Mwanafunzi afia kambini JKT Tabora

Mwanafunzi afia kambini JKT Tabora

Mwanafunzi wa kidato cha sita kutoka shule ya sekondari Loyola Halima Kitangila amefariki dunia huko Msange Tabora JKT kwa madai ya kuugua maleria.

My take
Kuna haja ya serikali kuangali utaratibu wa mafunzo hasa kwa watoto wa kike ambao hawaendi JKT kujitolea. RIP Halima.

Source: Tanzania Daima


Kule boarding schools kuna vifo vya wanafunzi kutokana na maradhi mbalimbali. Wapo pia wanafunzi wa day schools ambao hufia mikononi mwa wazazi/walezi wao kutokana na maradhi sasa utatwambiaje wanafunzi wakifa katika makambi ya JKT basi utaratibu uangaliwe upya(ufutwe?)????

Lete basi hapa na takwimu za wanafunzi wanaofia mashuleni na majumbani kwa mwaka tupate ulinganifu kama hutasema huko nako utaratibu uangaliwe upya.
 
Ni kwenye makambi ya JKT tu amabako huwezi kutumia net ya mbu kwa sababu hakuna sehemu ya kutundikia na hata mazingira ni mabovu. Pili ni vema wakaelewa watoto wa sasa ni kwenda nao taratibu kwani hawajazoea mazingirz ya shuruba ghafla ghafla. Waanze nao taratibu hadi wazoee na siyo kuwapigisha shuruba za mfululizo la sivyo watakufa wengi.
 
Hakika jeshini wanacheza sana na afya za binadamu. Nakumbuka miaka yetu ukiumwa kwanza hadi upewe pass ya kwenda hospital hiyo process tu unaweza kufa. Na kama unaumwa kiasi gani hakuna chakula cha wagonjwa. Wenzetu walikufa sana kwa uzembe. Yaani udhaifu, udhaifu kila eneo.
​ ulikuwa selule mkuu, vifo hata uraiani vinatokea kwa nini jeshini iwe nongwa...
 
mambo za kulazimishana jeshi karne hii azifai.
kuna tetesi uko magonjwa mengi watoto awalali vizuri
ukiumwa wanajua unazarau na unapata mateso zaidi.

wazaz mliopeleka watoto uko mshtuke. msije kupoteza watoto wenu.

Mimi nilikuwa jeshini, huko ukiugua kwanza unaanza kunyimwa chakula hivyo ni lazima utadhoofika tu, siri moja ya jkt ni kwamba ukiugua homa kali toroka mara moja usichelewe, bora urudi ufungwe
 
​ ulikuwa selule mkuu, vifo hata uraiani vinatokea kwa nini jeshini iwe nongwa...

"Hospitalini" kwenyewe watu wanakufa, iwe Tanzania, India, Ulaya au Marekani kwenye "mabingwa" wa tiba. Huko jeshini kuna nini cha kuzuwia vifo hasa kama vinavyotokana na malaria kwenye ukanda wetu?!!
 
Kama wenyewe viongozi wameenda jkt na uzalendo hawana,kazi ufisadi na ufataki,je hawa itakuwaje??,,,waseme tu ukweli kuwa jeshi linahitaji watu waliopitia mafunzo kwani vita vinanukia
 
Atachukuliwa hatua za kisheria ikiwa ni pamoja na kukosa uwezo wa kudahiliwa vyuoni.
Siyo enzi za ujima. Vyuo binafsi vipo kibao na vya nje ya nchi vipo kibao. Ila mi mwanangu nitamwambia awe jasiri akilemewa atoroke, na akifa nitahakikisha naenda kuwaua askari waliohusika kwa njia yeyote iwe risasi au njia nyingine. Inatia hasira, nikuze mtoto then aje auawe na wanajeshi! shit zao.
 
Kule boarding schools kuna vifo vya wanafunzi kutokana na maradhi mbalimbali. Wapo pia wanafunzi wa day schools ambao hufia mikononi mwa wazazi/walezi wao kutokana na maradhi sasa utatwambiaje wanafunzi wakifa katika makambi ya JKT basi utaratibu uangaliwe upya(ufutwe?)????

Lete basi hapa na takwimu za wanafunzi wanaofia mashuleni na majumbani kwa mwaka tupate ulinganifu kama hutasema huko nako utaratibu uangaliwe upya.
Acha ulimbukeni wewe. Jeshini ni Ubakaji+Uuaji. Hii kitu itakuja kuigharimu serikali. Mimi mwanagu afie huko mbona hapatatosha.
 
Hakuna jkt wanaenda kubaka na kuwapa ukimwi tu watoto wa watu
 
Hapa kinachozungumziwa mategemeo sio unafuu wa janga. Mtoto ni mtoto kwa mzazi.

Aliyepata divn foo hafai kuwa "tegemeo"?
Halafu kama mategemeo ni tofauti, inawezekanaje tena mtoto kuwa mtoto tu kwa mzazi?!!
 
Its very sad! Lakini hatuna haja ya kutuhumu moja kwa moja JKT is there no people who are dying at Muhimbili hospital. Kifo ni wajibu kikikuita haukatai. Japo inauma. Swala la kufanya uchunguzi ni kuonesha kutokuliamini jeshi hilo.
 
Shiittt!! Asije kuwa alibakwa, wazazi/ndugu waombe uchunguzi. R.I.P
Pia wanajeshi huwa hawana muda mtu akiugua mi nadhani huyo marehemu alionesha dalili na wao wakadharau.

Unadhani? sema unachokijua
 
Ndio maana wanangu hawatoenda huko hata iweje. Hawajaona mafunzo ya maana wanaenda kuwafundisha mambo ya kuiba kura wakati wa uchaguzi, haendi nooooo!
 
Acha ulimbukeni wewe. Jeshini ni Ubakaji+Uuaji. Hii kitu itakuja kuigharimu serikali. Mimi mwanagu afie huko mbona hapatatosha.


Story za vijiweni hizi kupotezea muda kusubiria wali wa mama Mudawote. Wake up!!!
 
Last edited by a moderator:
​ ulikuwa selule mkuu, vifo hata uraiani vinatokea kwa nini jeshini iwe nongwa...

Mkuu sikuwa Selule, nilikuwa mchapa kazi kiasi kwamba walinipa jina kabisa. Niliugua mara moja tu, tena tukiwa tumeshaukana ukuruta. Nilikuwa nawaona wale wanaougua, kuna selule kweli na wale genuine wagonjwa ila huduma ni mbovu sana. Kombania walikuwa wanachukulia mzaha sana kwa askari kuruta kuugua, kwa hiyo kufa ilikuwa ni rahisi sana.
 
Back
Top Bottom