Mwakyembe amshushua Tundu Lissu...

Mwakyembe amshushua Tundu Lissu...

Kwa waliomsikiliza Mwakyembe jana watakubaliana nami kwamba tuna shida sana kama Taifa.... Sikuamini macho na masikio yangu!! Ni kama vile Mwakyembe alikua ameshikiwa akili na kuwekewa akili za kina Kibajaji.. Kweli VX V8(Kilimo Kwanza zinabadilisha watu):doh:
 
Jana nilimdharau Mwakyembe alivyokuwa anajivuna na kuwaponda wenzake huku akishindwa kupinga hoja za wapinzani wake lakini ''Miafrika ndivyo tulivyo'' Nyani Ngabu

To educate a man in mind and not in morals is to educate a menace to society.
Theodore Roosevelt

Read more at To educate a man in mind and not in morals is to educate a menace to society. - Theodore Roosevelt at BrainyQuote
To educate a man in mind and not in morals is to educate a menace to society. - Theodore Roosevelt.
 
Haki ya nani Mh Mwakyembe ni jabali kalichambua lile lihuni lenye laana za wazazi wake kama karanga,wallah mi cpendi wanasiasa vichaa kama jitundu ni jitu la ovyo lisilofaa kuishi ktk jamii hakika Mwakyembe kalinyongelea mbali

Huna haja ya kupenda watu. Utalawitiwa! shauri yako! Hata ukitumwa jitahidi kuelewa utajibiwa nini!
 
Kwa muda mrefu nimekuwa nikimchukulia Dr Mwakyembe kama mwanasiasa aliye tofauti na wanasiasa wengine wengi ndani ya Chama cha mapinduzi japo utendaji wake kwenye nafasi yake ya uwaziri si ya kuvutia sana.
Kitu kimoja ambacho sikuwahi kukijua kuhusu huyu mheshimiwa ni juu ya tabia yake ya majivuno kutokana na usomi wake.Nilimshangaa sana jana kwa jinsi alivyokuwa anawasilisha hoja yake ya kutetea serikali mbili,Mheshimiwa Mwakyembe alitumia muda mwingi kuwakejeli akina Lissu na Jussa kutokana udogo wa umri wao na viwango vya elimu yao kuliko kujadili hoja zao.Ni dhahiri Dr Mwakyembe alikuwa amefadhaika sana kwa kuumbuliwa juu ya unafiki wake sasa akawa anatafuta namna jinsi ya kujinasua kutoka kwenye aibu ile,Kwa bahati mbaya sana alishindwa kuwahakikishia wenzie ndani ya Bunge kama kilichosemwa na wapinzani juu ya msimamo wake wa kuunga mkono muungano wa serikali tatu kwenye ile THESIS yake wakati ana-persue Ph.D yake nchini Ujerumani kama ni kweli ama la.Kusema kweli hakuna hoja ya maana Dr Mwakyembe aliyoiongea kupangua hoja za akina Lissu zaidi ya mashambulizi binafsi na majivuno.
Tukiachana na hayo ya utetezi wake wa kukana kwamba hakuwahi kuunga mkono muungano wa serikali tatu.Ebu tugeukie kwenye utetezi wa Dr Mwakyembe juu ya muungano wa serikali mbili.Hapa pia aliutumia muda mwingi kujisifia kuhusu usomi wake na kushiriki kuandika vitabu mbalimbali akishirikiana na wasomi wengine kama akina Prof Issa Shivji,Kweli rangi nyeusi inayoishi Afrika haiwezi kuacha asili yake ya ulimbukeni hata siku moja.Kwa namna ninavyofahamu wasomi wengi duniani ambao wamepata fursa wamefanya mambo makubwa sana kwenye jamii zao na ulimwnguni kwa jumla.Mfano Dr Carson,The NEURO SURGEON amefanya mambo makubwa kwenye kuboresha matibabu ya ubongo,Hawa ndiyo watu ambao hata wakijisifia kuwa wamesoma utakubaliana nao kwasababu wanastahili lakini kamwe hutawasikia akina Dr Ben Carson wakijisifia kuwa wao ni wasomi kuliko wengine isipokuwa matendo yao yanaongea mengi na hata kujizolea sifa lukuki ulimwenguni.
Nikirudi kwa wasomi wetu wa Afrika kusema kweli wanakera sana.Wao wanadhani kukusanya vyeti kutoka vyuo mbalimbali na kujifungia library kuandika vitabu wakitumia kazi za watu wengine ndiyo wamemaliza wajibu wao wa kulijenga Bara la Afrika.Leo Mwakyembe anaposimama pale Bungeni na kuanza kukejeli elimu za wenzake na kujisifia kwamba yeye amesoma sana kwakweli inasikitisha sana.Sisi hatukutaka kujua kuhusu elimu yake au kama aliandika vitabu,Tulichotaka kujua ni kama ni kweli aliunga mkono muungano wa serikali tatu kwenye THESIS yake wakati anasomea Ph.D yake nchini Ujerumani?Na jambo jingine tulilotaka kujua ni kwanini anatete muungano wa serikali mbili basi.
Tulichokishuhudia pale Bungeni ni Dr Mwakyembe kujaribu kutaka kupimana msuli na Lissu kwenye tasnia ya sheria,Kiuhalisia Dr Mwakyembe anatishwa na uwezo wa Lissu katika kuzichambua sheria na kwakuwa asili ya huyu mheshimiwa ni kutaka kujiona yuko ya wengine kwahiyo sehemu salama kwake ilikuwa ni kukimbilia kwenye Ph.D yake.Hakuna asiyejua kuwa Tundu Lissu amefanya mambo mengi ya kutukuka kwenye medani ya sheria hata kabla hajawa Mbunge.Lissu anazifahamu sheria za nchi hii practically.Nikija kwa mheshimiwa Mwakyembe sikumbuki aliwahi kufanya nini cha kukumbukwa katika nchi hii zaidi ya kushika chaki darasani.Nje ya taaluma yake ya ualimu hakuwahi kufanya jambo lolote la kujivunia.Kimafanikio kwenye medani ya sheria Lissu amefanya mambo mengi makubwa kuliko huyu mheshimiwa kwasababu Lissu amefanya kazi za uanasheria kwenye mahakama mbalimbali kwahiyo anafahamu vyema anachokipigania,Tofauti na Dr Mwakyembe ambaye anazifahamu sheria za nchi hii kinadharia zaidi.Natamani kumwona Dr Mwakyembe akisimama mahakamani akimtetea mtu au akitetea upandea wa pili halafu akashinda kesi,Mpaka atakapoanza kuyapata mafanikio ya kweli ya kutoa msaada wa kisheria kwa wengine kama afanyavyo Lissu ndipo tutakapoanza kumpa heshima anayotamani apewe.
Amepewa uwaziri wa mawasiliano na uchukuzi na sijaona kipya alichokileta kwenye sekta hiyo pamoja na kusoma kwake sana.Ifike wakati wasomi wa Afrika wabadilike sasa,Badala ya kukaa na kujisifia juu ya usomi wao ingekuwa busara kama wangeutumia usomi wao kuifanya Afrika sehemu bora ya kuishi duniani.Namsifu Tundu Lissu kwa kujaribu kufanya kile wasomi wengi wanashindwa kukifanya katika nchi hii,Nacho ni kusimama na wanyonge na kupambana na mfumo kandamizi unaowanyima fursa Watanzania kutimiza ndoto zao.Kwetu sisi Tundu Lissu ndiye msomi mwenye manufaa kwa nchi hii anayeitendea haki elimu yake na ndiye tunayemuamini na kumsikiliza zaidi kuliko hao wasomi wengine uchwara.

It is a thousand times better to have common sense without education than to have education without common sense.
 
Tindu lisu sheria haijui, anaedit michango ya wengine, anaweka mawazo yake halafu anajifanya kuyanukuu!
 
Huyu jamaa ana misifa kama bongo flavour boys. Huwezi kukana kitu kilichoandikwa. Mwakyembe alijishushua mwenyewe. Ni mtetezi wa serikli 3 lakini kajivisha ubongo wa Mrema. Watz wameelewa vizuri ujinga wa msomi huyu.
 
Mmekalia msumari naona mnalialia tuu.
Jana mmerudi bungeni kuchukua posho

Msumari umekalia ww k.e.n.g.e maji ww..!! Hamjui kujibu hoja za msingi mnatoa mipasho ndani ya BMK. Mumeo huwa hakuelekezi cha kufanya

Sent from my BlackBerry 9320 using JamiiForums
 
Dokta nina mpa heshima ni dokta anayetibu binadam na wanyama lakini hawa madokta wa ccm hawa na thesis zao za kukopi hawana lolote na hawana faida ktk nchi hii.. Kwa ujumla madokta na maprofesa wa Afrika ni wababaishaji, matumbo yako yana njaa wala usije ukawaamini

Sent from my BlackBerry 9320 using JamiiForums
 
Mwakyembe ni mnafiki tu, kuanzia kuhusika kumng'oa Lowassa kisa uwaziri mkuu, kukubali kupewa uwaziri na serikali ileile ya richmond na sasa kukataa vitabu vyake!!! Ni mnafiki tu!!!
 
Mi nasubiri mwenye hicho kitabu cha Mwakyembe atupie humu ndo tuchangie
 
BAVICHA kweli tatizo mtu huna hata shahada ya kwanza unamkosoa dr wa sheria huyo lisu hanalolote. Mwakyembe amefanya mwenyewe huo utafiti Leo hii unamkosoa mtu na utafiti wake ukumbuke kwamba utafiti haunadiliki hata miaka elfu kumi yale majibu yatabaki kama yalivyo. Sasa kama hujui kusoma majibu ya tafiti kaa kimya
 
Mwakyembe na 6 ndiyo wanafki wa kwa nchi yetu hii. Lakini watalaanika tu.
 
Hivi Mwakyembe na elimu yake yote anaweza kumnukuu maalim Seif? Tangu lini mke akamkana mme? Maalim kafunga ndoa na ccm, haiitaji akili kubwa kung'amua hilo, huyu dr vipi?
 
CCM wameligeuza Bunge la Katiba kuwa bunge la kuwasema UKAWA & Co.

Mimi nilidhani huu ndio wakati wao pekee wangeutumia kuonesha weledi wao kwa dhamana waliyoachiwa na hao waliosusa...

Ndio wakati sasa wale magwiji wao wangejenga hoja hai wakionesha wapi tulipokosea na nini kifanyike kututoa hapo...

Ajabu ni kila apewaye nafasi haishi kutumia walau nusu au zaidi ya muda wake kutoa vijembe lukuki pasipo kuweka bayana mambo tuyatazamiayo Watanzania
 
Kama wasomi ma Dr na Prof wameanza kukana machapisho yao Taifa linaelekea kubaya.
 
Mimi nilidhani angeelezea abstract ya kazi yake pale alipokuwa anamjibu mh. Lissu kuwa alitoa conclusion kwa kusoma mstari, badala yake na yeye kaishia katusomea mstari tu kwenye hiyokazi yake na kuanza kumchafua Maalimu Seif ili ajisafishe yeye. Sijui kwanini hawa wasomi wetu wanapenda kutumia taaluma zao kisiasa, badala ya kutoa ufumbuzi wa changamoto mbalimbali tulizonazo kulingana na fani zao walizobobea.
 
TUNDU LISSU haumbuliki WALA HAFEDHEHEKI ! NA MWAKYEMBE AKITAKA KUJIDHALILISHA ZAIDI BASI AENDELEE KUMSHAMBULIA LISSU .

No wewe ndiyo hujui. Kwa sisi tulioiona shule kidogo Lissu ni mbumbu. Huwezi kutoa kashfa kubwa kiasi hicho kwa nukuu alizotumia. Kama ana akili timamu asingeweza kusema ati saini imegushiwa? Lissu ni mnafiki sana!
 
Back
Top Bottom