We jamaa tulisoma wote nini umepiga mulemule
Hakuna aliekulia musoma enzi izo asijue MCC ukumbi wenye kila mchezo na burudani, havipo tena hivi.
Tuliosoma Kamunyonge kuangalia ndege kubwa zilizotua uwanjani kuanzia foka na zile kubwa za jeshi tena tukiwa karibu kabisa na running way ilikuwa kawaida, ili land tunalala chini, badae tunaenda darasani kuzichora
umitashumta uwanja wa Mwisenge kuogelea mwanzo mwisho.
Enzi izo kulikuwa na mashindano ya magari, na Pikipiki watu kama MAMAz na MaZida akichora 8 tunasema kapiga norinda.
Kwenda mjini uwanja wa ndege tunavuka kwa kutaim ndg hata kama ipo juu inazunguka utakimbia uiwai mara kadhaa ndege iliwakuta watu katikati ya running way nakulazimika kurudi juu.
Bwawa la kitaji tuliamini lina mashetani ukipita karibu kama mtoto utavutwa ndani
Tulienda majita na gari kama Ndomi na Bukwaya
Kila wikiendi au jioni tukitoka shule basi tunaangalia kama meli imekuja ikiwa imekuja tunakusanyana tunapakizana kwenye phonex kisha tunashindana kwenda bandarini kupanda meli, tulipahta sana Custom, bandarini tuliingia melini tunakula mashudu na mikate huko mpk jioni.
Wakati mwingine meli kubwa tulipotea na kulazimika kutafta wafanyakazi wa meli watutoe nje.
Stand ya zamani kulikuwa na na Tax (cab) za njano na mpangilio mzuri wa namba, ha ha baba angu alipenda sana kutumia namba 50 na 61 zilikiwa nzuri sana, enzi hizi za mwinyi pesa nje nje tax kama baiskel.
Tuliamini sana story za miujiza ya nyerere na kila ndege yake ilipotua Musoma ale uwanjano watoto wate wa Kamunyonge PS tulisimama madirishani kuchungulia Foka imekuja na Nyerere
I miss Home meen miaka mingi sijakwenda.