Stavros Myles
JF-Expert Member
- Jun 7, 2020
- 350
- 390
Nawapa Hi wana Jukwaa wote wa JamiiForum ila salamu zangu nyingi nawapa wana Jamii Intelligence.
Naomba niende moja kwa moja kwenye mada tajwa hapo juu, ila naomba nitoe angalizo kwa wale wadau wanaochangia jambo kwa makasiriko au hisia zao kali, mada hii inaweza isiwe kwa ajili yako.
Naomba niende moja kwa moja na mada ( Mungu hakuwa na mpango wakuwa na binadamu zaidi ya Eva na Adam ). Naomba kwanza kabla sijaenda mbele nitoe mahali ambapo unaweza kupatumia kama reference, soma kitabu cha Mwanzo katika Biblia Takatifu kwenye Agano la Kale.
Baada ya hapo naomba niendelee, kwa mujibu wa Biblia Adam alikuwa wa kwanza kabisa kuumbwa na baada ya yeye (Adam) kuwepo m/Mungu akaamua kutumia ubavu wa Adam kumuumba Eva (Eve). Eva aliumbwa kama msaidizi wa Adam, na siku zote wakiwa wanaishi Adam na Eva walikuwa wanaishi wakitembea na kufanya mambo mengi wakiwa watupu kabisa (Hawana nguo ). Hapa naomba niweke utuo kidogo, ukirudia kuisoma Mwanzo katika Biblia utakutana na kisa cha Eva kudanganywa na Ibilisi/Shetani/ Shweitani (though sina hakika na Uandishi wa hili neno la mwisho). Baada ya Eva kukubali kula tunda ambalo Mungu aliwakataza wasile alimshawishi Adam naye ale lile tunda. Baada ya kula lile tunda Adam na Eva wakajikuta wako tupu kabisa (Yaani Naked..nyama nyama ). Kabla sijaenda mbali nataka nijaribu kuchambua sentensi yangu niliyoiandika " Baada ya Eva kukubali kula tunda ambalo Mungu aliwakataza wasile ". Kama Mungu aliwakataza kula lile tunda la mti wa ujuzi wa mema na ubaya ina maana halisi na ya kawaida ya kwamba hakutaka wajijue ya kwamba walikuwa watupu (bila nguo) na kama wangejijua kama walikuwa tupu/naked wangetamaniana na mwisho wa siku wangefanya ngono/mjamiiano then mwishowe wangepata watoto na kuongezeka. Sasa kufikia hapa tunatakiwa tujue Mungu hakutaka uwepo wa binadamu wengine wengi isipokuwa uwepo wa Adam na Eva licha ya kuiumba dunia na Sayari nyingine nyingi. Kuna maswali mazito mengi hapa, sasa kwanini Mungu aliumba Ulimwengu mkubwa huu ambao hakutaka watu wengine wawepo (rejea hapo juu!) ?, Je Mungu alipanga kuwaumba viumbe wengine ambao alitaka wakae katika sehemu nyingine za dunia akiwa anawaweka Adam na Eva kwenye bustani?.
Sasa naomba niachane na mambo ya hapo juu tushuke kidogo hapa. Baada ya Adam na Eva kula lile tunda walifukuzwa kwenye ile bustani ya Eden na wakiwa huko walizaliana na kuanza kuongezeka, ila bado hata huu uzao haukuwa na baraka zozote za moja kwa moja kutoka kwa Mungu kwani hata majibu ya Adam yalikuwa yaliyojaa kiburi kizito mno kwani baada ya kuulizwa na Mungu kwanini alikula tunda alijibu " Si huyo mwanamke uliyenipa ndo kasababisha ".
Kwa sisi tuliopo kwa muda huu kama si Mungu kumtoa Yesu kristo kuja kutuokoa kwa kufa pale msalabani hatukuwa na thamani wala uhalali wa kuishi kabisa.
Nawasilisha, nakaribisha mawazo yenu. 🔌
Naomba niende moja kwa moja kwenye mada tajwa hapo juu, ila naomba nitoe angalizo kwa wale wadau wanaochangia jambo kwa makasiriko au hisia zao kali, mada hii inaweza isiwe kwa ajili yako.
Naomba niende moja kwa moja na mada ( Mungu hakuwa na mpango wakuwa na binadamu zaidi ya Eva na Adam ). Naomba kwanza kabla sijaenda mbele nitoe mahali ambapo unaweza kupatumia kama reference, soma kitabu cha Mwanzo katika Biblia Takatifu kwenye Agano la Kale.
Baada ya hapo naomba niendelee, kwa mujibu wa Biblia Adam alikuwa wa kwanza kabisa kuumbwa na baada ya yeye (Adam) kuwepo m/Mungu akaamua kutumia ubavu wa Adam kumuumba Eva (Eve). Eva aliumbwa kama msaidizi wa Adam, na siku zote wakiwa wanaishi Adam na Eva walikuwa wanaishi wakitembea na kufanya mambo mengi wakiwa watupu kabisa (Hawana nguo ). Hapa naomba niweke utuo kidogo, ukirudia kuisoma Mwanzo katika Biblia utakutana na kisa cha Eva kudanganywa na Ibilisi/Shetani/ Shweitani (though sina hakika na Uandishi wa hili neno la mwisho). Baada ya Eva kukubali kula tunda ambalo Mungu aliwakataza wasile alimshawishi Adam naye ale lile tunda. Baada ya kula lile tunda Adam na Eva wakajikuta wako tupu kabisa (Yaani Naked..nyama nyama ). Kabla sijaenda mbali nataka nijaribu kuchambua sentensi yangu niliyoiandika " Baada ya Eva kukubali kula tunda ambalo Mungu aliwakataza wasile ". Kama Mungu aliwakataza kula lile tunda la mti wa ujuzi wa mema na ubaya ina maana halisi na ya kawaida ya kwamba hakutaka wajijue ya kwamba walikuwa watupu (bila nguo) na kama wangejijua kama walikuwa tupu/naked wangetamaniana na mwisho wa siku wangefanya ngono/mjamiiano then mwishowe wangepata watoto na kuongezeka. Sasa kufikia hapa tunatakiwa tujue Mungu hakutaka uwepo wa binadamu wengine wengi isipokuwa uwepo wa Adam na Eva licha ya kuiumba dunia na Sayari nyingine nyingi. Kuna maswali mazito mengi hapa, sasa kwanini Mungu aliumba Ulimwengu mkubwa huu ambao hakutaka watu wengine wawepo (rejea hapo juu!) ?, Je Mungu alipanga kuwaumba viumbe wengine ambao alitaka wakae katika sehemu nyingine za dunia akiwa anawaweka Adam na Eva kwenye bustani?.
Sasa naomba niachane na mambo ya hapo juu tushuke kidogo hapa. Baada ya Adam na Eva kula lile tunda walifukuzwa kwenye ile bustani ya Eden na wakiwa huko walizaliana na kuanza kuongezeka, ila bado hata huu uzao haukuwa na baraka zozote za moja kwa moja kutoka kwa Mungu kwani hata majibu ya Adam yalikuwa yaliyojaa kiburi kizito mno kwani baada ya kuulizwa na Mungu kwanini alikula tunda alijibu " Si huyo mwanamke uliyenipa ndo kasababisha ".
Kwa sisi tuliopo kwa muda huu kama si Mungu kumtoa Yesu kristo kuja kutuokoa kwa kufa pale msalabani hatukuwa na thamani wala uhalali wa kuishi kabisa.
Nawasilisha, nakaribisha mawazo yenu. 🔌