Kwa mtazamo wangu,mtoto aliyepigwa hadi kufa huko Kagera alionewa sana,sana sana!!
Mwalimu aliyekuwa anatoa adhabu kwa mtoto yule anastahili adhabu kabisa,kwa sababu kitendo cha mtoto kumpokea mwalimu wake mizigo kilitosha kutambua tabia ya mtoto kabla ya kumuadhibu vikali.
Jambo la pili,kwa umri wa mtoto yule,hakuwa na uwezo wa kujitetea kwa kumkuda mwalimu wake,kwa hiyo mwalimu kuendelea kumpiga ni kujitoa ufahamu,na MAKUSUDI!(MWALIMU YULE AADHIBIWE TU,UMRI WA MTOTO NA KIPIGO CHA NAMNA YA ILIVYOSIMULIWA,SI JAMBO LINALOVUMILIKA)
Kwa upande wa kanuni za namna ya kuadhibu mwanafunzi shuleni,zinaweza kutekelezeka pasipo tatizo kwa watoto wenye kujielewa (waliolelewa kwa maadili ya heshima na wazazi wao)
Kwa watoto ambao kwao heshima si kipaumbele,(kuanzia kwa wazazi wao) hizi kanuni hazitekelezeki,(hasa sekondari) ambako mtoto ukimuita anaweza akagoma kuja,ukimfuata anaokota mawe,na kukutwanga nayo!(wapo watoto wa namna hiyo).
Mwanafunzi wa kidato cha tatu,anakuja shule asubuhi akiwa amevuta bangi,amekaa darasani hana daftari hata moja,ukimwambia habari ya kwenda kwa mkuu wa shule sijui kumtoa darasani,anaanzisha varangati,muda huo anajiona yeye ni Van Dame, au John Sina!
Application ya kanuni na sheria kwenye mazingira hayo ni ngumu sana,mwisho wa siku ni hisia na hasira huchukua nafasi!
Nadhani,ili kuweka sawa mambo haya,watoto wa aina ya kuvuta bangi,na watukutu kupindukia,wafukuzwe shule mara moja,(mamlaka hayo ipewe kamati ya nidhamu shuleni),kwa sasa mwanafunzi hawezi kufukuzwa shule mpaka bodi ya shule ikae,(na sijui huwa wanakaa mara ngapi kwa mwaka).
Lakini kwa utaratibu wa sasa,ambapo nasikia mwanafunzi hafukuziki shuleni mpaka bodi ya shule ikae na kuamua,kuna watoto wataendelea kuaumbua sana walimu huko mashuleni.
Wasalaam!
Sent using
Jamii Forums mobile app