Mwalimu wa Shule ya Msingi aliepata Div IV ya Pts 28 kidato cha nne anaandaa msomi gani hapo baadae?

Cheche Mtungi

JF-Expert Member
Nov 14, 2010
2,619
771
Mimi nashindwa kuelewa kwa nini walimu wanaofundisha shule za msingi na kidato cha nne wanachukuliwa wale waliopata alama za chini?
1.Grade A:Mwalimu aliepata divisio iv ya pts 28 anachaguliwa kuwa mwalimu,atamuandaa vipi mwanafunzi wakati mtu huyu uwezo wake sio mzuri?
Kwa nn tusiangalie mifumo ya kuchukua walimu kama ilivyo kwenye taasisi za elimu ya juu?
 
Hii inawezekana Tanzania tu! Na ndiyo moja ya mafanikio tunayoambiwa tusiyabeze!
 
Utasikia kauli kama 'walimu ni wito'...WTF!! Failures=Teachers nijitahidi kuulewa huu mlinganyo lakini wapi natoka kapa.
 
Halafu walimu hao hao wakifaulisha watoto wasio jua kusoma wala kuandika serikali inakuja juu na kuanza kuwachunguza?!
 
Si hilo tu, bali hata huyo mwenye division IV ya 28 ametumia cheti hicho kufanya mtihani wa form six na baadae kujiunga na elimu ya juu (Universities) - si unajua vyuo vikuu siku hizi vingi. Mkuu fanya utafiti mdogo utagundua hili.....!!1
 
Yeah sidhani kama mko sahihi! Mwalimu huyu ni mzuri! Hiyo ni social stratification from anthropology point of view. Me nachukua B.sc lakini mwalimu alie nifundisha msingi hana hata diproma BUT anafaa level ile. Kwani hajui 1 2=3? Dat y hajaambiwa akafundishe olevel.
 
Yeah sidhani kama mko sahihi! Mwalimu huyu ni mzuri! Hiyo ni social stratification from anthropology point of view. Me nachukua B.sc lakini mwalimu alie nifundisha msingi hana hata diproma BUT anafaa level ile. Kwani hajui 1 2=3? Dat y hajaambiwa akafundishe olevel.

Umeona eh? Kwamba alifaulu primary lakini akashindwa kufaulu sekondari siyo? Kwamba ana uwezo wa kuwafundisha praimare skul pyupils kufaulu praimare kama alivyofaulu yeye, siyo? Ahaaa.... nimeelewa sasa.
 
Mfumo wetu wa elimu ni mbovu sana, na unazalisha watu wabovu. Ukiangalia elimu ya TZ kwa ujumla aliyefeli na aliyepasi wote ni zao lile lile, iweje mtu afaulu kwa wizi wa mtihani, au kwa kukariri majibu tu. Zao la elimu yetu siyo critical, analytical wala visionary.

Kufeli ni tatizo moja na kukata taaa ni tatizo lingine, kwenye aisha hakuna kufeli kun -changamoto. Haiingii akilini mtoto kufeli masomo lazima kuwe na sababu za msingi, na hawa watoto tuna wa brabd failure wanakuwa anyo na kuikubali. Tubomoe mfumo wetu wa elimu sioni kama mitihani ya form four na six inatija kwani haipi uwezo halisi wa watoto wetu.

Haiwezekani mtoto alikuwa na maendeleo mazuri kwa miaka minne akafeli mtihani mmoja tu ukawa amepoteza miaka yake yote miine bure. Kama alifaulu form one, two, three lazima kuwe na sababu za msingi sana kufeshindwa mtihani mmoja tu wa mwisho kwenye somo husika.

Badala ya bkupigia kelele haya madara ya kufaulu je hata hao waliofaulu wanatofauti gani na hao walioshindwa?? Je hao wanaomaliza vyuo vikuu wanatofauti gani na hawa wa form six?? Elimu yetu inatayarisha wataalamu na watengeneza ajira au linazalisha mzigo kwa taifa. Kwa nini kila kada awe daktari au injinia yuko tayari kufanya kazi voda kwa kisingizio cha ajira hawawezi kujiajiri. Majibu ni elimu yetu haiandae kizazi kujitegemea.

Division mbovu tutaendelea kuziona sana na zitatuhudmia kwani ndio wengi tunaozalisha kwa ukosefu sio wa waalimu wabovu tu bali shule, mitaala, ukosefu wa vitabu nk vibovu.

Sio waliofeli tu wanatufundisha bali wanatutibu, wanatujengea nyumba zinazoanguka, wanatutawala, wanatuendesha, wanatutengenezea vyakula, ndio tunaowategemea sana halafu tunashangaa nchi haiendelei. Itaendeleaje wakati tumeandaa vihiyo watupu.

Mfumo wa elimu yetu ni mbovu sio alama ndio tatizo.
 
Hii inawezekana Tanzania tu! Na ndiyo moja ya mafanikio tunayoambiwa tusiyabeze!

msomi aliyebora ni yule anayeliona tatizo na kulitolea utatuz sasa watu weng mnaishia kusema ooh imepanda imeshuka,ok mnipe mfano wa nchi yoyote duniani ambayo wale waliofaulu for instance kwa kupata division I na II form 4 wanaenda kufundisha,alafu nani aende form 5&6?nani aende vyuo vikuu?
Anayefaulu vizur lazima aendelee acheni kuongelea vitu visivyowezekana.eti mwenye 1 na 2 akafundishe!!!alafu mwenye 4 ndo aende advance.mweeeee
 
Yeah sidhani kama mko sahihi! Mwalimu huyu ni mzuri! Hiyo ni social stratification from anthropology point of view. Me nachukua B.sc lakini mwalimu alie nifundisha msingi hana hata diproma BUT anafaa level ile. Kwani hajui 1 2=3? Dat y hajaambiwa akafundishe olevel.

ndo wasomi tulionao wanaishia kuropoka tu,haya mambo ndo yanavyoenda kote dunian,wakishayasikia mtaan wanayaleta vivyo hivyo bila kupima,haya waje watetee hoja yao
 
certification ndicho mnachokzngatia bt reality c kwel na mtihan c kpimo pekee cha kumtahn m2 right?organization,presentation of material ndo mpango na ualimu its all about proffsonalism na co kupata 1,2,3,4 au 0..
 
msomi aliyebora ni yule anayeliona tatizo na kulitolea utatuz sasa watu weng mnaishia kusema ooh imepanda imeshuka,ok mnipe mfano wa nchi yoyote duniani ambayo wale waliofaulu for instance kwa kupata division I na II form 4 wanaenda kufundisha,alafu nani aende form 5&6?nani aende vyuo vikuu?
Anayefaulu vizur lazima aendelee acheni kuongelea vitu visivyowezekana.eti mwenye 1 na 2 akafundishe!!!alafu mwenye 4 ndo aende advance.mweeeee

Darasa langu (Dipl Ed) 1993 - enzi hiyo ikiwa ni Dar es Salaam Teachers' College na waziri wa Elimu akiwa Prof Sarungi - mtu mwenye score ya chini kupata admission ilikuwa ni Div III. And I went on to teach and am still teaching. Unataka mfano mwingine?
 
Suala siyo serikali inachukua waliofeli bali hao ndiyo walioomba ualimu. Kama wewe una div. 1 omba ualimu uone kama utaachwa. Kingine kama maslahi ya walimu yakiboreshwa ina maana watu wengi watapenda kusomea ualimu na hivyo serikali inaweza kuwa na jeuri ya kusema ualimu mwisho div.3
 
Bora hawa wamegusa walau O-level. Unakumbuka wale walimu wa UPE(Ualimu Pasipo Elimu - jus a kid) ambao wengi wao ni std vii na mpaka leo wapo na hawa ndo wamenifundisha na leo najivunia kadegree kangu kako poa. :coffee:
 
Nyie mnaomsapoti huyu jamaa hamna busara na mko kisiasa:;........Nyie na degree zenu shule ya msingi mlisomea London::::::wote mmefundishwa na hawa.:::::ni ukosdfu wa adabu kumjadili mwalimu::watoto wenu mnawapeleka international tunawapiga bao university
 
Umeona eh? Kwamba alifaulu primary lakini akashindwa kufaulu sekondari siyo? Kwamba ana uwezo wa kuwafundisha praimare skul pyupils kufaulu praimare kama alivyofaulu yeye, siyo? Ahaaa.... nimeelewa sasa.

hiyo ndo point mkuu, ndomana kwa chuo kikuu, ma TA wanachukuliwa wale walofaulu vizuri coz wanafundisha watu wa leval sawa na yao.
 
Mimi nashindwa kuelewa kwa nini walimu wanaofundisha shule za msingi na kidato cha nne wanachukuliwa wale waliopata alama za chini?
1.Grade A:Mwalimu aliepata divisio iv ya pts 28 anachaguliwa kuwa mwalimu,atamuandaa vipi mwanafunzi wakati mtu huyu uwezo wake sio mzuri?
Kwa nn tusiangalie mifumo ya kuchukua walimu kama ilivyo kwenye taasisi za elimu ya juu?

Na ndiyo huyo huyo aliyekufaulisha wewe hata kupata jeuri ya kuja kuhoji uwezo wa huyo mwalimu. Au wewe hukufundishwa na walimu wa UPE? Wale waliokuwa wanamaliza darasa la saba na kurudi kuwafundisha darasa la saba wenzao? Je hao wanaofundisha universities na kwingineko mnakoona nyie ndiyo kwa maana sana hawakufundishwa na hao walimu wa UPE? Acheni dharau zisizo na mpangilio bwana. Nipeni mfano wa nchi ambayo walimu wa shule ya msingi ni wale waliopata div 1. Hata ulaya wanaokwenda kusomea ualimu ni wenye low grades za ufaulu ukilinganisha na fani nyingine kama udaktari, uanasheria na engineering. For years tumepata wataalamu wa kila aina kutoka kwa walimu hawa hawa mnaohoji leo uwezo wao.
Nawahakikishieni kwamba tatizo la elimu Tanzania halitokani na mwalimu kapata div ngapi bali linatokana na sera mbovu za maendeleo ya elimu nchini, ikiwemo ukosefu wa motisha kwa walimu.
 
Back
Top Bottom