa tunakula habari za uchunguzi kama kawa.
Mimi nawashauri hali halisi puplishers wasajili magazeti kama 10 hiviliwepo ggazeti kaka,mjomba,binamu,nkazamjomba,kilembwe,mjukuu,shangazi,shemeji nk ili likifungiwa moja tuendelee kupata habari.
 
Yaani bora wangefungia magazeti ya she gongo, ndio yanayochangia kuharibu wanafunzi wetu! na kuandika upuuzi wa vyumbani. Utakuta wanafunzi katika mifuko yao hawakosi magazeti hayo wanaendanayo sconga wakifika huko meno njeee!
 
Katika kile kinachoonekana ni kufuata ushauri wa JF katika kuhakikisha kuwa wananchi wanaendelea kupata habari zenye mshiko,leo Gazeti dada la MwanaHALISI la Mseto limebeba makala ya kisiasa tofauti na kawaida ya gazeti hilo kusheheni michezo.

Ukurasa wa mbele kabisa wa Mseto la leo kuna makala iliyoandikwa na Mhariri wa MwanaHALISI Comredi Jabir Idrissa yenye kichwa cha maneno 'Kilicholiponza MwanaHALISI ni hiki'.Katika makala hiyo,Idrissa anachambua kwakina makala zinazosemekana kuwa siliiudhi Serikali na kupelekea kufungiwa gazeti pendwa la MwanaHALISI.

Wakati huohuo,Gazeti la RaiaMwema linaloongozwa na Gwiji wa Uandishi, Jenerali Ulimwengu aka Mzee wa G55, nalo limejitokeza katika toleo la leo kupinga ubabe wa Serikali kufungiafungia magazeti ya kiuchunguzi. Aluta Continua...
Naona kama Wanatapa tapa vile mbona kilichoandikwa kwenye Mseto ni copy & Paste ya kilichoandikiwa kwenye Mwanahalisi Jumatano iliyopita.
 
Back
Top Bottom