Nakumbuka mwembeni center- kulikuwa kuna michezo mingi, tulikuwa tunacheza keram na monopoly game ya banki... Wakati mwingine tunaenda library kuu, ilikuwa karibu kwa wahindi, wanakaangiza unabaki kusikia harufu ya mapocho pocho ya kihindi.
Mama Keru, unamsahau vipi, watoto walikuwa wanaenda pale wanaagiza vimto halafu wanakimbia bila kulipa...
MCC ilikuwa zaidi ya Sabasaba ground - ngoma za asili toka maeneo mbalimbali, zilikuwa zinakuja.. Walikujaga wapemba / zanzibar walikuwa wanacheza, utoto bana tunaenda shangaa kiswahili chao.. hahaaha
Haya sasa siku nyingine watoto wa Nyakutonya, wanaenda kusumbua maaskari wa uwanja ndege,, wanaenda na pikipiki wanaanza kuzunguka uwanjani... wanawasha magari ya faya kuwafukuza , hola hola huwezi kuwakamata ..
Siku waliporudi maaskari vita vya Uganda kumuadhibu nduli Amini, tulijaa pale bandarini, hakuna sehemu ya kukanyaga..
Jioni tunaenda kuangalia mpira au mazoezi ya Mara shooting , Akina Mchumila, Joseph Maguti ...lakini kulikuwa na wanafunzi wenzetu walikuwa wanacheza akina Daku abdallah, Mahmoudi.
Musoma primary mtakumbuka Kuyenga au Lumelezi alikuwa anajiita kiboko yao, anasema jumatatu kila mtu na kifagio , watoto wote watawahi... Hata mbabe Abedi, alikuwa anabadilisha nyendo.. Basi raha nyingi .. Uji wa mapande pale Mkendo.. Acha Musoma raha ilikuwa ..
Sigara za kuruka .. mbabe Jose alikuwa na vijana wake kibao wa kennedy, halafu wote wamepiga chuma , eti siku hizi kuna Six pack!!! Kila mmoja kifua kimepanda....