MwanaHALISI laibukia MSETO...

nakumbuka kikwete alisifiwa wakat anazama madarakan hadi mwenyewe kwenye vyombo vya habari aliomba akosolewe....sasa mbona akikosolewa anavuta mdomo, prezidaa wangu u talk much bt u practice negative.
 
Teknolojia ya habari inaenda mbele wazee wanataka kuirudisha nyuma(Mzalendo na RTD) ni kifo na uhai, Tofauti kabisa.

Kwa kulifungia gazeti la mwanahalisi, taarifa ndiyo zitazidi kupatikana. Wazee (CCM) kumbukeni hukohuko mlipo kuna wazee wenye akili timamu wanaotoa taarifa juu yenu.
 
Nadhani na hapa JF inabidi kuwe na special platform ya Mwanahalisi na ikiwezekana Mwanahalisi sasa lianze kuuzwa online, hii Serikali dhaifu haiwezi kubishana na sauti ya Mungu.
 
kwa kweli serikali hawatendi haki maana hata sababu za kulifungia gazeti la mwanahalisi hazieleweki hasa kwa wadau wa habari na wanaoamini katika uandishi wenye kina na kweli.
 
Tena wanatakiwa ukurasa wa mbele wadilishe iwe "MSETO HALISI" Halafu wanaturudishia rangi zile zile na nondo za kiuchunguzi zile zile. Wasishau ushauri wangu wa kumuita Dr Ulimboka kuwa mgeni rasmi kwenye uzinduzi wa MSETO HALIS
 
Nawashauri Mwanahalisi watafute gazeti lingine na kutolea habari zake katika kipindim hiki.Tuko nyuma yenu na wadhalimu hawa wanaokataa ukweli watashindwa tuu ni suala la muda tuu.
 
Leo vijana wanaoniuziaga Mwanahalisi kila J5 wakaniambia nsipate hofu kuna MSETO badala yake.

Basi kwenye MSETO shujaa jasiri Kubenea karudia article yote iliyopelekea Mwanahalisi kufungiwa. Kalisome mwenyewe!


Talk about heroic perseverance......this one!!!!
 
mkuu hilo ni gazeti au nakala kwenye gazeti lingine? Tujuze kaka...
 
nilikuwa nikizungumza na ndugu yangu mmoja jioni hii akanambia kuwa eti gazeti la mwanahalisi limekuja kwa staili mpya mabapo eti kubenea anashusha habari nzito za uchunguzi kupitia gazeti la mseto linalomilikiwa na kampuni ya hali halis publishers na akanitolea mfano leo kuwa eti gazeti hili ambalo huwa ni mahsusi kwa ajili ya michezo headlne yake ilikuwa ni ya siasa na sio michezo.hili likoje jamani/naomba ufafanuzi
 
kama ni kweli na iwe hivyo,na kama si kweli na afanye hivyo.tutalinunuqa hilo gazeti kama maporomoko ya mto nile
 
nilikuwa nikizungumza na ndugu yangu mmoja jioni hii akanambia kuwa eti gazeti la mwanahalisi limekuja kwa staili mpya mabapo eti kubenea anashusha habari nzito za uchunguzi kupitia gazeti la mseto linalomilikiwa na kampuni ya hali halis publishers na akanitolea mfano leo kuwa eti gazeti hili ambalo huwa ni mahsusi kwa ajili ya michezo headlne yake ilikuwa ni ya siasa na sio michezo.hili likoje jamani/naomba ufafanuzi
Hana jipya anarudia tu uzushi aliyokwisha uandika huko nyuma, si unajua njia ya mwongo fupi.
 
Si kitu cha ajabu kwa gazeti la michezo kuta habari nyingine, na si kinyume cha sheria. Mara nyingi magazeti ya akina Shigongo huwa yanaandika habari za siasa, utadhani Uhuru.

isitoshe mwaka 1995 wakati akina Jenerali Ulimwengu walipoanzisha Dimba (la michezo) gazeti hilo lilikuwa linaandika habari za siasa, zakampeni za uchaguzi, hadi pale walipoanzisha Mtanzania, na baadaye RAI.

Lakini ninachohofia hapa ni kwamba katika serikali hizi za kihovyo hovyo inaweza pia kulifungia gazeti hilo kutimiza uchu wake wa kuwaziba wananchi wasijue jinsi serikali yao inavyofanya unyama kwa wananchi wake.

Halafu kitu zaidi kinachonishangaza ni kwamba serikali ilishindwa kabisa kuelezea kivipi Mwanahalisi kilisema uongo katika matoleo yake iliyotaja kukiuka maadili kuhusu sakata la Ulimboka.

Mimi nadhani imefika wakati sasa serikali iwaambie wananchi kuwa sakata la kutekwa ulimboka halikuwapo kabisa na kwamba daktari huyo huenda alipigwa na mke wake nyumbani.

Sijaona serikali kama hii. Lile gazeti la Rupert Murdoch la NEWS OF THE WORLD lilikowa linaandika habari za uongo za kupotosha umma na wahariri wake kudukuu simu za watu wengine hazlikufungwa na serikali ya huko Uingereza, mmiliki wake mwenyewe ndiyo aaliamua kulifunga kuondoa malalmiko.


 
nilikuwa nikizungumza na ndugu yangu mmoja jioni hii akanambia kuwa eti gazeti la mwanahalisi limekuja kwa staili mpya mabapo eti kubenea anashusha habari nzito za uchunguzi kupitia gazeti la mseto linalomilikiwa na kampuni ya hali halis publishers na akanitolea mfano leo kuwa eti gazeti hili ambalo huwa ni mahsusi kwa ajili ya michezo headlne yake ilikuwa ni ya siasa na sio michezo.hili likoje jamani/naomba ufafanuzi

Ni kweli kabisa seif, si unajua mpambanaji achoki! Na kitika kupambana njia yeyyote hutumika ili kuleta ukombozi.
 
Hiyo nimeipenda sana, sasa walifungie na hili tuone.
Michezo+ Habari za uchunguzi= Ukombozi
 
Back
Top Bottom