Musoma Mjini: Kunani pale??

Kimilidzo

JF-Expert Member
Jan 3, 2011
1,346
613
Hali ya kiuchumi katika mji wa Musoma si ya kuridhisha hata kidogo. Baada ya kukaa wiki mbili mfululizo pale mjini nimegundua hali imekuwa mbaya zaidi kiuchumi compared na mara ya mwisho nilienda. Ikiwa ni katikati ya msimu wa utalii mahoteli ya Musoma hayajai, wateja wengi wa mahoteli pale ni watumishi wa serikali waliodaka viposho vya semina na sio watalii.... Ukienda katika Beach kuanzia Tembo Beach hadi Matvilla beach unagundua kuwa beach zao ni za kiwango cha kidunia yani World Class, lakini hakuna watumiaji, ukiagiza Samaki wa kuchoma unaweza kupata baada ya saa mbili kwa kuwa hakuna stock hotelini kwa vile walaji hakuna, inabidi jamaa afuate sokoni fasta ndio akuchomee. Mji uko kilometer zisizozidi 60 kuingia mbuga ya Serengeti, unapishana na makumi ya magari ya kubeba watalii yakielekea mbugani, yana namba za kitanzania, ukisoma ubavuni yana anuani za Arusha, Dar au Moshi, watu wa Musoma wako busy kununua Noah na Hiace za kubeba abiria zikiwa na majina ya timu za Uingereza. Hawataki kugusa biashara ya kupeleka watalii mbugani
Karibu miji yote Tanzania siku hizi ukitembelea utakuta sekta ya ujenzi imepamba moto, maghorofa yanakwenda juu kwa kasi sana na ukiangalia kwenye ubao unaona Client pale ni mzawa fulani, lakini pale Musoma nimeona jengo linajengwa na mfuko wa hifadhi ya jamii, na ni kama ndio property pekee inayoendelezwa pale mjini.
Ukipita katika vijiji vinavyouzunguka mji utakuta hali ya chakula ni mbaya sana, mihogo ina ugonjwa wa Batobato na Mahindi yalikosa mvua hivyo wananchi wana njaa kali.
Lengo langu sio kuwaponda wana Musoma, ila nawapa Challenge kuwa wakati umefika muamke na kufanya kitu kuendeleza rasilimali zilizopo kule Musoma ili maisha yabadilike. Kuna kila rasilimali pale. Mind u that mkoa wa Mara una dhahabu kila kona na Samaki kibao ziwani. Kweli mnakubaliana na hii hali ya hotel inayochaji shs 50,000 malazi siku moja kuwa na wateja wawili karibu wiki nzima wakati wazungu wanatumia muda mwingi kwenye magari kufika Serengeti??
Najua ni sera mbovu za CCM kutoendeleza uwanja wa ndege wa Musoma, lakini na nyie mjiongeze, acheni kuporomosha majumba Mwanza na Dar, nendeni nyumbani mkaweke fursa za ajira kwa ndugu zenu...
Najua kuna wana JF kibao wa kutoka Mara kama Etaro, Nata, Ngoreme, Chacha, Mwita nk, Hebu tuelezeni kunani pale, mbona maisha yanazidi kuwa magumu?
 
Mkuu hukufika bandarini pale? Hivi kuna jahazi hata moja linafika pale kwa siku?
 
Mkuu hongera kwa kuliona hili swala hawa jamaa wa hapa wanadhani deal ni kushindana kukaa dar na mwanza kuna familia maarufu kweli katika huu mkoa lakini ukiangalia mchango wao katika kuundeleza mkoa wa Mara hakuna
Hali ya kiuchumi katika mji wa Musoma si ya kuridhisha hata kidogo. Baada ya kukaa wiki mbili mfululizo pale mjini nimegundua hali imekuwa mbaya zaidi kiuchumi compared na mara ya mwisho nilienda. Ikiwa ni katikati ya msimu wa utalii mahoteli ya Musoma hayajai, wateja wengi wa mahoteli pale ni watumishi wa serikali waliodaka viposho vya semina na sio watalii.... Ukienda katika Beach kuanzia Tembo Beach hadi Matvilla beach unagundua kuwa beach zao ni za kiwango cha kidunia yani World Class, lakini hakuna watumiaji, ukiagiza Samaki wa kuchoma unaweza kupata baada ya saa mbili kwa kuwa hakuna stock hotelini kwa vile walaji hakuna, inabidi jamaa afuate sokoni fasta ndio akuchomee. Mji uko kilometer zisizozidi 60 kuingia mbuga ya Serengeti, unapishana na makumi ya magari ya kubeba watalii yakielekea mbugani, yana namba za kitanzania, ukisoma ubavuni yana anuani za Arusha, Dar au Moshi, watu wa Musoma wako busy kununua Noah na Hiace za kubeba abiria zikiwa na majina ya timu za Uingereza. Hawataki kugusa biashara ya kupeleka watalii mbugani
Karibu miji yote Tanzania siku hizi ukitembelea utakuta sekta ya ujenzi imepamba moto, maghorofa yanakwenda juu kwa kasi sana na ukiangalia kwenye ubao unaona Client pale ni mzawa fulani, lakini pale Musoma nimeona jengo linajengwa na mfuko wa hifadhi ya jamii, na ni kama ndio property pekee inayoendelezwa pale mjini.
Ukipita katika vijiji vinavyouzunguka mji utakuta hali ya chakula ni mbaya sana, mihogo ina ugonjwa wa Batobato na Mahindi yalikosa mvua hivyo wananchi wana njaa kali.
Lengo langu sio kuwaponda wana Musoma, ila nawapa Challenge kuwa wakati umefika muamke na kufanya kitu kuendeleza rasilimali zilizopo kule Musoma ili maisha yabadilike. Kuna kila rasilimali pale. Mind u that mkoa wa Mara una dhahabu kila kona na Samaki kibao ziwani. Kweli mnakubaliana na hii hali ya hotel inayochaji shs 50,000 malazi siku moja kuwa na wateja wawili karibu wiki nzima wakati wazungu wanatumia muda mwingi kwenye magari kufika Serengeti??
Najua ni sera mbovu za CCM kutoendeleza uwanja wa ndege wa Musoma, lakini na nyie mjiongeze, acheni kuporomosha majumba Mwanza na Dar, nendeni nyumbani mkaweke fursa za ajira kwa ndugu zenu...
Najua kuna wana JF kibao wa kutoka Mara kama Etaro, Nata, Ngoreme, Chacha, Mwita nk, Hebu tuelezeni kunani pale, mbona maisha yanazidi kuwa magumu?
 
AAASSSAAANNNTTTEEE SSSSAAANNNAAA KIMILIDZO kwa kweli utakuwa umetugusa sana wengi, mm nadhani uendelee kufuatilia hiyo hali ya Mara na musoma kwa ujumla ilikuwaelewesha watu zaidi, kwa secta binafsi hasa biashara musoma pana tatizo sugu la watoza kodi TRA kila mfanyabiashara anayejaribu kujitokeza hicho ndio kilio kikuu, TRA wakiona tu investment yeyote utapambana na madai 25 x ya kipato chako wanakuvunja moyo kabisa unakosa Motivation kabisa ya biashara yako, na bado watakufirisi, na cha ajabu wanadiliki kutumia mbinu mbaya utadhani matapeli kama kugushi document,vitisho vya mara kwa mara kama ilivyokuwa polisi kubambika kesi za ajabu, wanakegemea maneno ya uongo mitaani, wkikusikia mitaani una pesa tu kesho yake barua ya TRA,,, hii imesababisha wajasiliamali wengi wamekimbilia mwanza, dar n.k. na hata vijumba vichache ulivyoviona ungepata fursa ya kuwauliza wangekujulisha hilo tatizo la TRA cha ajabu jinsi ulivyoona bado unakuta miaka kadhaa hapo nyuma mkoa wa MARA unakuwa wa nne kitaifa kwa kukusanya kodi.. unadhani nini madhala yake TRA IMEFILISI NA KUUA UCHUMI WA MARA. kwa hiyo wajanja wote tunakimbia na wote waliowahi aidha dar au mwanza wanajuta sana kwa kupoteza muda wao wa kufukuzana na TRA bila mafanikio.. Tunauchungu sana kwani mkoa wetu tunaupenda. very sorry for any inconvenience,,,....
 
Back
Top Bottom