Mshana Jr
Platinum Member
- Aug 19, 2012
- 269,634
- 697,845
Miaka 5 ya awamu ya tano inafikia tamati na pigo toka kwa nchi mwanachama kuweka katazo la bidhaa za jirani na mwanajumuiya zisiingizwe nchini mwake...Rwanda imepiga marufuku bidhaa za Tanzania zisiingie tena nchini mwake na sasa anataka na kufunga mpaka wa Rusumo
Migongano ipo popote na hata kwenye jumuiya kubwa kama hii haiwezi kukosekana.. Migongano na migogoro ipo mahali popote hata ndani ya familia...tatizo sio migogoro...!!! Tatizo ni namna ya kutatua tatizo linapotokea ama kuviwahi viashiria vya tatizo kabla halijamea
Hapa tutoke kidogo nje ya mipaka yetu ..tujadili siasa za kikanda, mahusiano na majirani na ushirikiano ndani ya jumuiya kubwa ya Africa mashariki...kwa hii miaka mitano jumuiya imekumbwa na migongano ya hapa na pale
Uganda na Kenya kuhusiana na mradi mkubwa wa bomba la mafuta...Uganda waliwachomolea Kenya dakika za mwisho na kupewa Tanzania...hii ilimuuma sana Kenya ambaye naye sasa anamcheka Mganda baada ya mradi husika kufunikwa na sintofahamu kubwa...!!!
Uganda na Rwanda.... Ishu ya wakimbizi na kufadhili ama kuhifadhi vikundi vya wapiganaji wenye nia ya kupindua serikali za mataifa husika
Kenya na Tanzania kuanzia kuchomeana bidhaa hai, kutaifisha mifugo ama kupiga faini kubwa mpaka kufikia kuwekeana makatazo ya kibiashara kwenye usafiri wa anga kisingizio kikiwa covid-19
Burudi na Rwanda ishu ya makundi yanayopinga serikali zao..tuhuma za kuhifadhi na kufadhili makundi husika
Lililo jipya ni hili la Tanzania na Rwanda kuhusu bidhaa na inavyoelekea mambo yanakwenda kwa haraka mno....lakini ninini kimetokea kati ya haya mataifa mawili? Jirani halafu wanajumuiya moja?
Mwanzoni mwa awamu ya tano mahusiano yetu yalikuwa ni mazuri sana mpaka redio mbao zikawa zinasema yake
Ya kwamba
Ushauri wa kununua ndege tena kwa cash tuliupata Rwanda
Ya kwamba
Ukuta wa Mererani lilikuwa ni wazo la Rwanda na eneo lote likawa linalindwa na wanajeshi wa Rwanda
Ya kwamba
Rais alikuwa na ulinzi maalum toka Rwanda
Ya kwamba
ushawishi wa Rwanda na ukaribu wa viongozi wakuu ndio uliochochea reli kujengwa kwenda Rwanda nchi ya watu wasiozidi milion kumi na kuacha kuipeleka Kongo nchi yenye watu zaidi ya milion mia
Ya kwamba
Mradi wa ujenzi wa bandari kavu eneo la Ruvu mizani na miundo mbinu ya moja kwa moja mpaka airport na bandarini ni ushawishi wa Rwanda kwa ajili ya mizigo yake
Sasa kama yote haya ni kweli ....ninini kimetokea all of a sudden!? Kuna wambea wanasema chinichini ni uhuni aliofanya rais wa Rwanda kwenye madini...kwamba alipiga mzigo wa kutosha na kusepa nao kihuni....zile za kimjinimjini.
Pamoja na kwamba sababu kubwa ni covid-19 ...kwakuwa kama jumuiya hawakuwa na sauti moja kwenye kukabiliana na hilo gonjwa na kila mtu akatenda kivyake
Mwanzoni wananchi wa nchi jumuiya walitishwa kuwa viongozi wao wana andaa kitu kinachoitwa BAHIMA EMPIRE na wanahakikisha hiyo ndoto inafanikiwa..hicho ni kipindi ambacho viongozi walikuwa wanatembeleana na kufanya mijadala pamoja
Viongozi walikuwa wanaalikana kwenye matendo ya furaha na huzuni pia.
Kwasasaa jumuiya ni kama imekuwa mfu...likitokea jambo lenye manufaa hasa kiuchumi wanaanza choyo na ubinafsi na kufanyiana hila
Zikitokea changamoto za usalama na mambo ya kisiasa wanaaza kunyoosheana vidole na kutuhumiana wenyewe kwa wenyewe.
Kule kutembeleana na kupeana zawadi kumekoma...covid inaweza kuwa kisingizio lakini nyuma ya pazia kuna picha kubwa zaidi isiyotolewa hadharani na pengine hii ndio inayofitinisha ile ndoto kubwa na ya muda mrefu ya kuwa na BAHIMA EMPIRE.!!
Lakini katika wote hawa MFITINI mkubwa ni nani!? Muda utasema..!!
Migongano ipo popote na hata kwenye jumuiya kubwa kama hii haiwezi kukosekana.. Migongano na migogoro ipo mahali popote hata ndani ya familia...tatizo sio migogoro...!!! Tatizo ni namna ya kutatua tatizo linapotokea ama kuviwahi viashiria vya tatizo kabla halijamea
Hapa tutoke kidogo nje ya mipaka yetu ..tujadili siasa za kikanda, mahusiano na majirani na ushirikiano ndani ya jumuiya kubwa ya Africa mashariki...kwa hii miaka mitano jumuiya imekumbwa na migongano ya hapa na pale
Uganda na Kenya kuhusiana na mradi mkubwa wa bomba la mafuta...Uganda waliwachomolea Kenya dakika za mwisho na kupewa Tanzania...hii ilimuuma sana Kenya ambaye naye sasa anamcheka Mganda baada ya mradi husika kufunikwa na sintofahamu kubwa...!!!
Uganda na Rwanda.... Ishu ya wakimbizi na kufadhili ama kuhifadhi vikundi vya wapiganaji wenye nia ya kupindua serikali za mataifa husika
Kenya na Tanzania kuanzia kuchomeana bidhaa hai, kutaifisha mifugo ama kupiga faini kubwa mpaka kufikia kuwekeana makatazo ya kibiashara kwenye usafiri wa anga kisingizio kikiwa covid-19
Burudi na Rwanda ishu ya makundi yanayopinga serikali zao..tuhuma za kuhifadhi na kufadhili makundi husika
Lililo jipya ni hili la Tanzania na Rwanda kuhusu bidhaa na inavyoelekea mambo yanakwenda kwa haraka mno....lakini ninini kimetokea kati ya haya mataifa mawili? Jirani halafu wanajumuiya moja?
Mwanzoni mwa awamu ya tano mahusiano yetu yalikuwa ni mazuri sana mpaka redio mbao zikawa zinasema yake
Ya kwamba
Ushauri wa kununua ndege tena kwa cash tuliupata Rwanda
Ya kwamba
Ukuta wa Mererani lilikuwa ni wazo la Rwanda na eneo lote likawa linalindwa na wanajeshi wa Rwanda
Ya kwamba
Rais alikuwa na ulinzi maalum toka Rwanda
Ya kwamba
ushawishi wa Rwanda na ukaribu wa viongozi wakuu ndio uliochochea reli kujengwa kwenda Rwanda nchi ya watu wasiozidi milion kumi na kuacha kuipeleka Kongo nchi yenye watu zaidi ya milion mia
Ya kwamba
Mradi wa ujenzi wa bandari kavu eneo la Ruvu mizani na miundo mbinu ya moja kwa moja mpaka airport na bandarini ni ushawishi wa Rwanda kwa ajili ya mizigo yake
Sasa kama yote haya ni kweli ....ninini kimetokea all of a sudden!? Kuna wambea wanasema chinichini ni uhuni aliofanya rais wa Rwanda kwenye madini...kwamba alipiga mzigo wa kutosha na kusepa nao kihuni....zile za kimjinimjini.
Pamoja na kwamba sababu kubwa ni covid-19 ...kwakuwa kama jumuiya hawakuwa na sauti moja kwenye kukabiliana na hilo gonjwa na kila mtu akatenda kivyake
Mwanzoni wananchi wa nchi jumuiya walitishwa kuwa viongozi wao wana andaa kitu kinachoitwa BAHIMA EMPIRE na wanahakikisha hiyo ndoto inafanikiwa..hicho ni kipindi ambacho viongozi walikuwa wanatembeleana na kufanya mijadala pamoja
Viongozi walikuwa wanaalikana kwenye matendo ya furaha na huzuni pia.
Kwasasaa jumuiya ni kama imekuwa mfu...likitokea jambo lenye manufaa hasa kiuchumi wanaanza choyo na ubinafsi na kufanyiana hila
Zikitokea changamoto za usalama na mambo ya kisiasa wanaaza kunyoosheana vidole na kutuhumiana wenyewe kwa wenyewe.
Kule kutembeleana na kupeana zawadi kumekoma...covid inaweza kuwa kisingizio lakini nyuma ya pazia kuna picha kubwa zaidi isiyotolewa hadharani na pengine hii ndio inayofitinisha ile ndoto kubwa na ya muda mrefu ya kuwa na BAHIMA EMPIRE.!!
Lakini katika wote hawa MFITINI mkubwa ni nani!? Muda utasema..!!