Kwa mazingir ya elimu ya bongo bila tuit hutoboi labda uwe unasoma huko feza lakin kwa hzi school za kata lazima ujiongeze maana vitu ni vingi sana muda mchache ukichek hao Necta hawachagui topic so lazima zote ziwe kichwani
Sikweli , ni bidii na kujua kutumia resources zinazokuzunguka na zilizopo
Nitoe mfano mm ,nilichaguliwa kutoka O level kata , nikapelekwa shule ya A level kata hapo pwani , ndio sisi tuliianzisha , mazingira si rafiki, tulichaguliwa 100 kufikia wiki 3 tumebaki 70.
Likizo 99% wanaenda dar kwenye hizo twishen za kina Mgote , muddy , n.k
Binafsi sikuwa na hela nami nilitaman kusoma hizo teisheni, hivo wenzangu wanapoelekea dar ,mm narudi kwetu iringa
Mwisho wa siku necta ilitoa majibu , mm nilipenda kucheza na akili za necta, nilicheza sana na past papers, review , practicals , na kila topic nilipenda kujua key points hasa ,
Mwisho wa siku tuliopata Marks nzuri za juu tulikuwa wawili na tulienda UDSM, wengi walipata div 3 ,wakajazana udom n.k
Hivo sikweli kuwa bila twishen hutoboi ,ni kujipanga
Amin nakuambia Necta ya Tz ni past papers , jitahidi kila topic kuipiga mwenyewe kwa kutumia resources mbali mbali utaielewa tu , then zama kwenye review
Necta hawachomoki