MUNGU nitie nguvu nimalize salama

MUNGU nitie nguvu nimalize salama

Ili kuwa inspire watu zaidi ungeongezea hivi;
Mimi ni mwalimu, mshahara wangu kwa mwezi ni xxxxx, mshahara ukitoka natumia 60% na Saving 40%. Nina kipato cha ziada kwa mwezi ni zzzzz. Kutokana na saving zangu kwa mwaka nimeweza kuaccumulate Tzs.xxxxxx ambazo ndo nimetumia kusimamisha huo mjengo 2016.
Kusimamisha huo mjengo gharama haipungui 10million kwa kuwa umetuambia umejenga 2016 hiyo in maana ulikuwa unasave almost 1million kila mwezi. Sasa kwa mishahara ya walimu tunayoijua ni ngumu sana kufanya saving ya million kila mwezi. Embu tupe mbinu ulizotumia ili na sisi 2017 tusimamishe boma kama hilo
 
kwa wewe mwalimu wa kike hatushangai mshahara unaenda kwenye ujenzi lakini pesa ya matumizi inatoka kwa bwana. Usishindane na mtoto wa kike pedeshee anamhonga noah wanangu wa old mosho someni mtatoboa in/roma voice/waambie
 
asante kwa kunitia moyo...nitapambana mpaka dakika ya mwisho...

Hongera sana binti wa kirombo, umepiga hatua kubwa sana. Kutoka uko chuo mwaka wa kwanza 2013 hadi kumaliza 2016 (Probably) and in less than a year uko na mjengo unashusha.

"Kudos"
upload_2017-1-10_12-58-47.png
 
Mkuu amejitahid sana huyu Dada ila hilo jengo halijafika million 10 zaid nichini yahapo yaan kama imekula sana nimilion 7, nahatua hiyo aliyofikia ndio ngumu zaidi nainahitaj gharama kubwa zaid yaaliyotumia mpaka hapo yaan naamini kama ametumia sana basi ndio kwanza yupo robo yagharama zote zampaka nyumba kukamilika. Kujengo pagara (boma) sio kaz ngumu kivile ila kujenga nyumba ndio mtiti ila kila kitu nimalengo2 hongera sana Dada naamini miaka 3 mbele nyumba itakuwa poa
 
mwanamke type yako kwangu hufai hata kuwa mke wa 4....sijaona umuhimu wa kuja kuonyesha mafanikio yako jf au labda unatafuta mwenza wakukupaulia na kukufanyia finishing
Povuuuuu kwa mm naona amefanya ki2 cha maana kwanza kusimamaisha mjengo ambaoa hata wengi we2 hapa jamaii forum tunaweza 2siwe nao Hongera kwako dada kingine unajua umekariri kuwa eti m2 ukiwa na matatizo ndo unatakiwa ku share na wa2 kwan ili iweje.hata furaha pia BIG UP SANA MISS ROMBO KAZAAAAAAA
 
OK ngoja Nami nimpe hongera niondoe majungu......Hongeera lkn usirudie tena kuja kuturingishia ilhali life limechange nowadays
 
Binti amkaaa..I have many reasons to congratulate, ni wasichana wachache sana wenye kariba kama yako kuweza kuyafanya haya bila kutegemea upande wa pili! Hakuna mkono wa shemeji yetu hapo hah hah
 
hongera sana binti wa kirombo Mungu akusaidie na kukutia nguvu umalize salama mjengo wako
 
Hongera zako bibie maneno yawapangaji yasikunyong'onyeshe
 
Awali ya yote napenda kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunipa afya njema na kuweza kuuona mwaka kwa amani,furaha na upendo.

Hii ndo tiba ya maumivu yangu ya mwaka 2016 niliyoamua kusimama nayo ambayo naamin itanipa furaha na heshima namshukuru Mungu hata kwa hapa nilipofikia maana changamoto za hapa na pale za mafundi wetu mnazijua .

Leo nimeamua kuwavunja ukimya walimu wenzangu nikawapitisha saiti nikawaambia hii ndo kazi ya mikono yang kuanzia mwaka 2016 niliyoianza .
"ukimwona mpole,mkimya huwezi jua hata kama anafanya vitu vya maendeleo hivyo"

Naweza mambo yote katika yeye anitiaye nguvu,asante Yesu kwa kunipa moyo na nguvu ya kuendelea na ujenzi..

Nihayo tuuu nimeona nisheee na nyie hata ukiachwa fanya maamuzi ya busara yatakayokupa furaha na heshima...fanya kitu cha maendeleo walimwengu washangae kuwa hata wew mwenyew unaweza kusimama bila 'bwana yule'
Mungu atutie nguvu sote [wewe+mimi+wapenda maendeleo]
Amin
 
Back
Top Bottom