nngu007
JF-Expert Member
- Aug 2, 2010
- 15,862
- 5,797
Tuesday, May 10, 2011
MRATIBU wa Maboresho katika Ofisi ya Rais, Ikulu, Singi Madaka, ameieleza Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, kuwa Mkurugenzi wa Kampuni ya Kufua Umeme ya Richmond, Naeem Gire, alihudhuria kama mjumbe kikao cha majadiliano ya rasimu ya mkataba na timu ya wataalam iliyoundwa na Serikali. Madaka aliiambia mahakama hiyo kuwa, katika kikao hicho, Gire alitambulishwa na Mohamed Gire ambaye naye alijitambulisha kama Mwakilishi na Msemaji Mkuu wa kampuni hiyo kwa Kanda ya Afrika Mashariki na Kati.
Madaka ni shahidi wa nne katika kesi ya kughushi na kutoa taarifa na hati za uongo inayomkabili Mkurugenzi wa Kampuni ya Richmond Tanzania, Naeem Gire. Katika ushahidi wake, Madaka alidai kuwa, Aprili mwaka 2006 akiwa Kamishina Msaidizi, Sera za Madeni katika Wizara ya Fedha kabla hajahamia Ikulu mwaka 2007, aliitwa na Katibu Mkuu wa wakati huo, Gray Mgonja na kumuagiza kwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini wa wakati huo, Arthur Mwakapugi ili akamuelekeze kazi ya kufanya.
Alidai kuwa, alipokwenda aliwakuta maofisa wengine kutoka Wizara ya Nishati na Madini, Benki Kuu ya Tanzania (BoT) na wengine kutoka Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali. "Tukiwa hapo, Mwakapugi alitueleza kuwa nchi iko kwenye dharura kuu ya umeme na kwamba tunaweza kuingia gizani wakati wowote hivyo zinafanyika juhudi za kutatua tatizo hilo kupitia zabuni ya kupata wakodishaji wa kufua umeme wa dharura iliyokuwa imeitishwa na Tanesco.
"Kwa mujibu wa zabuni ile, Tanesco walikuwa wametoa taarifa kwamba, wazabuni wote walikuwa hawafai, hivyo Serikali ilikuwa inatafuta njia nyingine ya dharura kupata ufumbuzi wa tatizo hilo ambapo Wizara ya Nishati na Madini iliamua kuitisha makampuni yale yale nane yaliyoomba zabuni awali ili yatoe ufafanuzi wa kitaalam kuhusu uwezo wao wa kutatua tatizo hilo," alidai Madanka.
Aliendelea kudai kuwa, baada ya hapo iliundwa timu ya wataalam yeye akiwa Mwenyekiti na kazi ya timu hiyo ilikuwa ni kupokea majina ya makampuni manane na kuwasilisha majumuisho Wizara ya Nishati na Madini. Alidai kuwa kwa msingi wa maelekezo hayo Aprili 22-24, mwaka 2006 timu hiyo iliagizwa kukutana na kampuni hizo nane katika hoteli ya Protea kwenye chumba cha kufanyia kazi ambapo kampuni saba tu ndizo ziliwasilisha maelezo yao isipokuwa Kampuni ya Gapco.
Wakati akiendelea kutoa ushahidi wake Wakili wa Serikali, Shadrack Kimaro, aliiomba Mahakama ipokee nakala ya ripoti hiyo kama sehemu ya kielelezo cha ushahidi katika kesi hiyo lakini Wakili wa utetezi Alex Mgongolwa alipinga kupokelewa kwa nakala hiyo kwa madai kuwa haikua nakala halisi hivyo haifai kupokelewa kwa mujibu wa sheria. Akiendelea na ushahidi wake Singi alidai kuwa baada ya ripoti hiyo ya wataalam kukabidhiwa Wizara ya Nishati na Madini, Juni mwaka, 2006 aliitwa tena na Mgonja na kutakiwa aende kwa Mwakapugi ili akaendelee na kazi waliyokuwa wameianza. Akiwa kwa Mwakapugi alikutana na maofisa wengine na kuwaeleza wajadili kwa kina juu ya mapendekezo ya Kampuni ya Richmond kuhusu kutatua tatizo la umeme.
Baada ya hapo, shahidi huyo alidai, kuwa Juni 5, mwaka 2006 walikutana na wawakilishi wa Richmond katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa Dar es Salaam (DICC) kwa ajili ya majadiliano ya rasimu ya mkataba, ambapo waliohudhuria walikuwa Julius Sarote kutoka Wizara ya Nishati na Madini, Mohamed Gire na Mwanasheria wao, Curtbet Tenga na Naeem Gire. Alidai kuwa rasimu ya mkataba iliainisha vipengele vyote kuhusu masuala ya fedha, kiufundi, jinsi ya kuendesha mradi na muda wa kukamilisha mradi wenyewe na kwamba katika kusaini mkataba, Kampuni ya Richmond iliwakilishwa na Mohamed Gire na Serikali alisaini yeye (Madaka).
Shauri hilo litaendelea leo.
Mwakapugi atajwa Kesi ya Richmond
MRATIBU wa Maboresho katika Ofisi ya Rais, Ikulu, Singi Madaka, ameieleza Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, kuwa Mkurugenzi wa Kampuni ya Kufua Umeme ya Richmond, Naeem Gire, alihudhuria kama mjumbe kikao cha majadiliano ya rasimu ya mkataba na timu ya wataalam iliyoundwa na Serikali. Madaka aliiambia mahakama hiyo kuwa, katika kikao hicho, Gire alitambulishwa na Mohamed Gire ambaye naye alijitambulisha kama Mwakilishi na Msemaji Mkuu wa kampuni hiyo kwa Kanda ya Afrika Mashariki na Kati.
Madaka ni shahidi wa nne katika kesi ya kughushi na kutoa taarifa na hati za uongo inayomkabili Mkurugenzi wa Kampuni ya Richmond Tanzania, Naeem Gire. Katika ushahidi wake, Madaka alidai kuwa, Aprili mwaka 2006 akiwa Kamishina Msaidizi, Sera za Madeni katika Wizara ya Fedha kabla hajahamia Ikulu mwaka 2007, aliitwa na Katibu Mkuu wa wakati huo, Gray Mgonja na kumuagiza kwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini wa wakati huo, Arthur Mwakapugi ili akamuelekeze kazi ya kufanya.
Alidai kuwa, alipokwenda aliwakuta maofisa wengine kutoka Wizara ya Nishati na Madini, Benki Kuu ya Tanzania (BoT) na wengine kutoka Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali. "Tukiwa hapo, Mwakapugi alitueleza kuwa nchi iko kwenye dharura kuu ya umeme na kwamba tunaweza kuingia gizani wakati wowote hivyo zinafanyika juhudi za kutatua tatizo hilo kupitia zabuni ya kupata wakodishaji wa kufua umeme wa dharura iliyokuwa imeitishwa na Tanesco.
"Kwa mujibu wa zabuni ile, Tanesco walikuwa wametoa taarifa kwamba, wazabuni wote walikuwa hawafai, hivyo Serikali ilikuwa inatafuta njia nyingine ya dharura kupata ufumbuzi wa tatizo hilo ambapo Wizara ya Nishati na Madini iliamua kuitisha makampuni yale yale nane yaliyoomba zabuni awali ili yatoe ufafanuzi wa kitaalam kuhusu uwezo wao wa kutatua tatizo hilo," alidai Madanka.
Aliendelea kudai kuwa, baada ya hapo iliundwa timu ya wataalam yeye akiwa Mwenyekiti na kazi ya timu hiyo ilikuwa ni kupokea majina ya makampuni manane na kuwasilisha majumuisho Wizara ya Nishati na Madini. Alidai kuwa kwa msingi wa maelekezo hayo Aprili 22-24, mwaka 2006 timu hiyo iliagizwa kukutana na kampuni hizo nane katika hoteli ya Protea kwenye chumba cha kufanyia kazi ambapo kampuni saba tu ndizo ziliwasilisha maelezo yao isipokuwa Kampuni ya Gapco.
Wakati akiendelea kutoa ushahidi wake Wakili wa Serikali, Shadrack Kimaro, aliiomba Mahakama ipokee nakala ya ripoti hiyo kama sehemu ya kielelezo cha ushahidi katika kesi hiyo lakini Wakili wa utetezi Alex Mgongolwa alipinga kupokelewa kwa nakala hiyo kwa madai kuwa haikua nakala halisi hivyo haifai kupokelewa kwa mujibu wa sheria. Akiendelea na ushahidi wake Singi alidai kuwa baada ya ripoti hiyo ya wataalam kukabidhiwa Wizara ya Nishati na Madini, Juni mwaka, 2006 aliitwa tena na Mgonja na kutakiwa aende kwa Mwakapugi ili akaendelee na kazi waliyokuwa wameianza. Akiwa kwa Mwakapugi alikutana na maofisa wengine na kuwaeleza wajadili kwa kina juu ya mapendekezo ya Kampuni ya Richmond kuhusu kutatua tatizo la umeme.
Baada ya hapo, shahidi huyo alidai, kuwa Juni 5, mwaka 2006 walikutana na wawakilishi wa Richmond katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa Dar es Salaam (DICC) kwa ajili ya majadiliano ya rasimu ya mkataba, ambapo waliohudhuria walikuwa Julius Sarote kutoka Wizara ya Nishati na Madini, Mohamed Gire na Mwanasheria wao, Curtbet Tenga na Naeem Gire. Alidai kuwa rasimu ya mkataba iliainisha vipengele vyote kuhusu masuala ya fedha, kiufundi, jinsi ya kuendesha mradi na muda wa kukamilisha mradi wenyewe na kwamba katika kusaini mkataba, Kampuni ya Richmond iliwakilishwa na Mohamed Gire na Serikali alisaini yeye (Madaka).
Shauri hilo litaendelea leo.
Mwakapugi atajwa Kesi ya Richmond