Mwaka ndio unaisha, tuongee kikubwa

Mwaka ndio unaisha, tuongee kikubwa

mutant gene

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2014
Posts
876
Reaction score
326
Eti mimi si ndio kaka yenu bana, kwahiyo ni lazima niwaulize.

Kama wewe ni mdada, mwaka ndio huo unaisha una mipango gani juu ya kuolewa? maana siku zinavyozidi kwenda na umri unazidi kusogea? (wale wanachuo au wanafunzi haiwahusu nyie someni kwanza mmalize)

Kama wewe ni kaka una mipango gani ya kuoa maana na wewe umri wa kuoa umeshafika una kila kitu. umejiajiri, kuajiriwa, kipato kizuri, mshahara mzuri, biashara zako zinaendelea vizuri kwa ufupi maisha ni mazuri.

sasa unasubiri nini? au unataka mpaka upigiwe kengele?( hapa wale wenye kukaa home au chumba kimoja na sitting room haiwahusu ninyi jipangeni kwanza)

eenhe!! sasa niambieni kaka yenu mmipango yenu juu ya hilo jambo. NAWASIKILIZA!!!
 
Ati "NAWASIKILIZA" unaushahidi? Any way mimi tayari em ngoja tuone maoni ya makapera sugu humu.
 
Let's face it. CCM wenyewe hawawezi kuongoza. Kwa kifupi ni hakuna anayeweza kuiongoza Tanzania kwa sasa. Kama yupo mtajeni tumchambue hapa. Hili linchi linajiendesha lenyewe tu.

ya kweli hayo masai dada na yule jamaa yako anasemaje? hana mpango?
 
Last edited by a moderator:
Eti mimi si ndio kaka yenu bana, kwahiyo ni lazima niwaulize.

Kama wewe ni mdada, mwaka ndio huo unaisha una mipango gani juu ya kuolewa? maana siku zinavyozidi kwenda na umri unazidi kusogea? (wale wanachuo au wanafunzi haiwahusu nyie someni kwanza mmalize)

Kama wewe ni kaka una mipango gani ya kuoa maana na wewe umri wa kuoa umeshafika una kila kitu. umejiajiri, kuajiriwa, kipato kizuri, mshahara mzuri, biashara zako zinaendelea vizuri kwa ufupi maisha ni mazuri. sasa unasubiri nini? au unataka mpaka upigiwe kengele?( hapa wale wenye kukaa home au chumba kimoja na sitting room haiwahusu ninyi jipangeni kwanza)

eenhe!! sasa niambieni kaka yenu mmipango yenu juu ya hilo jambo. NAWASIKILIZA!!!

kaka mkubwa mbona unazeeka vibaya?yaani unazeeka huku unapoteza kumbukumbu?umeshasahau kwamba nimeshaoa?
 
Umri wa kuoa na kuolewa ndio umri upi huo?
 
Mkuu acha dharau...chumba kimoja na sitting rum unaona kidogo...??? U must have problems
 
Umri wa kuoa na kuolewa ndio umri upi huo?

Umri wa kuowa ni upi na umri wa kuolewa ni upi? Na je kuowa au kuolewa ni lazima?

Nitarudi.

naweza nikasema hakuna umri maalum wa kuoa. ila kwa binti itakuwa vizuri pale atakapo maliza masomo yake. na kwa mwanaume vilevile atakapo maliza masomo yake na akishajijenga vya kutosha basi ni vizuri kuoa. kitu kingine ni pindi kijana wa kike au wa kuime akionesha kujitambua kikamilifu kiakili.
 
Back
Top Bottom