Ta Muganyizi
R I P
- Oct 19, 2010
- 5,361
- 2,734
Tukivunja muungano wazenji watahangaika sana.Sasa hivi wanaona oa sababu tumewaachia wanavinjari huku bara waache mchezo bana alh!
Yes, I agree 400 percent. Nawashukuru sana Wazanzibar, tena saaaana, kwa kukataa hili li Muungano. I couldn't thank you enough.Safi sana...unajua sometimes wazanzibar kichwani zikiwa yes wanafanya mambo ya maana sana....
Sisi wenyewe hatuutaki muungano, na aliyeauandaa muswada bila ya kuwashirikisha ni genious fulani hivi kwani alijua kitakachofuata.
Much thanx to him na wazanzibar kwa ujumla
Mike muungano huu haukuwa kwa ridhaa ya wananchi, ni mapatano kati ya Nyerere na karume. Sasa wakati umefika wananchi ndio waamue kama wanauhitaji au la, wasitupelekeshe sisi.Huwezi kulinganisha E.A.C na huu muungano wa kiini macho.Nikiuangalia muungano katika World Politics Persperctives nachelea kuungana na wote wanaotaka muungano huu uvunjwe, huu sio muda wa kuuvunja muungano bali ni muda wa kuuimarisha zaidi muungano kuliko wakati wowote ule uliopita. Nchi zote duniani zenye kuona mbali zinazungumzia kwa namna moja au nyingine kuungana sio kutengana,katika misingi hiyo sioni faida yoyote ya kuvunja muungano bali kuuimarisha uwe bora zaidi.Wazanzibar wanaotaka muungano uvunjike ni wanasiasa wachache wenye uroho wa madaraka tu, naamini wazanzibar wa kawaida wanautaka muungano na ni kweli muungano ni muhimu sana kwa pande zote mbili, japo ni imani yangu binafsi kwamba wazanzibar wanafaidi sana muungano kuliko wabara.Sudan ya kusini imejitenga, sio kwa sababu wanapenda kujitenga la hasha ni kwa sababu ya wenzao wa kaskazini kutowathamini, na ndio maana wanazungumzia kujiunga na Jumuiya ya Afrika mashariki na baadaye East African Federation, kwa kuwa wanaelewa umuhimu wa umoja.Hivi vi nchi vidogovidogo tena maskini katika dunia ya sasa vtaishia kuwa watumwa tu wa nchi za magharibi. Kama kweli waznz katika kujadili muswada wa katiba mpya waliuchana muswada na kuondoka katika mkutano sioni kama huo ni ustaarabu zaidi ya upumbavu, kwa kuwa pale kilichohitajika ni nguvu ya hoja na wala sio hoja ya nguvu.Tuuzungumzie muungano kwa nia ya kuuboresha sio kuubeza wala kuuvunja, na mwingine eti badala ya kutoa hoja yeye anamlaumu nyerere si ujinga huo, nyerere yeye alifanya kazi yake nzuri kwa mujibu wa wakati wake na amekwishajiondokea.Tujenge hoja tuache ubabaishaji.
Mkuu.Mtoto akiwa mkorofi usimwazibu wakati hajatenda kosa. Msubilie pale atakapotenda kosa hapo hapo muanzishie adhabu ya nguvu. Zanzibar naona wanakaribia kutenda kosa na kwa sababu tunajua ni wakorofi basi hapo ndo watajua kwamba sisi ni watawala wao. Tunasubiri siku wakitangaza wamejitenga, ndo watajua kwamba sisi ni nchi na wao ni mkoa. Sijui watakimbila wapi tena na hiyo bahari. Hamtaki muungano au hamutakaki muungano na Tanganyika ila na Waarabu. Akili zote za wazazibari zipo Uarabuni. Jaribu muone
kama muswaha haukutaja KAdhi na OIC. ni ovias utakataliwa na wala-urojo