Just Pray
JF-Expert Member
- Nov 7, 2023
- 2,142
- 4,779
Mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Angasi Robert Okechi, amesema kuwa katika nchi zilizoendelea, Bunge ni mahali pa watu wenye upeo mkubwa wa fikra na maarifa, ambapo wabunge hukutana kuandaa mipango mikakati ya maendeleo ya muda mrefu kwa manufaa ya taifa.
Akizungumza leo Juni 22, 2025 jijini Dar es Salaam, mbele ya wanahabari, Angasi amesema tofauti na mataifa mengine, hapa nchini baadhi ya wabunge huingia bungeni kwa lengo la kupanga mbinu za kisiasa zitakazowarejesha madarakani ifikapo mwaka , badala ya kujadili masuala ya msingi ya maendeleo.
“Mbunge anatakiwa aingie bungeni kuwasemea wananchi wake kwa maslahi mapana ya nchi. Lazima awe na uwezo wa kuandaa mpango mkakati na kuupeleka bungeni ili utungwe sheria zenye manufaa kwa wananchi,” amesema.
Aidha, Angasi amekosoa tabia ya kuchagua wabunge kwa misingi ya umaarufu au uwezo wa kifedha bila kuzingatia elimu na uelewa wa masuala ya kisheria na kiuchumi.
“Haiwezekani mtu mwenye elimu ya darasa la saba, kwa sababu tu anajua kusoma na kuandika, anazo fedha na anajua kuzungumza vizuri, apewe jukumu la kutunga sheria za kuongoza taifa. Bunge ni chombo nyeti kinachopaswa kuwa na watu makini,” amesisitiza.
Angasi amehimiza Watanzania kuwaamini vijana waliobobea kutoka vyuo vikuu na vyuo vya kati, kwa kuwa wanaweza kuibua mipango madhubuti ya kulisaidia taifa kwa nguvu na maarifa yao.
Akizungumza leo Juni 22, 2025 jijini Dar es Salaam, mbele ya wanahabari, Angasi amesema tofauti na mataifa mengine, hapa nchini baadhi ya wabunge huingia bungeni kwa lengo la kupanga mbinu za kisiasa zitakazowarejesha madarakani ifikapo mwaka , badala ya kujadili masuala ya msingi ya maendeleo.
“Mbunge anatakiwa aingie bungeni kuwasemea wananchi wake kwa maslahi mapana ya nchi. Lazima awe na uwezo wa kuandaa mpango mkakati na kuupeleka bungeni ili utungwe sheria zenye manufaa kwa wananchi,” amesema.
Aidha, Angasi amekosoa tabia ya kuchagua wabunge kwa misingi ya umaarufu au uwezo wa kifedha bila kuzingatia elimu na uelewa wa masuala ya kisheria na kiuchumi.
“Haiwezekani mtu mwenye elimu ya darasa la saba, kwa sababu tu anajua kusoma na kuandika, anazo fedha na anajua kuzungumza vizuri, apewe jukumu la kutunga sheria za kuongoza taifa. Bunge ni chombo nyeti kinachopaswa kuwa na watu makini,” amesisitiza.
Angasi amehimiza Watanzania kuwaamini vijana waliobobea kutoka vyuo vikuu na vyuo vya kati, kwa kuwa wanaweza kuibua mipango madhubuti ya kulisaidia taifa kwa nguvu na maarifa yao.