Mwakyembe amshushua Tundu Lissu...

Mwakyembe amshushua Tundu Lissu...

Na kabla ya Tundulisu kuvuliwa degree yake iff possible wan ndio wajivue za kwao na udr, uprofesser wao kwa kumu award incompetent student degree na pia kumfundisha vibaya mpaka kufikia hatua ya kudanganya Taifa. Hili sio tatizo la Tundulisu ila la walimu wa Tundulisu.
 
Mwakyembe kama wengine wote wa kijani maana akili zao wote zinatunzwa kwenye bakuli la mwenge, mwenge ukiwashwa tu akili zao zinaungua mle ndani matokeo wanakana hata akili zao wenyewe chezea kijani, chezea ccm banaaa weee
 
tundu lisu kapotezwza mbayaa hahaha duhhhhhhh aibu aibu aibu kuu
 
Namnukuu dr mwakyembe akihoji kitabu chake kutumiwa vibaya na tundu lissu "Mh mwenyekiti huwezi ukakisoma kitabu hiki kwa haraka haraka ukakielewa kama unavyosoma gazeti la Tanzania Daima"

QUOTE]

Kweli CCM is a mental disease, badala ya huyu Dr. Mwakyembe kujificha kwenye hiyo statement tata atwambie katika alikuwa anamaanisha nini aliposema the ONLY alternative is three government. "Asijimwamba fai" kwamba kitu alichoandika kwenye kitabu chake ni kigumu kueleweka. Watu tunasoma nuclear physics tunaelewa hiyo DS yake kwenye kitabu ndiyo iwe ngumu kueleweka?!. Huyu Dr. bure kabisa, wala hana hadhi ya kumjibu TL.

UMENENA MUUNGWANA KUNA HAJA YA WAUNGWANA KUANZA KUIATA KOLEO NI KOLEO NA SIO UMA KUBWA
 
Huyu mwakyembe ni mpuuzi kabisa wala hajajibu hoja ya Tundu Lissu anaropoka tu kama walivyo wenzake na ndio maana hao hao ambao leo hii anawaunga mkono walitaka kumuua kwa sumu -------- sana wewe mwakyembe Lissu kasema kuwa hakuna popote pale ambapo panaonyesha kuwa serikali ya mapinduzi ya zanzibar likiwemo baraza la wawakirishi kulidhia muungano huu. Wewe unaishia kuharisha tu, wewe kweli ulistahili kufa tu mnafiki mkubwa wewe na ndio maana kwenye ripoti ya richmond ulificha baadhi ya taarifa ili kumnusuru kikwete kubwa jinga wewe.
 
Nilitegemea Mh Mwakyembe angefafanua alichomaanisha kwenye andiko lake la PHD na hata kama ni kupinga kwa kipindi hiki ambapo Zenj wameshakuwa nchi yaenye mamlaka kamili.

Ni ngumu sana unapotaka kwenda na mkumbo wa wenzako wakati imani yako moyoni iko tofauti. Mlio mjengoni simamieni haki ya Watanzania na Mungu atawawezesha kufikia malengo. La sivyo siku zaja mtasema mbona hatukukubaliana na maamuzi fulani? Hapo ndio kutakuwa na kulia na kusaga meno!

Wasomi mmetuangusha sana sana kwa sababu hamsemi yaliyo moyoni mwenu mnatoa ya kuambiwa na kwa jinsi hii mnaonekana kwamba elimu yenu hamuitumii ipasavyo.
 
Namnukuu dr mwakyembe akihoji kitabu chake kutumiwa vibaya na tundu lissu "Mh mwenyekiti huwezi ukakisoma kitabu hiki kwa haraka haraka ukakielewa kama unavyosoma gazeti la Tanzania Daima"
Aisee Wasomi wetu huwa nawafurahia saaaana, kwani hicho kitabu amekiandikaje mpaka kisieleweke? Ina maana watu wote humu hamna hata mmoja mwenye copy? tuleteeni copy tuone ugumu wa kukisoma kama anavyodai mwandishi. Halafu tutachangia vizuri, bila hivyo tutakuwa bias.
 
Tunaomba mwenye nakala ya ukurasa alionukuu Lissu atuwekee hapa
 
Ushabiki mwingi humu "closed mind"

bora umeliona hilo mkuu! Watu hawajengi hoja kaz yao ni kukejeli tu kama wanahoja za kumkosoa Mwakyembe waziweke wwaz au kama wanazo hoja za kumkosoa au kumuunga mkono Lissu pia waweke wazi....... Waseme kwavp Lisu ni mpotoshaji au kivip Mwakyembe anapotosha..... Watu wamejaa ushabiki wa vyama tu
 
Mwakyembe anataka kukataa kauli yake kweli ccm ni kiboko anaogopa kuoza huku akitembea -------- sana huyu.pia ni mnafiki mno huyu kweli lissu asikielewe kitabu chake kwani kakiandika kwa lugha ya kinyakyusa? Aibu kwake na ccm nzima. Kazi ya kuondoa utawala wa intarahamwe madarakani bado ni ngumu ila time will tell.
 
Ile sumu iligusa kwenye IKULU YA MWAKYEMBE kwisheni - 😕 HAJITAMBUI
 
Is this real from a phd holder ?
Truth is self-sustained !

With due respect, I would replace 'Sustaining' instead of the underwritten word, Otherwise I concur with a substantial point you intended to deliver!.
 
Mwakyembe kwa sasa ni kama walivyo wajinga wengine ndani ya ccm wanaogopa s3 kwa kuwa maslahi ya ccm yanakufa kifo cha mende. kama baba yako alijenga nyumba ya nyasi sio dhambi wala matusi wewe ukimjengea nyumba ya kisasa. Sasa hawa wanafiki eti tuwaenzi wazee wetu ila ni hawahawa walio liua azimio la arusha sasa sijui wanamuenzi vipi mwalimu. Huuu ndio tunaita upumbavu wa kupitiliza.
 
kama seif hamad alisema kiongozi unatakiwa usimamie maneno yako,je,mwakyembe amesimamia yale aliyoya andika ktk kitabu chake kilichonukuliwa na lissu?,na kama lissu hakusema ukweli je mwakyembe amekanusha kuwa hajaandika kilichosemwa!,kama kunyang'anywa digrii waanze na yeye anayekana maandishi yake.kuhusu eti mwalimu hakufundishi kila kitu kwa kuwa utamzidi huo ni upuuzi na ndio maana hili taifa linakuwa masikini kila uchao sababu ya ubinafsi.du!,kumbe udsm wanatoa digrii za vijarida!,aibu kwa wasomi wa nji hii.

unaweza kutuletea link ya kitabu cha mwakyembe? Ili na ss tujue unafki wake!
 
Sikutegemea nae mwakyembea awe bomu hivyo.. Kitabu umeandika wewe..tena kwenye huo mstari umetumia neno..3 government is the ONLY way.. Leo unakana kwa sababu ya siasa za kipumbavu za ccm..kweli bongo tumelaaniwa

Umelaaniwa wewe na UKOO WAKO
 
Kwa muda mrefu nimekuwa nikimchukulia Dr Mwakyembe kama mwanasiasa aliye tofauti na wanasiasa wengine wengi ndani ya Chama cha mapinduzi japo utendaji wake kwenye nafasi yake ya uwaziri si ya kuvutia sana.

Kitu kimoja ambacho sikuwahi kukijua kuhusu huyu mheshimiwa ni juu ya tabia yake ya majivuno kutokana na usomi wake.Nilimshangaa sana jana kwa jinsi alivyokuwa anawasilisha hoja yake ya kutetea serikali mbili,Mheshimiwa Mwakyembe alitumia muda mwingi kuwakejeli akina Lissu na Jussa kutokana udogo wa umri wao na viwango vya elimu yao kuliko kujadili hoja zao.

Ni dhahiri Dr Mwakyembe alikuwa amefadhaika sana kwa kuumbuliwa juu ya unafiki wake sasa akawa anatafuta namna jinsi ya kujinasua kutoka kwenye aibu ile,Kwa bahati mbaya sana alishindwa kuwahakikishia wenzie ndani ya Bunge kama kilichosemwa na wapinzani juu ya msimamo wake wa kuunga mkono muungano wa serikali tatu kwenye ile THESIS yake wakati ana-persue Ph.D yake nchini Ujerumani kama ni kweli ama la.Kusema kweli hakuna hoja ya maana Dr Mwakyembe aliyoiongea kupangua hoja za akina Lissu zaidi ya mashambulizi binafsi na majivuno.

Tukiachana na hayo ya utetezi wake wa kukana kwamba hakuwahi kuunga mkono muungano wa serikali tatu.Ebu tugeukie kwenye utetezi wa Dr Mwakyembe juu ya muungano wa serikali mbili.Hapa pia aliutumia muda mwingi kujisifia kuhusu usomi wake na kushiriki kuandika vitabu mbalimbali akishirikiana na wasomi wengine kama akina Prof Issa Shivji,Kweli rangi nyeusi inayoishi Afrika haiwezi kuacha asili yake ya ulimbukeni hata siku moja.Kwa namna ninavyofahamu wasomi wengi duniani ambao wamepata fursa wamefanya mambo makubwa sana kwenye jamii zao na ulimwnguni kwa jumla.

Mfano Dr Carson,The NEURO SURGEON amefanya mambo makubwa kwenye kuboresha matibabu ya ubongo,Hawa ndiyo watu ambao hata wakijisifia kuwa wamesoma utakubaliana nao kwasababu wanastahili lakini kamwe hutawasikia akina Dr Ben Carson wakijisifia kuwa wao ni wasomi kuliko wengine isipokuwa matendo yao yanaongea mengi na hata kujizolea sifa lukuki ulimwenguni.

Nikirudi kwa wasomi wetu wa Afrika kusema kweli wanakera sana.Wao wanadhani kukusanya vyeti kutoka vyuo mbalimbali na kujifungia library kuandika vitabu wakitumia kazi za watu wengine ndiyo wamemaliza wajibu wao wa kulijenga Bara la Afrika.Leo Mwakyembe anaposimama pale Bungeni na kuanza kukejeli elimu za wenzake na kujisifia kwamba yeye amesoma sana kwakweli inasikitisha sana.

Sisi hatukutaka kujua kuhusu elimu yake au kama aliandika vitabu,Tulichotaka kujua ni kama ni kweli aliunga mkono muungano wa serikali tatu kwenye THESIS yake wakati anasomea Ph.D yake nchini Ujerumani?Na jambo jingine tulilotaka kujua ni kwanini anatete muungano wa serikali mbili basi.

Tulichokishuhudia pale Bungeni ni Dr Mwakyembe kujaribu kutaka kupimana msuli na Lissu kwenye tasnia ya sheria,Kiuhalisia Dr Mwakyembe anatishwa na uwezo wa Lissu katika kuzichambua sheria na kwakuwa asili ya huyu mheshimiwa ni kutaka kujiona yuko ya wengine kwahiyo sehemu salama kwake ilikuwa ni kukimbilia kwenye Ph.D yake.

Hakuna asiyejua kuwa Tundu Lissu amefanya mambo mengi ya kutukuka kwenye medani ya sheria hata kabla hajawa Mbunge.Lissu anazifahamu sheria za nchi hii practically.Nikija kwa mheshimiwa Mwakyembe sikumbuki aliwahi kufanya nini cha kukumbukwa katika nchi hii zaidi ya kushika chaki darasani.Nje ya taaluma yake ya ualimu hakuwahi kufanya jambo lolote la kujivunia.

Kimafanikio kwenye medani ya sheria Lissu amefanya mambo mengi makubwa kuliko huyu mheshimiwa kwasababu Lissu amefanya kazi za uanasheria kwenye mahakama mbalimbali kwahiyo anafahamu vyema anachokipigania,Tofauti na Dr Mwakyembe ambaye anazifahamu sheria za nchi hii kinadharia zaidi.Natamani kumwona Dr Mwakyembe akisimama mahakamani akimtetea mtu au akitetea upandea wa pili halafu akashinda kesi,Mpaka atakapoanza kuyapata mafanikio ya kweli ya kutoa msaada wa kisheria kwa wengine kama afanyavyo Lissu ndipo tutakapoanza kumpa heshima anayotamani apewe.

Amepewa uwaziri wa mawasiliano na uchukuzi na sijaona kipya alichokileta kwenye sekta hiyo pamoja na kusoma kwake sana.Ifike wakati wasomi wa Afrika wabadilike sasa,Badala ya kukaa na kujisifia juu ya usomi wao ingekuwa busara kama wangeutumia usomi wao kuifanya Afrika sehemu bora ya kuishi duniani.

Namsifu Tundu Lissu kwa kujaribu kufanya kile wasomi wengi wanashindwa kukifanya katika nchi hii,Nacho ni kusimama na wanyonge na kupambana na mfumo kandamizi unaowanyima fursa Watanzania kutimiza ndoto zao.

Kwetu sisi Tundu Lissu ndiye msomi mwenye manufaa kwa nchi hii anayeitendea haki elimu yake na ndiye tunayemuamini na kumsikiliza zaidi kuliko hao wasomi wengine uchwara.
 
Mwaka 92 ni hawahawa ccm walisema wapinzani wataanzisha vita leo hii ni hawahawa wanasema eti s3 jeshi litapindua serikali, kwani hiyo ndiyo kazi ya jeshi? Kupindua serikali na huu ni muendelezo wa upuuzi wa ccm ili kuwaogopesha wananchi hawa ccm wanajoinakuwa wao ndio wenye hati ya kutawala. Hakukosea prof Lipumba alipo wabatiza jina la intarahamwe hakika hawa ni intarahamwe.
 
Hiki ndicho alichochangia Dr Mwakyembe?

Maana yake sijaona hoja yeyote kwa nini hataki serikali tatu na badala yake anataka mbili, ameishia tu kumtukana Tundu Lissu na kumshambulia Maalimu Seif, kama ndivyo hivi, naungana na Mwandishi nguli Privatus Karugendo kwamba hawa wajumbe hawaelewi ni nini wanafanya huko Dodoma.
 
Back
Top Bottom