Musoma: Tujikumbushe 1980 - 1990

Musoma: Tujikumbushe 1980 - 1990

Kulikuwa na mbabe mmoja mrefu, kipande cha mtu..! Mtu wa mazoezi sana Mbeba vyuma pale DIOSES halafu fundi Pikipiki, Alikuwa na Pikipiki kubwa Jeusi akiitwa SANCHO mnamkumbuka?
 
Kulikuwa na mbabe mmoja mrefu, kipande cha mtu..! Mtu wa mazoezi sana Mbeba vyuma pale DIOSES halafu fundi Pikipiki, Alikuwa na Pikipiki kubwa Jeusi akiitwa SANCHO mnamkumbuka?
Ile hotel jirani na dioses,iliitwaje ?
 
Ja mimi mpk leo niko musoma tokea nimezaliwapo 1995 nimeona mengi mazuri na mabaya ndani ya musoma tokea ile ajari ya meli iliyo lipuka enzi zile kule kastamu
enzi ya makundi ya ugomvi kama west lawama,mbio za vijiti,jamaica mokers,jitume,mdomo wa furu n.k
nakumbka kile kiwanda cha mikate cha mugube na winners
nimesoma shule nyingi za msingi lakn kama
musoma
iringo
mwisenge
john bosco
o level ni mwisenge secondary but a level nimesoma moshi majengo
daah.. Nakumbuka enzi hizo kanjanja na msomi ndo walikua na tv cable
enz za nyanganira na didi msira koko walikua wapinzani kwenye siasa mtaa wa iringo
tulikua tunaogelea kwa marwa jenelo ila maji yalikua marefu kweli
nawakumbka sana hawa maticha mwalimu harrison na mwalimu temu wangap wanawakumbuka?

Musoma love you..
Nimesoma iringo,2005 ,kanjanja alikua na tabia goli likielekea tu kufunga ana chezea channel znagom
 
Kwa taarifa yenu. Lile eneo lililoko kati ya stendi. Mtaa wa kusaga, mtaa wa sokoni, na barabara ya Nyerere lilikuwa bustani nzuri katikati kukiwa na maji yatiririkayo. Sina uhkika lakini bustani hiyo imeendelea kulipiwa na serikali ya uingereza kuitunza mpaka ikaleta mzozo halmashauri kwa kuwa hela hizo zilikuwa zinaliwa na wajanja.
Zamani sana miaka ya sabini mtaa wa Kusaga ulikuwa wa madanguro, wenyewe wakiuita BKB-sikuwahi kutafuta kujua maana yake kwa vile nilikuwa mdogo sana; kwa hiyo watu wa heshima walikuwa hawapiti mtaa huo wakati wa mchana. Kwenda kununua santuli (Shs 12) pale Bonanza House (nimeona online kuwa siku hizi inaitwa Kigera House) iliyokuwa junction ya Mkendo na Kusaga, watu walikua wanazunguka ama kupitia Market street au Mwigobelo.
 
Pale kanisa katoliki musoma kulikuwa na Padre James akimaliza misa anavua joho anaanza kupiga makofi watoto waliokuwa wanacheza kanisani.
Miaka ya mwanzoni 70 hiyo.
Padri James namkumbuka, na mimi ni kati ya watoto unaowasema tuliokuwa tukiimba naye wakati wa Askofu John Rudin. Padri James alihamishiwa Busegwe akaletwa Padri Alexander Choka; suji kama bado yupo.
 
Mkuu unamkumbuka Msomi bwana bwana ya Nani? Bwana ya MAMA RHOBI hahahaha
Bwana alimaliza digrii ya engineering kwa first class, na alikuwa ameajiriwa kufundisha chuo kikuu cha Dar es Salaam. Ila aliamua kurudi kuendeleza biashara za nyumbani na kuziweka katika levo mpya; nilipta kwenye baa yake mwanzoni mwa miaka ya tisini ilikuwa inatesa sana pale Musoma.
 
Mkendo Garage, Disco Center, Makoko Center, Mutex, Abel Mwanga, Mutaragara Chirangi, Power Musoma, Bukwaya Express, Musoma Bus, Biafra, Mwigobelo Dispensary, Makoko Pork, Enzi zetu hizo, 1984-1992
Disco Centre iliitwa Makongoro Music Centre pale Mukendo
 
Hivi wakati wa UMISETA zile vurugu za Mara Sec na Musoma Tech bado zipo maana hao watoto walikua wanafunga Mji kabisaa. Musoma Day shule ya Watoto wababe ipo bado
 
Padri James namkumbuka, na mimi ni kati ya watoto unaowasema tuliokuwa tukiimba naye wakati wa Askofu John Rudin. Padri James alihamishiwa Busegwe akaletwa Padri Alexander Choka; suji kama bado yupo.
Busegwe is my primary school aisee
 
Ipo mpaka leo
Tuweke mapicha ya musoma mjini nime miss sana uwo mjini.....

Shule yangu ya john bosco bado ipo nakumbuka long way back 2003 ndio tulikuwa batch ya kwanza kumaliza la saba katika shule hiyo.....
 
Wachezaji mahiri wa mpira wa Miguu..

Enzi hizo Ahmad Omary Nyarujoya alichezea Young Africans akitokea Musoma.
Ally Mchumila/Mkombozi pia alichezea Young Africans akitokea Musoma.

Marehemu Nico Bambaga alichezea Simba na Malindi akitokea Musoma..

Kulikuwa na vipaji sana enzi hizo kina Bita John aliyewahi kuchezea Pamba FC .

Miaka ile timu za mpira wa miguu kama Usagishaji,RTC ya Musoma,Pamba ya Musoma.

Waamuzi maarufu wa mpira wa Miguu enzi hizo Mzee Abdi..kina Okuku..sijui kama bado wako hai.

Dunia inaenda kasi sana.
 
..duh nimekumbuka shule yangu ya msingi Mkendo primary school... Na musoma club pale wakuu walikua wanavinjari ..akiwemo mshua wangu....

..katika yote uliyasahau ni ile vita ya IDD amin jinsi ndege za kivita za tz zilivyokua zinakuja kugeuzia musoma angani....na kumbuka ndege moja ilianguka maeneo ya mutex...
...nakumbuka ile ndege ya mwalimu nyerere pia..Fokker ilivyokuwa inatua Na kupaa kwa mbwembwe...
...enzi hizo tunaishi hapo nyumba za national house majita road...

...musoma hotel enzi hizo ilibamba sana....

..bila kusahau maziwa ya musoma na nguo za mutex....Na samaki watamu vimoro vya sangara....na mabinti warembo wa musoma na shombo lao la samaki....just amazing memories..
 
Back
Top Bottom