Muumini auawa na mchungaji

Muumini auawa na mchungaji

Status
Not open for further replies.
Hapa mwenye kutakiwa kuwa na imani ya kutosha ni nani? Hebu ndugu zanguni wenye uelewa wa kutosha njooni mtupe Darasa. Nitafurahi sana kama hii mada itachangiwa sana na watu wenye kuujua ulimwengu wa roho.

Wengi wa Elimu ya kawaida watampiga vita huyu mchungaji, Lakini ningependa kusikia wenzetu wanaoujua ulimwengu wa roho wanasemaje?
Una akili timamu wewe...???
 
Huu mjadala sio wa kuendelea kuuhoji ni wa kipumbavu kabisa, wewe kama mchungaji iweje unamtestia spika alaf unalikalia,si umpige bunduki ieleweke na sio kumtesa kihivyo kama sio upumbavu ni nini?..na huyo aliyeambiwa alale zilikua sijui hazimtoshi ama ni imani imemuingia kisawasawa mpaka akaitikia wito huo, sasa matokeo yake ndio hayo, muumini kapotezwa, mchungaji anakula bata.
 
Innallillah!! Mbona mambo yanazidi kua mambo jamani hivi hawa walokole watakuja kuelimika lini yaa rabi toba!

Nimepatwa na uchungu sana kwa huyo mwanamke maskini anakufa huku anajiona pengine aliogopa kutoa ishara yoyote kua anaumia.... watoto hawana mama, mume amekosa mke, wazazi wamekosa mwana,
Eeeh Mola tuokoe kwa watu madhalimu.
 
Hapa mwenye kutakiwa kuwa na imani ya kutosha ni nani? Hebu ndugu zanguni wenye uelewa wa kutosha njooni mtupe Darasa. Nitafurahi sana kama hii mada itachangiwa sana na watu wenye kuujua ulimwengu wa roho.

Wengi wa Elimu ya kawaida watampiga vita huyu mchungaji, Lakini ningependa kusikia wenzetu wanaoujua ulimwengu wa roho wanasemaje?
Mungu hajaribiwi Wala hadhihakiwi we unafanya demo juu ya uwezo wa Mungu ili iweje.kama umeishiwa mbinu za kuhubiri tafuta kazi nyingine.
 
Mazingaombwe yamekataa inawezekana kuna jamaa atakuwa kageuza shati au tshirt ndani ya kanisa,ona sasa kashaua mwenzake,ukongaaa ya kisouth hiyooo inamuita,,pole mchungaji,,vitu vingne sio vya kujaribu,,ukijikuta fundi kuna wenzako mafundi zaidi
 
Hii dini ya ajabu sana hata ukiangalia watu wake usoni utaona kuna kitu wamenyimwa hovyo sana,sijui tatizo ni nguruwe au vipi
WEWE SASA UMEKOSA ADABU, IMANI ISIYO YAKO YAKUUMIZA WAPI!
JAMBO LA MSINGI HAPO NI MAARIFA YA MHUBIRI NA ANAOWAHUBIRI-MIMI HUJANIJARIBU KIASI HICHO.
 
HOSEA 4 :6 'Watu wangu wanaangamia kwa kukosa maarifa........'

Miujiza ya kweli (inayofanyika kwa Kutumia Jina la Yesu Kristo), ina malengo ya kumtukuza Mungu na kuondoa matatizo mbalimbali yanayowakabili wanadamu- kama vile magonjwa.

Lakini Miujiza feki inamtukuza shetani na inakuwa kama maonyesho au Mazingaombwe. Tujifunze kusoma Biblia, ili tusidanganywe na manabii feki, ambao wanamtumkia Ibilisi.
 
Una akili timamu wewe...???
Nahisi wewe ndio hauna akili timamu kwasababu hujanielewa nina imani wenye akili Timamu wamenielewa.
Naomab nielewe hivi.

1. Mchango wangu umekaa kiswali, (mwenye kutakiwa kuwa na imani ni nani?) kwasababu kwenye mada tulishaambiwa mchungaji kasema muumini alikua na imani haba, ningekua namuunga mkono singeuliza swali.

2. Nimeomba wale wanaoujua ulimwengu wa kiroho waje watusaidie na sisi tupate kuelewa kwasababu kinachofanywa na huyo mchungaji ni zaidi ya kuona na kusoma unayoyasoma

3. Sina muda wa kupoteza na wewe
 
Mungu hajaribiwi Wala hadhihakiwi we unafanya demo juu ya uwezo wa Mungu ili iweje.kama umeishiwa mbinu za kuhubiri tafuta kazi nyingine.

Nakuunga mkono asilimia 100% Kuna mchangiaji mmoja amesema kama kweli alitaka kutenda Muujiza angelala chini huyu mchungaji wamuwekee spika yeye. lakini haya mambo Tunahitaji kuelewa zaidi kutoka kwa wanaoujua ulimwengu wa roho, Mimi hainingii akilini kwamba mtu anaweza kufanya jambo la kupumbavu hivi na kusababisha umauti wa binadamu mwenziye na kutoa such a simple excuse.

Hiyo ni kwa akili yangu ya kidunia, lakini kuna watu wanujua ulimwengu wa roho wanaweza kutufungua macho zaidi.
 
Safi sana, hizi dini zikianza kuwatoa roho kwa design zote itadhihirisha umbumbumbu wa waumini!
 
kuna tofauti gani kati ya miujiza na mazingaobwe?
Hakuna tofauti na muujiza wa kutoa sadaka eti mungu anakuona mpaka mfukoni wakati unafadhili uzinzi wa ma"faza"
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom