Musoma: Tujikumbushe 1980 - 1990

Musoma: Tujikumbushe 1980 - 1990

CABIN wao wanaita kwa mzee KIBINI

Niliwahi kufika sehemu hiyo maharufu ukifika musoma na siku ya kutaka kuondoka na zawadi ya sato/sangara fresh wa kukaanga unapelekwa au kutajiwa hapo.
 
Nakumbuka mwembeni center- kulikuwa kuna michezo mingi, tulikuwa tunacheza keram na monopoly game ya banki... Wakati mwingine tunaenda library kuu, ilikuwa karibu kwa wahindi, wanakaangiza unabaki kusikia harufu ya mapocho pocho ya kihindi.

Mama Keru, unamsahau vipi, watoto walikuwa wanaenda pale wanaagiza vimto halafu wanakimbia bila kulipa...

MCC ilikuwa zaidi ya Sabasaba ground - ngoma za asili toka maeneo mbalimbali, zilikuwa zinakuja.. Walikujaga wapemba / zanzibar walikuwa wanacheza, utoto bana tunaenda shangaa kiswahili chao.. hahaaha

Haya sasa siku nyingine watoto wa Nyakutonya, wanaenda kusumbua maaskari wa uwanja ndege,, wanaenda na pikipiki wanaanza kuzunguka uwanjani... wanawasha magari ya faya kuwafukuza , hola hola huwezi kuwakamata ..

Siku waliporudi maaskari vita vya Uganda kumuadhibu nduli Amini, tulijaa pale bandarini, hakuna sehemu ya kukanyaga..

Jioni tunaenda kuangalia mpira au mazoezi ya Mara shooting , Akina Mchumila, Joseph Maguti ...lakini kulikuwa na wanafunzi wenzetu walikuwa wanacheza akina Daku abdallah, Mahmoudi.

Musoma primary mtakumbuka Kuyenga au Lumelezi alikuwa anajiita kiboko yao, anasema jumatatu kila mtu na kifagio , watoto wote watawahi... Hata mbabe Abedi, alikuwa anabadilisha nyendo.. Basi raha nyingi .. Uji wa mapande pale Mkendo.. Acha Musoma raha ilikuwa ..

Sigara za kuruka .. mbabe Jose alikuwa na vijana wake kibao wa kennedy, halafu wote wamepiga chuma , eti siku hizi kuna Six pack!!! Kila mmoja kifua kimepanda....
 
CABIN wao wanaita kwa mzee KIBINI

Niliwahi kufika sehemu hiyo maharufu ukifika musoma na siku ya kutaka kuondoka na zawadi ya sato/sangara fresh wa kukaanga unapelekwa au kutajiwa hapo.
Jirani na kwangu hapo... hahaa haa..
 
Shibe ya kutosha enzi hizo ukienda Mwigobero samaki kwa koleo,soko la Nyasho au Kamunyonge, jinumbu jifuru ugari wa udaga we achaaaa!!!
Mwigobero yupo mshikaji tulimaliza naye la saba hapo town.. Nilikwenda na wife miaka ya nyuma alinipa mzigo wa kutosha samaki.. Siku hizi hakuna kitu hapo.
 
Mwaka 70 mpaka 72 nilikuwa nasoma Mwembeni; nilikutana na Nyerere na kushikana mikono sana alipokuwa akija kusali kanisa la Katoliki pale Cathedral Musoma wakati wa mwisho wa mwaka. Nyang'ombori na Mzee Bilali gari ya Kuni walikuwa maarufu kwa upande wao. Ila Fares Nyakutonya na Mutaragara Chirangi walikuwa maarufu sana pale mjini
 
Nimekumbuka Musoma kitongoji cha Kamunyonge, mitaa ya Mukendo na Shabani...Taxi maarufu number 50. Disco kule officers mess na watoto wa kula nao bata wa Buhare chuoni kule. Makoko kule kwa mapadre wamewazalisha na kuwajengea nyumba wadada. Beach party makoko pia. Musoma ilikua ya motoo sana enzi hizo . Jumamosi, lazima twende bandarini asubuhi mida ya saa 4 na kuiwahi meli ya MV Bukoba inatia nanga ikitokea kisumu tulikua tunaenda kununua mikate ya Kenya mitamu hio na laini.
 
Bwana alimaliza digrii ya engineering kwa first class, na alikuwa ameajiriwa kufundisha chuo kikuu cha Dar es Salaam. Ila aliamua kurudi kuendeleza biashara za nyumbani na kuziweka katika levo mpya; nilipta kwenye baa yake mwanzoni mwa miaka ya tisini ilikuwa inatesa sana pale Musoma.
Bila shaka hapa unamuongelea Engineer wa Telecommunications Joseph Bwahna [Joseph 90"]

Alikua na ukumbi wa kutizama cinema pale pia anataka uje umevaa smart na necktie zile kama huna unanunua pale ndio unaingia ndani.
 
Wachezaji mahiri wa mpira wa Miguu..

Enzi hizo Ahmad Omary Nyarujoya alichezea Young Africans akitokea Musoma.
Ally Mchumila/Mkombozi pia alichezea Young Africans akitokea Musoma.

Marehemu Nico Bambaga alichezea Simba na Malindi akitokea Musoma..

Kulikuwa na vipaji sana enzi hizo kina Bita John aliyewahi kuchezea Pamba FC .

Miaka ile timu za mpira wa miguu kama Usagishaji,RTC ya Musoma,Pamba ya Musoma.

Waamuzi maarufu wa mpira wa Miguu enzi hizo Mzee Abdi..kina Okuku..sijui kama bado wako hai.

Dunia inaenda kasi sana.
Hata George Masatu alitokea Musoma huko huko ingawa kipaji chake kilianza kupanda akiwa Pamba ya Mwanza
 
Back
Top Bottom