WAZIRI wa Uchukuzi, Dk Harisson Mwakyembe amewataka wadau wa usafiri wanaojadili sera ya reli kutumia utaalamu na uzoefu walionao kupanga aina ya daraja la reli ambayo Tanzania inaweza kuwa nalo na namna itakavyonufaika.
Mwakyembe alitoa kauli hiyo jana alipokuwa akifungua washa ya siku mbili ya wadau wa reli inayokutana jijini Dar es Salaam kupitia na kujadili mapendekezo ya kamati ya uandaji sera ya reli nchini itakayotumika kama muongoza wa usafiri huo hapa nchini.
Akizungumza kwenye uzinduzi huo, Dk Mwakyembe alisema wadau hao wanapaswa kutumia utaalamu na uzoefu wao kupata aina ya reli itakayotumika nchini lakini pia kutengeneza sera itakayosaidia kurejesha hadhi ya usafiri wa reli nchini ambao kwa sasa umepoteza mvuto.
Umuhimu wa usafiri wa reli katika kukuza uchumi katika kila Taifa duniani uko wazi, kwa hapa nchini siku za nyuma reli ilisaidia kusafirisha mizigo na pia abiria, wananchi walinufauka na gharama nafuu na pia urahisi wake,lakini baada ya ubinafisishaji wa reli ya kati na pia Tazara usafirishaji wa watu na mizigo umekuwa na changamato kubwa, alisema Mkwakyembe na kuongeza:
Pamoja na ukubwa wa nchi yetu na ongezeko la watu wanaokadiriwa kuwa zaidi ya 40 wamekosa huduma bora ya usafiri wa mizogo na abiri hali hiyo imewakosehsa huduma bora za kiuchumi ambazo ni muhimu kw amaendeleo yao na Taifa kwa ujumla, alisema.
Alisema nchi imewekeza kwenye barabara ambazo ni gharama kwa kusafirisha mizigo na hata kuzihudumia na wakati huo huo ni rahisi kuharibika na kuliingizia hasara ya matengenezo ya mara kwa mara.
Kwa sasa Tanzania inashindwa kunufaika na fursa ya kibiashara iliyopo baina ya nchi sita jirani ambazo hazijapakana na bahari za Uganda, Burundi, Rwanda, Malawi Zambia na Jamhuri ya Demokrasia ya Kongo kutokana na kukosekana na usafiri wa reli kutopewa kipaumbele, ninafikiri Tanzania kutokana na hali nzuri nya kijografia inaweza kunuafaika na aina hiyo ya usafiri.alisema Dk Mwakyembe.
CHANZO: http://moses-ayoub.blogspot.com/
Mwakyembe alitoa kauli hiyo jana alipokuwa akifungua washa ya siku mbili ya wadau wa reli inayokutana jijini Dar es Salaam kupitia na kujadili mapendekezo ya kamati ya uandaji sera ya reli nchini itakayotumika kama muongoza wa usafiri huo hapa nchini.
Akizungumza kwenye uzinduzi huo, Dk Mwakyembe alisema wadau hao wanapaswa kutumia utaalamu na uzoefu wao kupata aina ya reli itakayotumika nchini lakini pia kutengeneza sera itakayosaidia kurejesha hadhi ya usafiri wa reli nchini ambao kwa sasa umepoteza mvuto.
Umuhimu wa usafiri wa reli katika kukuza uchumi katika kila Taifa duniani uko wazi, kwa hapa nchini siku za nyuma reli ilisaidia kusafirisha mizigo na pia abiria, wananchi walinufauka na gharama nafuu na pia urahisi wake,lakini baada ya ubinafisishaji wa reli ya kati na pia Tazara usafirishaji wa watu na mizigo umekuwa na changamato kubwa, alisema Mkwakyembe na kuongeza:
Pamoja na ukubwa wa nchi yetu na ongezeko la watu wanaokadiriwa kuwa zaidi ya 40 wamekosa huduma bora ya usafiri wa mizogo na abiri hali hiyo imewakosehsa huduma bora za kiuchumi ambazo ni muhimu kw amaendeleo yao na Taifa kwa ujumla, alisema.
Alisema nchi imewekeza kwenye barabara ambazo ni gharama kwa kusafirisha mizigo na hata kuzihudumia na wakati huo huo ni rahisi kuharibika na kuliingizia hasara ya matengenezo ya mara kwa mara.
Kwa sasa Tanzania inashindwa kunufaika na fursa ya kibiashara iliyopo baina ya nchi sita jirani ambazo hazijapakana na bahari za Uganda, Burundi, Rwanda, Malawi Zambia na Jamhuri ya Demokrasia ya Kongo kutokana na kukosekana na usafiri wa reli kutopewa kipaumbele, ninafikiri Tanzania kutokana na hali nzuri nya kijografia inaweza kunuafaika na aina hiyo ya usafiri.alisema Dk Mwakyembe.
CHANZO: http://moses-ayoub.blogspot.com/