Mwanafunzi wa Kidato cha Tano aolewa kwa Tsh. 30,000 DC Mtatiro aingilia kati na kuvunja ndoa

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Apr 18, 2017
2,813
11,991
Mkuu wa Wilaya ya Tunduru, Julius Mtatiro amevunja ndoa ya kinyemela ya kimila iliyokuwa imefungwa baina ya "Muddy Muuza Urembo" wa Tunduru Mjini na Binti aliyechaguliwa kujiunga na elimu ya Kidato cha Tano katika Shule ya Wasichana ya Masasi.

DC Mtatiro ameongoza vyombo vya usalama kuwakamata wazazi waliomuoza binti huyo pamoja na washenga waliohusika na akafanikiwa kumtia mbaroni mtuhumiwa Muddy Muuza Urembo majira ya saa 6 usiku akiwa anaishi na binti huyu wa shule kinyumba kwenye Kijiji cha Muungano, Tunduru Mjini.

81c98d28-bb45-4b52-96bf-b47f57f3aeab.jpg
Mzazi wa binti amekiri kumuoza binti huyo kwa mahari ya shilingi 30,000 kwa madai kuwa binti hakuwa tayari kuendelea na kidato cha tano.

Hata hivyo, DC Mtatiro alivyomuhoji binti huyo, binti alikiri kutaka na kupenda kuendelea na masomo yake ikiwa atapewa nafasi hiyo.

Mtatiro amemkabidhi binti huyo kwa taasisi inayolea na kufadhili wanafunzi wilayani Tunduru iitwayo KALAMU EDUCATION FOUNDATION (KEF) ili ihakikishe msichana huyo anaendelea na masomo.

Makamu Mwenyekiti wa KEF ambaye pia ni Diwani wa Kata ya Masonya Wilaya ya Tunduru, Bwanali amekiri kupata taarifa kuhusu binti huyo na kuahidi kuwa taasisi yao itamsimamia.

Mtatiro amesisitiza binti huyo atasimamiwa aendelee na masomo yake na kuendeleza ndoto yake na amewaasa Wazazi wa Tunduru kuachana na mambo ya zamani ya kuoza mabinti ambao wana nafasi ya kuwa na mchango mkubwa zaidi kwa Taifa.

Watuhumiwa watano kwa jumla wanashikiliwa na Polisi wilayani Tunduru wakiendelea kuhojiwa juu ya kula njama na kumuoza binti huyo.

Pia soma Ruvuma: Wazazi waliomuozesha mwanafunzi kwa Tsh. 30,000 waomba radhi
 
Sasa kama kaamua kuolewa kwa hiari yake, serikali inaingilia vipi? Mpaka anaolewa ina maana anajitambua kimakuzi na kijinsia.

Huko ni kumvunjia haki zake za faragha na mahusiano yake. Mtoto ni yule ambaye hayo mambo hayajui na viungo vyake havina uwezo wa kuhimili vitendo vya unyumba
 
Sasa kama kaamua kuolewa kwa hiari yake, serikali inaingilia vipi? Mpaka anaolewa ina maana anajitambua kimakuzi na kijinsia. Huko ni kumvunjia haki zake za faragha na mahusiano yake. Mtoto ni yule ambaye hayo mambo hayajui na viungo vyake havina uwezo wa kuhimili vitendo vya unyumba
Acha kukurupuka soma story nzima, binti wamemhoji amesema hakutaka kuolewa alitaka kuendelea na masomo wazazi wake wakamforce, ninyi ndio mnaojifanya mnazijua sana haki za wanawake
 
Sasa kama kaamua kuolewa kwa hiari yake, serikali inaingilia vipi? Mpaka anaolewa ina maana anajitambua kimakuzi na kijinsia. Huko ni kumvunjia haki zake za faragha na mahusiano yake. Mtoto ni yule ambaye hayo mambo hayajui na viungo vyake havina uwezo wa kuhimili vitendo vya unyumba
ok, sawa. Aliyekuwa anamuo hakujua kuwa ni mwanafunzi? Nchi hii wanafunzi hawaolewi hata kama tayari wana uwezo wa kuhimili maisha ya unyumba
 
Acha kukurupuka soma story nzima, binti wamemhoji amesema hakutaka kuolewa alitaka kuendelea na masomo wazazi wake wakamforce, ninyi ndio mnaojifanya mnazijua sana haki za wanawake
KWAHIYO NA WEWE UNAAMINI...IONEKANE SERIKALI INAMLAZIMISHA AKASOME YEYE HATAKI...?

SASA HIYO "AKATIMIZE NDOTO ZAKE" WATAISEMEA WAPI KAMA HIYO NDOTO AMEIKANA?
 
Acha kukurupuka soma story nzima, binti wamemhoji amesema hakutaka kuolewa alitaka kuendelea na masomo wazazi wake wakamforce, ninyi ndio mnaojifanya mnazijua sana haki za wanawake
inasikitisha sana....

nasoma comments kila mtu anaona bora abaki tu kwenye hio ndoa ya mchongo.... eti hawezi tena kutulia darasani.

sijui watu hawana akili, au nini....
 
Back
Top Bottom