Mwakyembe amfukuza mfanyakazi aliyestaafu 2013

Jambo leo na masogange

"By W. J. Malecela - Eti source ni Radio One? duh!! ile wanayoitumia UKAWA kila wakati!! ama kweli ukistaajabu ya musa utaona ya firauni

Le Mutuz"

Yaani some times Le mutuz akili zake kama maisha yake,yaani always amekaa kimzahamzaha kupita kiasi
 
Huyo mstaafu alikua anatafuta nini ofisini mpaka leo,Hapa Kamani anaweza kuona anamkomoa Mwakyembe kumbe anaonyesha udhaifu wake.

we nae tumia bas japo ka akili ka darasa la sita
kinacha mwasha Mwakyembe kufukuza kaz wafanyakaz wa wizara nyingne ni nini? Alafu mbaya zaidi anafanya hvo bla kumuhusisha wazir wa wizara husika. Unategemea Kamani afanyeje. Uo ndo unafki wa kutaka aonekane yeye Mwakyembe ni mfanyakaz kumbe unafki mtupu
 
Hii ndio athari za udikteta,unaweza kuhamuru hata marehemu afukuzwe kazi,angefuata cardinal principal of natural justice kuwa -a person should not be condemned unheard,angewapa nafasi ya kuhojiwa ,kujitetea na kisha kutoa maamuzi bila shaka angegundua kuwa kati ya majina aliyopewa wako wastaafu.Ni kweli anatoa maamuzi ya jazba na ya kukurupuka
 
ANAYETAKIWA KUJIBU hayo maswalini kamani ni kwanini mtu astaafu mwakajana na mpaka sasa anasomeka km mtumishi inamaana kwamba wanalipa mishahara hewa kibao
 
Hata Kama Kweli Mwakyembe kakosea ..KULIKUWA na haja gani ya waziri Kamani kuongea HADHARANI bila kuongea wenyewe kwa Siri ....hata Kama kakosea bado Waziri Mwakyembe anabaki na haki ya kuchukua hatua kwa kuwa wafanyakazi husika ...wamekuwa posted uwanja wa ndege na kuna AGIZO la Rais la kusafisha vitendo Vya RUSHWA ,aibu ,Madawa ya kulevya pale uwanjani ..Sasa Kama waziri anataka kuendelea kuwatumia wafanyakazi wake wa wizara ya Kilimo walioko pale ...Njia rahisi angewapangia tu sehemu nyingine mbali na uwanja wa ndege au Bandarini

Kuchukua hatua haraka ni jambo jema mkuu lakini unajisikiaje mtu anavaa majukumu yako tena mbele ya vyombo vya habari anafukuza mtu aliye chini yako na unaona kupitia taarifa ya habari tu eti waziri husika atapewa taarifa!!!!

Angesema nitamjulisha waziri husika ili wahusika wafukuzwe kazi.....haipendezi kumwambia waziri mwenzako kuwa nitakutaarifu rasmi kupitia public media.........Mwakyembe kachemka.......
 
Huko ndiko kunaitwa kukurupuka. Lakini pia sina uhakika taratibu za kazi serikalini zinasemaje kama Waziri anaweza kumfukuza kazi mfanyakazi yeyote wa serkali hata kama hayuko kwenye wizara yake!!!!! Nafikiri kwa kuweka mambo sawa Mwakyembe angetangaza kuwafukuza hao wafanyakazi kutoka kwenye nafasi zao ndani ya airport ili warudi kwenye wizara zao na huko angemshauri waziri mwenzake kuwafukuza kazi. Lakini sio yeye kuwafukuza kazi.

Tiba

Yes...that is my point....Rais au Waziri mkuu ndio anaweza kuchukua maamuzi kama hayo....kesho waziri Mwakyembe atamfuta kazi ofisa wa Polisi alafu aseme kupitia tv kuwa atamtaarifu IGP baadae!!!! Zipo namna za kuchukua hatua lakini si namna hii............
 
Duh! huku sasa kuumbuana.kwa nini waziri kamani asimtafute kwanzan Dr. Mwakyembe ili waweke sawa records zao kabla ya kuruka hewani?

Na kwanini Mwakyembe aruke hewani bila kuwasiliana na Waziri Titus Kamani!
 
Hawa mawaziri wa jk yani ni vichekesho tu
Sasa mtu kama mwakiembe ni mtu wa kukurupuka bila sababu sasa ona kamfukuza mstaafu kazi
Inamaana anafanya vitu bila tafiti za maana aibu!


Je kama ni mstaafu lakini hajatolewa kwenye malipo-mstaafu hewa ,au alifanya matukio kabla ya kustaafu?
 
Nguruvi3 lile Baraza lako la mawaziri, tena! Waziri mmoja anamshangaa waziri mwenziwe kupitia vyombo vya habari! Teamwork!
Sugu alisema baraza la mawaiziri ni wapumbavu watu wakambeza. Sasa onayanayotokea kutoka baraza moja
 
Last edited by a moderator:
Kwa nini wasinge wasiliana kwanza kabla ya kila mmoja kukimbilia vyombo vya habari?
 
Huyo Waziri asubiri Video yake itakaporushwa hewani maana Mwakyembe ameona video na sura zake!!!
 
Aliyetangazwa fukuzwa wakati ni Mstaafu amfungulie Mwakyembe kesi ya kumzalilisha..... this country bwana!
 
Sarakasi zinaendelea,,, haya huwezekana tanzania tu,,, haya watalii mje kuangalia ajabu lingine hili....
 
waziri titus kamani amesema mmoja wa watu waliotangazwa na mwakyembe juwa wamefukuzwa aiport jana alishastaafu tangu 2013 na sio mfanyakazi wa serikali tangu wakati huo.

Waziri kamani amesema ameshangazwa kuona mstaafu anatangazwa kuwa alikuwa mfanyakazi wa wizara yake kama alivyotangaza mwakyembe jana.

Hata hivyo waziri kamani amesema anasubiri taarifa zaidi toka kwa dr mwakyembe kuhusu hatua alizotangaza jana kufukuza wafanyakazi wa wizara yake waliokuwa wakifanya kazi jknia.

Source:radio one habari



ikiona hivyo ku,,aa.....zao ujue huyo mtu yuko kwenye payroll toka aondoke


aende kuchunguza again afukuze dir wa taa na manager wake wanaosaini uchafu /....


Akuna tofauti na kumlipa marehemu .........
 
ukichunguza hiyo wizara ina asili ya ukabila

alikuja yule mh wa wa TANGA AKAMWEKA ATCL NDUGU YAKE WA TANGA

AMEFUKUZWA TU GAFLA KAJA HUYU MNYAKYUSA KAMWEKA MWENZAKE MNYAKYUSA AIKUCHUKUA HATA SIKU 15

SO UJUE KUNA KITU WANAPATA SI WAJINGA ATI
 
Ni dhahiri kabisa kuchomekwa kwa jina la mstaafu ni njama za mafisadi kutaka kudhohofisha jitihada za Mwakyembe. Hupaswi kulalamika wakati mwenzako anajaribu kufanya kitu kusaidia hali mbaya iliyotawala kwenye ule uwanja. Unapaswa kulaani watu wanaotaka kumuhujumu!
Mkuu hii inaonyesha jinsi ambavyo si makini na anafanya kazi k8majungu majungu tu
 
Ukisema hajafanya lolote unakosea, je wajua mapato ya tra bandarini baada ya mwakyembe kuichukua bandari yamepanda kwa kiasi gani? Usiendeshwe na hisia zaidi kuliko uhalisia. Isiwe tu ilimradi mtu atukanwe na kuchafuliwa, hajafikia kufanya vizur sana ila ktk wizara yake anajitahidi na kila mtu analiona. Akifanya vema tumpe pongez na akikosea pia sio tu kila kitu kiwe negative tu. Ina maaana hamuoni rushwa ilivyoshamir uwanja wa ndege? Sasa jamaa anathubutu nyie mnamponda? Sijui mna maana gani?
Mkuu
Mapato ya TRA kuongezeka ni Obviously factor, kwakuwa na mizingo imeongezika. Idadi ikiongezeka ya mizigo na mapato yataongezeka.

Ama mapato uameongezeka kwa mizigo ile ile?

Zamani TRA walikuwa wanakusana billion30 kwa mwez kipind cha mkapa, sasa ni Ni zaidi coz wawekezaji na wafanyabiashara wameongezeka so hiyo ni Obvious. Hakuna jipya
 
Back
Top Bottom