Mvi ni dalili ya uzee au ni kitu gani...?

Mtambuzi

Platinum Member
Oct 29, 2008
8,810
15,398
African_couple.JPG

Kama mvi ni kipimo cha busara.......... Kwa nini zifichwe?

Kwa zamani ingekuwa ni muhali mkubwa mtu kuuliza swali la aina hii, kwa sababu mvi zinahesabiwa kama dalili ya busara, bila shaka zikihusianishwa na kuona mengi ambayo ni wenye umri mkubwa tu waliokuwa na nafasi hiyo. Lakini leo, mvi ni kisirani na karibu kila mtu anajaribu kuzikimbia, kwani kuendalea kuwa kijana ni sifa kubwa. Kwa sasa uzee unanuka na kila mmoja anajaribu kuukimbia kwa njia mbalimbali ikiwemo ya kukana umri na kujirudisha nyuma kimatendo. Kwa kifupi hii ndiyo historia ya mvi, usiziogope bure!

Karibu rangi zote asilia za nywele zinatoka kwenye kitu kiitwacho melanin, ambacho huzalishwa na mwili kutokana na seli zinazofahamika kama melenocytes. Nywele zinapobadilika na kuwa nyeupe ina maana kwamba, melenocytes haizalishi tena melanin. Mabadiliko haya ya nywele kutoka rangi nyeusi na kukosa rangi (mvi) siyo hatua ya siku moja bali mwaka na miaka, kwani nywele moja hubadilika baada ya muda mrefu na nyingine na nyingine. Siyo hatua ya siku moja tu. Kwa kadiri mtu anavyozeeka ndivyo ambavyo uwezo wa mwili kuzalisha melanin unavyopungua.

Uwezo huu huanza kupungua mtu anapofikia umri wa miaka 35 au 40. Lakini watu wengine huanza kuota mvi wakiwa na umri wa miaka hata 20 tu. Je, hii nayo inatokana na nini?
Pengine ni jambo la ajabu kwamba kuvuta sigara kunatajwa kama sababu ya kuchochea mtu kupata mvi akiwa na umri mdogo. Ukiwachunguza wavuta sigara wazuri, utagundua kwamba wameanza kuota mvi mapema kuliko umri wa miaka 35 au 40. Matatizo kwenye kiungo kinachodhibiti ukuaji mwilini, yaani thyroid huweza pia kusababisha mtu kupata mvi kabla ya kufikisha umri wa miaka 35. Pia ukosefu wa vitamin B12 unatajwa kwa sababu nyingine.Kuna watu ambao hata kama wana umri wa miaka 60 bado hawataki kuona nywele nyeupe vichwani mwao .

Watu hawa huangaika huku na kule kutafuta dawa kuondoa mvi na pengine kutumia rangi ya nywele ili kufanya rangi ya nywele nyeupe zisionekane. Huu ni kama mwendawazimu kwa kiasi fulani. Kwanini? Kwanza kuna ukweli kwamba nyingi kati ya hizo zinazodaiwa kuwa rangi za kuondoa mvi, zina athari katika mwili wa mtumiaji. Lakini wendewazimu mkubwa zaidi ni kitendo chao cha kukataa ukweli ambao inabidi wajivunie.
Mvi bado ni dalili ya busara. Kama umefikia umri wa kuota mvi na hujafanya jambo lolote la maana na hujatoa mchango wowote wa maana kwa familia yako au jamii unamoishi ni lazima utaficha mvi zako. Kwanini? Kwa sababu utaona haya sana kuonekana kwamba umri wako ni mkubwa lakini hujafanya lolote.

Ninaposema mchango wa maana sina maana ya fedha au mali, bali zaidi nina maana ya mawazo ya kujenga na pengine kuandaa misingi ya kujenga kwa nia ya kuleta maendeleo baadaye.
Hebu chunguza kwa makini, utagundua kwamba watu wote wanaojaribu kuficha mvi ni wale watu ambao wametawaliwa sana na vionjo na tamaa ya miili yao kuliko maendeleo ya binadamu. Ni wale watu ambao hata kama wana fedha, hawajajua hasa wako hapa duniani kwa sababu gani. Hivi ndivyo ilivyo kwa sababu watu wa aina hii huhofia sana umri, huhofia sana kufa kwa sababu hawajakamilisha walichokuja kukifanya duniani kwasababu hawajajua bado.
 
ni kweli ndugu Mtambuzi...binafsi nilikuwa na rafiki O-level ambaye alikuwa na mvi kichwan lakin alikuwa na matendo yenye busara ingawa sijui ni kwa nini akawa na ilhali ni under 20 inawezekana ni urithi.
 
ni kweli ndugu Mtambuzi...binafsi nilikuwa na rafiki O-level ambaye alikuwa na mvi kichwan lakin alikuwa na matendo yenye busara ingawa sijui ni kwa nini akawa na mvi ilhali ni under 20 inawezekana ni urithi.
 
​basi mimi ni mjinga namba moja kwa sababu umri nilionao na mvi zilizokuwepo kichani na kwenye ndevu ni balaa
Sa hata mimi ni kama wewe, ni wachache wenye akili we watazame wengi wao wanazipaka rangi ndevu/nywele zao kua nyeusi huoni kama wajinga.
 
sasa ile hali ya kupaka dawa au piko ili ziwe nyeusi hapo ndio ujinga unapoanzia.kwa sababu mtu akikuangalia usoni anajua tu hili zee.na kama bado yanki anajua juu huyu bado dogo
 
sasa ile hali ya kupaka dawa au piko ili ziwe nyeusi hapo ndio ujinga unapoanzia.kwa sababu mtu akikuangalia usoni anajua tu hili zee.na kama bado yanki anajua juu huyu bado dogo
Kwa hio tunakubaliana wengi wao ni wajinga.
 
Exceptions zipo, lakini mvi ni dalili ya uzee. wanaokuwa na mvi at 20s or 30s, ni matatizo ya genes. Wanaopaka rangi nyewele ili ziwe nyeusi na hivyo waonekane bado vijana -hii ni psychological problem-wanajua umri wao, lakini hawataki kukubaliana na hali halisi. Mimi nilikuwa mmoja wao na pamoja na ku-dye nywele zangu mara kwa mara bado niliendelea kuamkiwa na watoto na vijana: "babu shikamoo". Mwishowe ilibidi niache.
 
Basi mie nina upungufu wa vitamini B12 cause nina mvi mbili tatu na umri wangu bado kabisa..
 
aisee mimi ni mvivu sana wa kusoma, nitarudi baada kumalizia nilipofika!
 
tabasamu ni ishara ya furaha,
Chozi ni ishara ya kilio,
Jasho ni ishara ya kuchoka,
Mvi ni ishara ya ..... : (a) uzee (b) inheritance (c) kuishi miaka mingi (d) U-Lowasa
 
Back
Top Bottom