Munich Security conference: Netanyahu awakebehi Waajemi

MALCOM LUMUMBA

JF-Expert Member
Jul 26, 2012
20,897
63,783
Huyu jamaa ni mkorofi sana,
Kaenda na mabaki ya ndege ya Irani ambayo haina rubani (Drone) akamuuliza waziri wa Iran kama anaikumbuka na akasema ni lazima aikumbuke kwasababu ni yao. Akatuma ujumbe kwamba waambie madikteta wa Iran wasiwajaribu Waisrael. Lakini naona kwa yanayoendelea sasa hivi nchini Syria, Iran na Israel watakuja kutuletea matatizo makubwa sanaaaaa! Mashariki ya kati imekaa vibaya sanaaa na vita ikianza Iran basi India, Pakistan na Uchina watahusika kwa kiasi kikubwa sanaa.
 
Huyu jamaa ni mkorofi sana,
Kaenda na mabaki ya ndege ya Irani ambayo haina rubani (Drone) akamuuliza waziri wa Iran kama anaikumbuka na akasema ni lazima aikumbuke kwasababu ni yao. Akatuma ujumbe kwamba waambie madikteta wa Iran wasiwajaribu Waisrael. Lakini naona kwa yanayoendelea sasa hivi nchini Syria, Iran na Israel watakuja kutuletea matatizo makubwa sanaaaaa! Mashariki ya kati imekaa vibaya sanaaa na vita ikianza Iran basi India, Pakistan na Uchina watahusika kwa kiasi kikubwa sanaa.

Kwa jicho 3 inaonekana huyo Benjamin ana maumivu sana na hakutarajia labda ile F16 itunguliwe kwa kifupi yupo kwenye povu
 
jamaa atakuwa yupo frustrated. inaonekana mipango yake ya kudistabilize middle east imegonga mwamba baada ya Irani na Urusi kuingilia kati hence povu!!:):). kaspeech kakipovupovu.

Fuatilia hii conference utaona kuna vita kubwa sana sanaa inakuja dhidi ya Urusi.
Maana wazungu wameona yote yanayoendelea sasa hivi yana mkono wa Mrusi...Kuanzia silaha za Uchina, Silaha za Iran, Silaha za Korea Kaskazini Ushindi wa Syria. Yaani Agenda imekuwa ni Urusi...
 
Siasa za mashariki ya kati ni ngumu sana sanaa.
Ziko kama zile za Ulaya kipindi cha Reformation (Protestants V Catholics
)
Wengi tunasema chanzo ni mafuta lakini zimeanza hata kabla ya kristo kuzaliwa.
Mkuu heshima yako...
Hapo kwenye Red naomba unielezee ilikua vipi..
Àksante
 
Siasa za mashariki ya kati ni ngumu sana sanaa.
Ziko kama zile za Ulaya kipindi cha Reformation (Protestants V Catholics)
Wengi tunasema chanzo ni mafuta lakini zimeanza hata kabla ya kristo kuzaliwa.
Nakubaliana na wewe Kiongozi; mafuta sio chanzo cha mauwaji hapo Middle East. Tangu enzi za tawala za Babeli, Rumi, Ottoman, n.k. wanachinjana tu hao majamaa. Mudi mwenyewe kakata shingo nyingi sana katika harakati zake zile; watu wengi sana wamekatwa koromeo kwa kigezo cha dini. Duh! Damu nyingi sana zinatoa machozi ardhini ukanda huo.
 
Fuatilia hii conference utaona kuna vita kubwa sana sanaa inakuja dhidi ya Urusi.
Maana wazungu wameona yote yanayoendelea sasa hivi yana mkono wa Mrusi...Kuanzia silaha za Uchina, Silaha za Iran, Silaha za Korea Kaskazini Ushindi wa Syria. Yaani Agenda imekuwa ni Urusi...
To put it clear; tatizo ni Putin!
 
Back
Top Bottom