Munich Security conference: Netanyahu awakebehi Waajemi

Munich Security conference: Netanyahu awakebehi Waajemi

Mkuu huyo jamaa kwenye comments zako ndiyo yupo hivyo aisee usimshangae
Ni kweli huyo jamaa akili yake siku zote huwaza kukashifu imani za wengine tu,ndio uwezo wake wa kufikiri ulipoishia hapo hana lingine alijualo.
 
Siasa za mashariki ya kati ni ngumu sana sanaa.
Ziko kama zile za Ulaya kipindi cha Reformation (Protestants V Catholics)
Wengi tunasema chanzo ni mafuta lakini zimeanza hata kabla ya kristo kuzaliwa.
kristo yupi...kama ni yesu wa nazareth wa kwenye biblia jibu ni kwamba hakuwahi kuwepo
 
Chanzo #1 cha migogoro ya Mashariki ya Kati ni DINI ama directly au indirectly hayo mengine yanajazilizia tu. Niorodheshe michache;
(a) Houthi kule Yemen - power struggle between Shia and Sunni - DINI
(b) Qatar Vs Saudi Arabia and others - Qatar anatuhumiwa na wenzie ku-support makundi ya kigaidi - DINI.
(c) Iran support for Hamas Vs Israel - DINI
(d) Palestine Vs Israel - Mji wa Jerusalem - DINI
(e) Iran support for Hizbullah Vs Israel (kuifuta katika uso wa dunia) - DINI
(f) Iran support for Syria - Shia influence - DINI
(g) Muslim Brotherhood Vs Coptic (Egypt) - DINI
(h) Iraq - Shia Vs Sunni - DINI
(i) etc. etc. etc.
Kwa namna moja au nyingine lazima "elements" za dini ziwepo popote penye migogoro middle east unlike other parts of the world.
wrong.

(a)houth and yemen sio dini,kumbuka yemen ya sasa ni muungano wa south yemen na north,
houth walikuwa sidelined ndo wakaanzisha movement,
tatizo kubwa la yemen ni foreign interference.

(b)qatar na saud ,wote walikuwa group moja wakimpiga vita assad,lakini "atar inashea visima vya gase na iran na ilikuwa lazima wawe na diplomatic relation,saudia wakamuona Qatar ni msaliti.

(c)hamas ni sunni,iran kuwasaidia hamas ni kwasababu wapalestina wako occupied na israel,nothing more.

(d)palestina vs israel,it is not about jerusalem peke yake,it is about resisting israel occupation in palestine land.

(e)iran support hizbullah again not about religion,hata rais wa lebanon ni mkiristo,mkuu wa majeshi mkirsto na jana waziri wa mambo ya nje ya marekani alikuwa huko lebanon akiwambia eti serikali ya lebanon iinyang'anye hizbollah silaha in exchange marekani itaizuia israel isichimbe mafuta ya lebanon,
Rais michael oun amekataa.

Hizbollah ndo iliikomboa lebanon toka mikononi mwa israel.


Narudi kumalizia
 
Iran kuisupport syria sio kwa ajili ya kueneza ushia,mpaka dakika hii asilimia kubwa ya jeshi la assad ni sunni,sasa hoja ya dini hapa haipo,same applied to iraq,
iran huzisaidia hizi nchi ili kugain influence in a friendly way,tofauti na nchi kama marekani,wanatoa misaada in exchange na influence,yaani marekani akikusaidia anataka akutawale anavyotaka,kisiasa na kiuchumi,hali haiko hivyo kwa iran,
mnakumbuka mwaka 2014 wakati ISIS wanakaribia kuiteka baghdad na damusca.
Iraq iliomba msaada wa marekani,na jamaa wakawa wanajivuuta vuta kumbe wanaotea ISIS waingia baghdad na isingekuwa iran kuingilia kati,
iraq na syria sasa hivi wangekuwa chini ya ISIS.

(E)muslim brotherhood haiko vitani na coptic,
isis ndo wanaua coptic,

all in all,jamii ya mashariki ya kati including israel wanaweka mambo ya imani mbele,kila wanachokifanya,so ukiona hivyo usidhani issue ni dini
 
kwema mkuu! hata hiyo ya kuangukia kwao ni maujanja
ni kweli pilot wako vizuri maana walijua wangeangukia syria yangekuwa mengine wakajitahidi kufika nyumbani.
 
Hapa ndipo pana tatizo,

Mosi,
Nimekuuliza swali rahisi hujanijibu.
Can you separate any state law (Whether its Positive or natural) from the Legal System ??
Jibu la hili ndilo litafungua uwanja mwingine mpana kimtazamo kwamba Iranian Legal System is a Holistic one; In the sense that it is a creature of Secular, non-secular, traditional laws and positive laws (Laws made my a legislature)

Pili,
Na pia huwezi kusema Supreme Leader Ayatollah ni kiongozi wa Kiroho tu wakati he Wields a considerable powers beyond those of the President. Tuangalie uhalisia wa mambo tofauti na vile vitabu vinatuambia:
1. Ayatollah is the Commander in Chief of all the Iranian Forces.
- The Iranian President cannot appoint Minister of Intelligence and Foreign affairs without the approval of the Ayatollah.
- And he is the one who has all the political powers to declare war and peace on behalf of the Islamic Republic.
2. He is the head of all branches of the government (The Judiciary, The Legislature and the Executive)
3. He has the ability to Veto legislation passed by the parliament.
4. He can dismiss and reinstate minister of the executive of the Islamic Republic.

NB: Mpaka hapa bado tu unahisi kwamba Ayatollah ni kiongozi wa Kiroho tu na siyo Siasa wakati ana nguvu za kuingilia moja kwa moja utendaji kazi wa mihimili yote ya Serikali ???

Tatu,
Tafadhali naomba uelewe lugha Khamenei alitoa mapendekezo na Ushauri na kauli yake haioneshi kuwa amekataa.
Msuome hapa tena "I didn’t tell him not to participate, I told him I won’t recommend him participating" Ni wapi ambapo Khamenei amekataza Ahmedinejad asigombee ?? USHAURI ni tofauti na KATAZO, hivyo mtu unaweza kuukubali au kuukataa wala hufungwi na mtu.

Nne,
Islamic Laws are not only laws as per Quran and Hadith.
In Muslim Jurisprudence Islamic law has more than four Sources apart from these you have mentioned. (Find them)
Sasa kuna kitu unashindwa kukielewa hapa, Islamic Law is one of the major sources of law within the Islamic Republic.
Kila sheria inayotungwa ni ndani ya nchi ni lazima iwiane na Sheria za kiislamu (Any positive laws enacted must be in conformity with the Sharia and traditional laws so as to create Congruence and harmony within the legal system).

Hivyo basi kama ambavyo Papa au Malkia wa Uingereza walivyo viongozi wa Kisiasa na kiroho ndivyo ilivyo kwa bwana Ayatollah Khamenei. Ukifuatilia nchi Uingereza mpaka kufika mwak 2014 bado kulikuwa na kosa la Blasphemy against God, The Church of England and The Queen: Hii sheria ilikuwa inashughulikiwa na mahakama za kawaida kabisaaaa.

NB: Tanzania yenyewe Sheria za Kiislamu ni Sehemu ya Sheria za nchi na zinafanya kazi kwa Waislamu kwenye baadhi ya mambo yanayowahusu, lakini ili ifanye kazi ni lazima ilingane na sheria za nchi (Positive laws). Lakini Iran ni kinyume kabisa, ili sheria za nchi zipite ni lazima zikubaliane na Sheria za kidini (Sharia Law). Na ndiyo maana Iran ni nchi ya kidini kwasababu msingi wa Sheria, Siasa na Uchumi ni Sheria za Kiislamu...

Tano,
Narudia tena kusema hivi,
Huwezi kulinganisha Siasa za Tanzania na zile za Iran kwasababu utakuwa unafananisha maji na mafuta.
Tena huwezi kuielewa katiba ya nchi ya Tanzania bila kupitia mapendekezo ya NYALALI COMMISSION, never ever!
Tanzania yetu kuna ukomo wa Uraisi na katiba imesema wazi kabisa kama nilivyokuwekea mfano hai hapo juu.....!

I rest my case!
Punguza ujuaji na ku-complicate mambo manake from the beginning huishi kujitia "oh; unajua hili;.oh unajua lile" with inclusion of lots of terms! Twende kiuhalisia!

Simple and clear hoja ilikoanzia ni kwamba ulidai Ahmedinejad alishindwa uchaguzi na Rouhan!

Hapa peke yake unaonesha siasa za Iran huzifahamu!

Nikakuambia hakushindwa bali alishatumikia 2 terms na kikatiba asingeweza kugombea 2013!

Nikakuambia 2017 alifanya come back attempt kwa sababu katiba ya Iran inasema sitting president anaweza kugombea only one consecutive term itakayoweka a total of 2 consecutive terms. Lakini kv 2013 hakugombea, bila shaka akaona ile requirements ya 2 consecutive terms ceased to work kv katiba haisemi what kama ametumikia 2 terms halafu akafuata Rais mwingine! Hapo nikakupa mfano wa katiba ya URT!

Nilipotoa mfano wa URT ndipo nawe ukaleta habari za Islamic Law! Nikakujibu Iranian Predency has nothing to do with Islamic Laws!

Kwahiyo jaza ma-terms yako uwezavyo ambayo kuyajibu ni very simple hata kama si mwanasheria! Hoja ni kwamba, Rais wa Iran hachaguliwi kwa sheria za kiislamu!

Ingawaje mara kwa mara umekuwa ukinihoji ikiwa nafahamu hili, mara oh kama nafahamu kwa nia ya kuonesha upo deep; in short unaonekana huzifahamu siasa za Iran!

And FYI, hata hiyo Legal System unayoimba kila wakati haipo kama unavyodhani!

Wakati pale juu kuna Supreme Leader mwenye lots of power backed by religious laws, chini yake kuna The Executive Power.

Kwenye executive power ndipo anapatikana President ambae anachaguliwa kama tunavyochagua sisi and Islamic Laws has nothing to do wit presidency.

Aidha hapa ndipo inapatikana timu ya uongozi wa serikali!

Tafuta katiba ya Iran Article 114 to 132 ndiyo inaelezea kwa kirefu hii Executive Power halafu rudi hapa na hizo habari za Islamic Laws!

Baada ya Executive Power, ndipo unakutana na Legislative Power.

Ndani ya Legislative Power, ndimo miongoni mwa bodies zinazounda zipo zile ambazo purely ni religious kama vile The Guardian Council ambayo inaundwa na Islamic Scholars.


Na ni hawa jamaa ndio walimkata Ahmedijenad in 2017!

Bunge nalo, ni sehemu ya Legislative Power na ingawaje Bunge linaitwa Islamic Consultative Assembly, lakini lina uwakilishi wa Wayahudi & Wakristo according to katiba yao.

Ukitoka kwenye hiyo branch ndo unakutana na mfumo wa mahakama ambao nao ni very complex.

Hizo Islamic Laws unazoimba tangu asubuhi ndizo zipo huko BUT depending na stage ya mahakama husika!

Kwahiyo huwezi kuilezea legal system ya Iran kiujumla jumla kama unavyofanya wewe na kutoa conclusion kwavile tu umesikia Iran is an Islamic country with Islamic law ndo ukadhani kila kitu kinapelekwa Kiislam Islam!
 
Walivyopigana The Ottoman Empire na The British Empire kuhusu Mashariki ya kati kwenye vita ya kwanza ya dunia dini ilihusika vipi ?? Nakubaliana na wewe kwamba dini imechochea sana huu mgogoro. Japo swala la msingi kabisa uliloliacha ni kwamba umeaungalia huu mgogoro ambao ni wa kimataifa katika nyanja ya kikanda tu. Nadhani tuhusishe kila chembe kwenye huu mgogoro: Iran, Muslim Brotherhood, Palestine, Israel, Hezbollah, Daesh na Iraq zipo na ndiyo hatari sana lakini pia usisahau kwamba huu mgogoro umekuwepo sana pale hata kabla ya hawa wadau na unavaa sura mpya kila siku.

Zamani Ulikuwa katika sura ya Crusade na Jihad,
Ukabadilika na kuvaa sura mpya ya Siasa za kimataifa kama ambapo mataifa Makubwa kama The Russian Empire, Imperial Germany, The British Empire, The Republic of France na The Ottoman Empire yalihusishwa moja kwa moja kugombania ile ardhi ya Mashariki ya kati. Hapa dini ilihusika kidogo sanaaa, zaidi zaidi maslahi ya mataifa makubwa ndiyo ilikuwa ni chanzo.

Jiulize hivi Uingereza wasingekubaliana kubaliana na Wazayuni hadi kupelekea The Balfour Declaration leo hii huu ugomvi ungekuwa wapi ??
AU Marekani na Warusi wasingekubaliana kuigawanya Palestina mwaka 1947 chini ya Umoja wa Mataifa na Yerusalem ingebaki chini ya Umoja wa Mataifa kama ilivyokubalika leo hii huu mgogoro ungekuwa wapi ??
AU Marekani na Urusi leo waamue kujitoa nje ya Mashariki ya kati na kuweka vikwazo vya Silaha eneo lile huu mgogoro utachukua sura gani ??
The main issue hapa ni dini, angalia British empire aliivunja ottoman empire baada ya hapo uisilamu haujawahi kuwa na khilafa tena, katika hii vita ya kwanza ya dunia majeshi ya uengereza yakiongozwa na meja gen Allen B waileteka aridhi ya palestina, baada ya hapo wakaanza mpango wa kuwakusanya wayahudi ambao walkuwa wametimuliwa siku nyingi sana kutoka aridhi takatifu na kuanza kuwarudisha tena pale mashariki ya kati. Baada ya zoezi hilo kukamilika mnamo mwaka 1948 taifa la Israel likaasisiwa upya kupitia umoja wa mataifa. Na Israel aliona kama hii haitoshi bila wao kuimiliki Jerusalem, kila kiumbe anafahamu unapotaja Jerusalem unataja eneo takatifu, unataja dini, hata kwa ndugu zangu waisalumu wanajua umuhimu wa hilo eneo kwa sababu ya uepo wa mskiti wa al-aksa. Israel vivile waliona kwamba eneo walilopewa halkuwa lote kama vile walivyopewa na Mungu baada ya kutoka utumwani Misri dini hiyo , so kutokana na hii sababu Israel analenga kuwachokoza majirani zake ili waanzishe vita, baada ya vita atateka maeneo na kuwa miliki yake.
 
The main issue hapa ni dini, angalia British empire aliivunja ottoman empire baada ya hapo uisilamu haujawahi kuwa na khilafa tena, katika hii vita ya kwanza ya dunia majeshi ya uengereza yakiongozwa na meja gen Allen B waileteka aridhi ya palestina, baada ya hapo wakaanza mpango wa kuwakusanya wayahudi ambao walkuwa wametimuliwa siku nyingi sana kutoka aridhi takatifu na kuanza kuwarudisha tena pale mashariki ya kati. Baada ya zoezi hilo kukamilika mnamo mwaka 1948 taifa la Israel likaasisiwa upya kupitia umoja wa mataifa. Na Israel aliona kama hii haitoshi bila wao kuimiliki Jerusalem, kila kiumbe anafahamu unapotaja Jerusalem unataja eneo takatifu, unataja dini, hata kwa ndugu zangu waisalumu wanajua umuhimu wa hilo eneo kwa sababu ya uepo wa mskiti wa al-aksa. Israel vivile waliona kwamba eneo walilopewa halkuwa lote kama vile walivyopewa na Mungu baada ya kutoka utumwani Misri dini hiyo , so kutokana na hii sababu Israel analenga kuwachokoza majirani zake ili waanzishe vita, baada ya vita atateka maeneo na kuwa miliki yake.

hapana sio dini...mambo yapo hivi...kila jamii dunia inamigogoro kwa sababu ya tofauti zetu hadi ktk primitive level mfano mfupi vs mrefu.
kimsingi ni third part ndo mfaidikaji wa hizi tofauti zetu..sasa globalist capitalist ni mafundi sana wa kutumia hizi fursa..ukiaangalia kwa makini ME inasifa kubwa nne
1.ni sehemu yenye jamii nyingi zinazoona fahari juu mitazamo yao kama njia sahihi ya maisha mathalani falme,shia,sunni,kurd,jews,arabs nk.
2.ni kama wapo katikati kijiografia.
3.kuna hazina kuubwa ya mafuta na gesi.
4.wapo weak kimkakati sio wababe kama China,Urusi au NK(labda Irani ila anatafutwa hata kwa kuroga)
sasa kwa dunia yenye kiu ya gas na oil hasa China ni dhahiri Globalist watatumia haya mapungufu kupiga pesa.huumizi kichwa kuwagawa watu wenye tofauti ...mfano kama kuna jamii mbili moja wanatahiri wengine hawatahiri na wasio tahiri ni watawala wenye sera zinazopinga ubeberu..kwanza anzisha NGO hamasisha tohara..kwa misimamo ya kundi jingine ni dhahiri watawala wataweka polisi na jeshi kupinga...sasa sie si tuna F 35 tunakuja kupiga polisi na jeshi lenu kwa sababu hamtii haki za binadamu...tunaweka wanao enda tohara kwa masharti ya kubeba oil na gasi kwa 98:2 pace.
Zambia ni nchi ya kikristo nilitegea ISIS waweke kambi ndola.
 
The main issue hapa ni dini, angalia British empire aliivunja ottoman empire baada ya hapo uisilamu haujawahi kuwa na khilafa tena, katika hii vita ya kwanza ya dunia majeshi ya uengereza yakiongozwa na meja gen Allen B waileteka aridhi ya palestina, baada ya hapo wakaanza mpango wa kuwakusanya wayahudi ambao walkuwa wametimuliwa siku nyingi sana kutoka aridhi takatifu na kuanza kuwarudisha tena pale mashariki ya kati. Baada ya zoezi hilo kukamilika mnamo mwaka 1948 taifa la Israel likaasisiwa upya kupitia umoja wa mataifa. Na Israel aliona kama hii haitoshi bila wao kuimiliki Jerusalem, kila kiumbe anafahamu unapotaja Jerusalem unataja eneo takatifu, unataja dini, hata kwa ndugu zangu waisalumu wanajua umuhimu wa hilo eneo kwa sababu ya uepo wa mskiti wa al-aksa. Israel vivile waliona kwamba eneo walilopewa halkuwa lote kama vile walivyopewa na Mungu baada ya kutoka utumwani Misri dini hiyo , so kutokana na hii sababu Israel analenga kuwachokoza majirani zake ili waanzishe vita, baada ya vita atateka maeneo na kuwa miliki yake.

Mosi,
Utasemaje dini wakati ni tatizo kubwa wakati mpango wa kuivunja Ottoman Empire ulisainiwa na viongozi wa dini ya Kiislamu kama Sharif Husayn ibn Ali , ambaye alikubaliana na Uingereza atawaongoza waarabu kuanzisha uasi dhidi ya Watururuki akitegemea kwamba Waturuki wakianguka basi watapewa eneo kubwa la kutawala. Hapa dini inaingieaje wakati Waislamu wenyewe Waislamu, Wayahudi na Wakristo walikuwa upande moja kumpiga vita Uturuki ambaye alikuwa ndiyo dola kubwa la Kiislamu ??? Hebu tueleweshe dini inaingieje hapa...!

Pili,
Umeshindwa kuangalia upande wa pili wa shilingi kwasababu kwenye ule ugomvi wa Mashariki ya kati hadi kufika vita ya kwanza ya dunia Mataifa ya Kikristo na Kiislamu kama Imperial Germany, Ottoman Empire na Austria yalikuwa upande moja yakimtetea Sultan wa Ottoman asinyang'anywe majimbo na Urusi, Uingereza na Ufaransa. Hoja ya dini ipo lakini haina nguvu sanaa (Not Water tight) kwasababu TRIPLE ALLIANCE iliiundwa biana ya falme za Kikristo na Kiislamu (Ottoman Empire, Imperial Germany, Austria and Bulgaria) na TRIPLE ENTENTE iliundwa na baina ya falme za Kikristo kama (British Empire, The Republic of France, Imperial Russia, International Jewry Movement na Arab Liberation Groups)

Tatu,
Unasahau ukweli ambao Prof Frantz Fanon aliwahi kuusema kwamba tatizo kubwa lililopoelekea na kuchochea Vita na Migogoro tokea karne ya 18 hadi 20 lilikuwa ni IMPERIALISM (Excessive Imperialism). Maslahi ya mataifa makubwa yaligongana kwa kiwango cha juu ndiyo dunia ikashuhudia yaliyotokea mwaka 1914-1918 na 1939-1945. Sasa ukisema dini unasahau kwamba Mabepari wao hawajali sana dini lakini wanaitumia dini kama chombo cha kufanyia unyonyaji.
Waislamu na Waarabu kama Saudi Arabia, Syria, Qatar, Egypt n.k watakuja kuchelewa sana kung'amua hili kwamba leo hii wako Salama kwasababu tu wako upande wa maslahi wa mataifa makubwa kama Urusi, Uingereza, Uchina au Marekani. Ndiyo maana baada ya Camp David Accords 1979 Raisi wa Misri Anwar El Sadat aliachana na mambo ya dini kabisa kwasababu aligundua ukweli moja tu: Ili Misri iishi inabidi iende nje ya dini na iangalie maslahi yake binafsi.

NB: Hivyo usisahau kwamba maslahi ndiyo yameweza kuwafanya Wassuni wa Saudi Arabia ambao wamefundishwa tokea utotoni kwamba Wakristo na Wayahudi ni Makafiri na wanapaswa kuuwawa, leo hii wakae meza moja na Wayuhudi wa Israel na Wakristo wa Marekeni na kufanya biashara huku wakiwaumiza Waislamu wenzao walioko nchini Syria na Yemen.
Unavyoichukulia dini wewe mtu wa Afrika ni tofauti kabisa na jinsi haya mataifa makubwa yanaichukulia dini..

Nne,
Dini kilikuwa ndicho kigezi kikubwa cha vita pale Mashariki ya kati hata kabla ya kuzaliwa Yesu (K.K) na Wakristo, Wayahudi na Waislamu walichinjana sana. Lakini ni lazima ufahamu kwamba ugomvi unapokuwa wa muda mrefu bila suluhu kuna aidha ukaja ukaisha au ukaongezeka kutokana na maslahi fulani fulani. Kitaalamu tunasema ugomvi wowote ule una hatua zake hadi kufika mwisho. Hata kama tukisema tatizo ni dini mbona yule Sultan Salahadeen wa Waislamu alikweza kufanya Amani na Wakristo hadi Mashariki ya kati ikawa na amani.

NB 1: Kuna msemo Professor Malcom Shaw alishawahi kusema kwamba "Human Beings are in a constants competition and conflicts but they all desire one thing in common , Prosperity and Peace" hivyo swali rahisi tu. Je ni kweli ugomvi wa Mashariki ya kati hauna suluhu kweli au wale watu hawataki amani kweli ??? Jibu ni moja tu: UKIONA MWANADAMU ANAFURAHIA UGOMVI AU KITU AMBACHO KINAMUUMIZA BASI JUA KWAMBA ANAPATA MASLAHI MAKUBWA NA HICHO KITU KUWEPO. Leo hii ule ugomvi hauiishi kwasababu kuna watu wananufaika sana na vile vifo vya watoto, ugaidi na magonjwa ya pale Mashariki ya kati. Lakini kama ule ugomvi utakapochukua sura mpya na kuliumiza kila taifa basi jua ni lazima utafikia mwisho tu kwasababu NO ONE WANTS TO ACHIEVE THE STATE OF ANARCHY.

NB 2:
Jiulize kwanini Ulaya ya leo wanaomba sana Mungu ule ugomvi wa Mashariki ya Kati Uishe ?? Jawabu ni rahisi sana: Kipindi hiki ule ugomvi una hatari nyingi sana kwa Usalama wao kuliko faida. Leo hii Wazungu wa Ulaya wawe upande wa Israel na Marekani bila kufikiria unadhani watapona na lile rundo la Maelfu ya Wakimbizi.


HITIMISHO:
Dini pekee ni sababu ndogo sanaa,
Na tusiuangalia huu ugomvi katika mtazamo wa Kiislamu kama tunavyofundishwa Madrasa au Kikristo Sunday School huko makanisani. Kuuelewa huu ugomvi ambao unahatarisha amani ya dunia inabidi usiridhike na majibu ya Mchungaji au Imamu wako, na uangalie na jinsi gani huu mgogoro unaathiri mataifa mengine ya dunia kwa namna ambavyo yanahusiana na Mataifa yaliyoko pale Mashariki ya kati. Tusipende majibu marahisi marahisi tu!
 
Punguza ujuaji na ku-complicate mambo manake from the beginning huishi kujitia "oh; unajua hili;.oh unajua lile" with inclusion of lots of terms! Twende kiuhalisia!

Simple and clear hoja ilikoanzia ni kwamba ulidai Ahmedinejad alishindwa uchaguzi na Rouhan!

Hapa peke yake unaonesha siasa za Iran huzifahamu!

Nikakuambia hakushindwa bali alishatumikia 2 terms na kikatiba asingeweza kugombea 2013!

Nikakuambia 2017 alifanya come back attempt kwa sababu katiba ya Iran inasema sitting president anaweza kugombea only one consecutive term itakayoweka a total of 2 consecutive terms. Lakini kv 2013 hakugombea, bila shaka akaona ile requirements ya 2 consecutive terms ceased to work kv katiba haisemi what kama ametumikia 2 terms halafu akafuata Rais mwingine! Hapo nikakupa mfano wa katiba ya URT!

Nilipotoa mfano wa URT ndipo nawe ukaleta habari za Islamic Law! Nikakujibu Iranian Predency has nothing to do with Islamic Laws!

Kwahiyo jaza ma-terms yako uwezavyo ambayo kuyajibu ni very simple hata kama si mwanasheria! Hoja ni kwamba, Rais wa Iran hachaguliwi kwa sheria za kiislamu!

Ingawaje mara kwa mara umekuwa ukinihoji ikiwa nafahamu hili, mara oh kama nafahamu kwa nia ya kuonesha upo deep; in short unaonekana huzifahamu siasa za Iran!

And FYI, hata hiyo Legal System unayoimba kila wakati haipo kama unavyodhani!

Wakati pale juu kuna Supreme Leader mwenye lots of power backed by religious laws, chini yake kuna The Executive Power.

Kwenye executive power ndipo anapatikana President ambae anachaguliwa kama tunavyochagua sisi and Islamic Laws has nothing to do wit presidency.

Aidha hapa ndipo inapatikana timu ya uongozi wa serikali!

Tafuta katiba ya Iran Article 114 to 132 ndiyo inaelezea kwa kirefu hii Executive Power halafu rudi hapa na hizo habari za Islamic Laws!

Baada ya Executive Power, ndipo unakutana na Legislative Power.

Ndani ya Legislative Power, ndimo miongoni mwa bodies zinazounda zipo zile ambazo purely ni religious kama vile The Guardian Council ambayo inaundwa na Islamic Scholars.


Na ni hawa jamaa ndio walimkata Ahmedijenad in 2017!

Bunge nalo, ni sehemu ya Legislative Power na ingawaje Bunge linaitwa Islamic Consultative Assembly, lakini lina uwakilishi wa Wayahudi & Wakristo according to katiba yao.

Ukitoka kwenye hiyo branch ndo unakutana na mfumo wa mahakama ambao nao ni very complex.

Hizo Islamic Laws unazoimba tangu asubuhi ndizo zipo huko BUT depending na stage ya mahakama husika!

Kwahiyo huwezi kuilezea legal system ya Iran kiujumla jumla kama unavyofanya wewe na kutoa conclusion kwavile tu umesikia Iran is an Islamic country with Islamic law ndo ukadhani kila kitu kinapelekwa Kiislam Islam!
Duh haya maswali ni magumu sana umemuuliza watu wengi sana wana chukuliaga Iran kama nchi ya kiisalam 100% mwanzo ata mimi nilijuwaga hivyo nikakutana na bint mmoja kuongea naye kavaa kama katokea kuswali kumuuliza jina nikashangaa wa 2 naye hivyo hivyo wa 3 naye hivyo hivyo !!
Dah
 
Punguza ujuaji na ku-complicate mambo manake from the beginning huishi kujitia "oh; unajua hili;.oh unajua lile" with inclusion of lots of terms! Twende kiuhalisia!

Hoja ya mimi kuwa mjuaji inatokea wapi ??
Umeishiwa na hoja unaanza kunishambulia mimi sasa! (Ad hominem arguments)
Umekasirika hivi kisa mjadala wa kitaaluma ambao una lengo la kutuongezea wote maarifa ??
Hizi kehebi zinaashiria kitu kimoja tu kinachotutesa wasomi wengi wa Tanzania "Intellectual Arrogance"

NB: Usisahau kwamba ntaendelea kuleta maneno (inclusion of terms) kwasababu kila neno linaloongelewa hapa lina maana yake kabisa katika ulimwengu wa Sheria, Siasa na Falsafa. Hivyo utanisamehe sana kama nakuboa au nakukera kwa kufanya hivi, kwasababu kwangu mimi kila neno katika sentensi lina maana yake ambayo mimi nataka kuielewa.

And FYI, hata hiyo Legal System unayoimba kila wakati haipo kama unavyodhani!

Ungekuwa unajua nini maana ya Legal System basi nina uhakika tusingefika hapa tulipo. (Hili nina uhakika 100%)
Walau hata kama ungekuwa umesoma vizuri MUSLIM JURISPRUDENCE na CONSTITUTIONAL LAW vizuri basi ni lazima tungeelewana na kama kupishana tungepisha kidogo sanaaa. Lakini nimekwambia vitu ambavyo viko wazi sana ambavyo mtoto anayesoma Sheria pale UDSM mwaka wa kwanza anavifahamu kwa undani.

NB: Au niombe msaada kwa watu wengine aidha mimi ndiyo naweza kuwa sielewi,
Hivi ndugu Prof unaweza kutenganisha Sheria za dini nje ya Legal System hasa kwenye nchi ambayo ni ya Kiislamu kikatiba ?? Au ni jambo la Busara kisheria kufanya Comparative Analysis baina ya Islamic Legal System na Common Law Legal System ??

Mkuu wangu myplusbee tuyaache haya mambo maana hayatatusaidia sanaa na wala hatutafika popote.
Cheers to you mkuu!
 
Hoja ya mimi kuwa mjuaji inatokea wapi ??
Umeishiwa na hoja unaanza kunishambulia mimi sasa! (Ad hominem arguments)
Umekasirika hivi kisa mjadala wa kitaaluma ambao una lengo la kutuongezea wote maarifa ??
Hizi kehebi zinaashiria kitu kimoja tu kinachotutesa wasomi wengi wa Tanzania "Intellectual Arrogance"

NB: Usisahau kwamba ntaendelea kuleta maneno (inclusion of terms) kwasababu kila neno linaloongelewa hapa lina maana yake kabisa katika ulimwengu wa Sheria, Siasa na Falsafa. Hivyo utanisamehe sana kama nakuboa au nakukera kwa kufanya hivi, kwasababu kwangu mimi kila neno katika sentensi lina maana yake ambayo mimi nataka kuielewa.



Ungekuwa unajua nini maana ya Legal System basi nina uhakika tusingefika hapa tulipo. (Hili nina uhakika 100%)
Walau hata kama ungekuwa umesoma vizuri MUSLIM JURISPRUDENCE na CONSTITUTIONAL LAW vizuri basi ni lazima tungeelewana na kama kupishana tungepisha kidogo sanaaa. Lakini nimekwambia vitu ambavyo viko wazi sana ambavyo mtoto anayesoma Sheria pale UDSM mwaka wa kwanza anavifahamu kwa undani.

NB: Au niombe msaada kwa watu wengine aidha mimi ndiyo naweza kuwa sielewi,
Hivi ndugu Prof unaweza kutenganisha Sheria za dini nje ya Legal System hasa kwenye nchi ambayo ni ya Kiislamu kikatiba ?? Au ni jambo la Busara kisheria kufanya Comparative Analysis baina ya Islamic Legal System na Common Law Legal System ??

Mkuu wangu myplusbee tuyaache haya mambo maana hayatatusaidia sanaa na wala hatutafika popote.
Cheers to you mkuu!
I am humbled kuitwa huku na mwanazuoni Malcom Lumumba kushiriki Kwenye huu mjadala. Nikianza na Legal system ya nchi kama Tanzania, Kifungu cha 4 cha Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya 1977, kinaelezea kuhusu mugawanyo wa madaraka wa mihimili ya serikali kama, Bunge, Executives na Mahakama. nimeanza kusema hivi kwa sababu kuna hoja huko mbele itakayojibiwa kuhusu Legal system, Katiba and jurisprudence. Katiba yetu inatamka wazi kuwa Mfumo wa kisheria nchini Tanzania unategemea sheria ya kawaida ya Kiingereza ( English common law).. Hata hivyo Kwa mjibu wa ibara ya 2 of the Judicature and Application of Laws Act, Cap. 358, common law, doctrines of equity and statutes of general application are enforceable in Tanzania. Kwa mantiki ya kifungu cha sheria hapo juu, sisi tuliotawaliwa na waingereza tumejikuta tukitumia English Legal system, ingawa siyo wote e.g America etc. Baada ya utangulizi huu, nijikite kwenye kujibu hoja.though katika upembuzi wangu haraka haraka, nimeweza ku-note vitu vifuatavyo kutoka kwa mchambuzi wa awali comredi
myplusbee kama ambavyo nitaonyesha hapo chini;-

  1. Either mchambuzi hafahamu maana ya legal system, utendaji kazi wake na chanzo chake...
  2. Either Hafahamu maana ya jurisprudence na mapana yake..
  3. Either Ametawaliwa na hisia/emotions na kushindwa kujenga hoja bila kuathiri taratibu nyingine..
vyovyote itakavyokuwa, mimi naamini hakuna anayejua yote. ndo maana tupo kujifunza kila siku. kama Lord denning alivyosema, If we never do anything which has not been done before, we shall never get anywhere.

Nini maana ya Legal system? ni mfumo unaohusu utaratibu au mchakato wa kutafsiri na kutekeleza sheria. Inafafanua haki na majukumu kwa njia mbalimbali. Three major legal systems of the world consist of civil law, common law and religious law. Nijuavyo mimi nchi kama Iran mfumo wa kisheria rasmi ni muunganiko wa maadili na usomi /uwanazuoni kutoka kwa Uislam na tamaduni za Ki-Persia. Iran inafuata Islamic legal system na iko identified kama Islamic state.

kwa kuzingatia maelezo hapo juu, huwezi kutenganisha Sheria za dini nje ya Legal System hasa kwenye nchi ambayo ni ya Kiislamu kikatiba kama Iran.

Article 114 of Iran Constitution: It provides, The President of the Republic is elected for four years by the direct vote of the people. His consecutive election is allowed just for one additional term. Sina cha kuongeza wala kupunguza.

Article 115: The President of the Republic must be elected from among the religious and political elite who meet the following qualifications: Iranian origin, Iranian nationality, administrative leadership, clear past record, honesty and piety, believing in the fundamentals of the Islamic Republic of Iran and the official religion of the country.

Bila hata kwenda mbali, Rais anachaguliwa kwa mujibu wa katiba inayotokana na sheria za kidini yenye kulinda maadili, desturi, taratibu na mila za dini ya kiislam. kwa tofasiri nyingine, ili uweze ku-qualify kuchaguliwa kuwa rais nchini Iran-lazima uwe fundamentalists na muumin mkubwa wa uislam. (emphasis is mine)

Labda nikuulize ndugu, uliposema "Tafuta katiba ya Iran Article 114 to 132 ndiyo inaelezea kwa kirefu hii Executive Power halafu rudi hapa na hizo habari za Islamic Laws!" Je ulisoma na kuelewa vifungu hivyo?" kama ni hapana, basi shaka ondoa mkuu, that's why tupo kujadili @myplusbee
 
Back
Top Bottom