Mungu Haishi. Maana Si Kiumbe

Mungu Haishi. Maana Si Kiumbe

Kitabu kuandikwa " Mungu akasema" au kikaandikwa "mimi Mungu nasema" ni maamuzi ya muandishi. Maamuzi ya muandishi si maamuzi ya miungu. Haitbibitishi kama vimetoka kwa miungu, hiyo ni style tu ya uandishi.
Ndio mjue kwamba Mmepotoshwa sana. Maana Hakuna Sehemu Mungu kaongea zaidi kitabu kinakuwa MUNGU AKASEMA.. MUNGU ALISEMA. Maana yake Hapa Mungu anasimuliwa

Kitabu akisema. MIMI MUNGU NASEMA. MIMI. MUNGU NAKUAMBIA HIVI.. MIMI MUNGU NATAKA UNIABUDU HVI

vyote vinamasimulizi ya kusimulia Mungu kama Hadithi
 
Babu zetu walio ishi na kufa kabla ya hivi vitabu havijaja,walimjua Mungu ?
Quran 16: 36

Na kwa hakika kwa kila umma tuliutumia Mtume kwamba: Muabuduni Mwenyezi Mungu, na muepukeni Shetani. Basi kati yao wapo alio waongoa MwenyeziMungu. Na kati yao wapo ambao ulio wathibitikia upotovu. Basi tembeeni katika ardhi, muangalie ulikuwaje mwisho wa wanao kanusha.


Babu zako walishapata muonyaji ila kama kawaida walimdhihaki au hata kumuua mwonyaji kama mnavyofanya sasa vitukuu vyao.
 
Hana Sifa hizo unazotaka wewe mkuu. UHAI NA UFU ni sifa za Kiumbe. Mungu si Kiumbe kwahiyo Unaposema nikupe jibu unataka nikupe jibu kwamba Mungu ni kiumbe

Mungu ni Enzi ndio maana Mnamuita Mwenyezi Mungu hana Sina za Kiumbe wewe kiumbe ndio una sifa Za Uhai na UFU
Kwahiyo sasa Mungu yupo na sifa gani....yaani Hayupo hai na wala hafi?

Upo sawa kichwani kweli au umeamka na hangover?
 
Majibu ninayo ila muda wa kukwambia sina maana ushaufanya moyo wako kuwa mgumu
Moyo wangu si mgumu kama Kuna Ukweli. Mfano Wewe umezaa mtoto huyo Mtoto Asipokupa Hela Utamlaani!? Kama Ungekuwa na Uwezo wa Kumlaani

Sasa Mungu amekuumna Halafu bado anataka Vitu kutoka Kwako je Yeye kakosa Nini Mpka aombe sadaka ili Aridhike
 
Quran 23:91

Mwenyezi Mungu hana mwana yeyote, wala hanaye mungu mwengine. Inge kuwa hivyo basi kila mungu angeli chukua alivyo umba, na baadhi yao wangeli washinda wengine. Mwenyezi Mungu ameepukana na sifa wanazo msifu.


Quran 21:

22. Lau wangeli kuwamo humo miungu wengine isipo kuwa Mwenyezi Mungu basi bila ya shaka hizo mbingu na ardhi zingeli fisidika. Subahana 'Llah Ametakasika Mwenyezi Mungu, Bwana wa A'rshi (Kiti cha Enzi), na hayo wanayo yazua.


23. Yeye hahojiwi kwa ayatendayo, na wao ndio wanao hojiwa kwa wayatendayo.
Sasa haya ni maneno ya kitabu walichoandika wakoloni. Nani kawambia miungu lazima igombanie vitu pale ilivyoandikwa,"ingekua hivyo basi kila Mungu angelichukua alivyoumba".
Wewe unajuaje kama miungu iligawana kuumba viumbe tofauti kwenye sayari tofauti utajuaje? Hata waarabu walioandika kuran hawawezi thibitisha chochote.
 
Sayari zipo nyingi. Sio lazima miungu igombanie ardhi ya dunia hii. Inaweza kugawana. Hakuna anaejua chochote
Quran 23:91

Mwenyezi Mungu hana mwana yeyote, wala hanaye mungu mwengine. Inge kuwa hivyo basi kila mungu angeli chukua alivyo umba, na baadhi yao wangeli washinda wengine. Mwenyezi Mungu ameepukana na sifa wanazo msifu.



Kauli zako zinajichanganya sana
 
Kitabu kuandikwa " Mungu akasema" au kikaandikwa "mimi Mungu nasema" ni maamuzi ya muandishi.

Basi Vitabu ni vya Waandishi si vya Mungu wala mtu asiseme mwandishi aliongizwa na Roho Mtakatifu kuandika kama Maamuzi anayo yeye mwandishi aandike ajuacho

Maamuzi ya muandishi si maamuzi ya miungu. Haitbibitishi kama vimetoka kwa miungu, hiyo ni style tu ya uandishi.

Haya Ndio ukweli kwamba Vitabu vingi ni maamuzi ya Waandishi ndio maana Vitabu hivyo vinaupotoshaji mwingi. Unaambiwa Injili ni ya YOHANA ila Si Yohana aliyeandika. Kama Angekuwa ni Yohana basi Tungetakiwa kusikia kwamba Mm Yohana nilipanda Mlimani na Yesu nikamuoma Yesu akiongea na Musa na Elia
 
Watu wamepotoshwa Ndugu yangu. Mungu ameumba Viumbe wengi samaki.. Tembo.. Milima.. Bahari.. Mito.. Malaika.. Majini n.k halafu Eti binadamu tu ndio afanane na Mungu

Halafu kwenye Mahubiri unaambjwa tena Hana Wa Kufanana Naye
Shida ni watu hawataki kujifunza historia za chimbulo la hzi dini ktk mlengo wapili
 
Hao tunajua Wanaishi kama Yalivyo majini n.k Maana Wapo katika Sayari yao na Si Hii Tunayoishi sisi wangekuwa wanaishi hapa Kwetu tungejua Wapo Mtaa fulani
Wewe Umejuaje kama yanaishi kama yalivyo majini? Na hiyo sayari yao inaitwaje? Na kama umeweza kujua ya kwamba uthibitisho wa hao malaika kuishi hakujahusisha wewe kuona wakipanga mtaani kwako au kujua walikopanga asa ni vipi kuishi kwa Mungu unataka mpaka aonekane mitaani au kujulikana nyumba aliyopanga?
 
Quran 23:91

Mwenyezi Mungu hana mwana yeyote, wala hanaye mungu mwengine. Inge kuwa hivyo basi kila mungu angeli chukua alivyo umba, na baadhi yao wangeli washinda wengine. Mwenyezi Mungu ameepukana na sifa wanazo msifu.


Quran 21:

22. Lau wangeli kuwamo humo miungu wengine isipo kuwa Mwenyezi Mungu basi bila ya shaka hizo mbingu na ardhi zingeli fisidika. Subahana 'Llah Ametakasika Mwenyezi Mungu, Bwana wa A'rshi (Kiti cha Enzi), na hayo wanayo yazua.


23. Yeye hahojiwi kwa ayatendayo, na wao ndio wanao hojiwa kwa wayatendayo.
Ukileta vitabu kumtetea Mungu Unakuwa Unaendelea Kujipotosha zaidi
 
Hao wanaopigana Si kwamba Wanapigana na Mungu mwenye Vyote ila Wanapigana Viumbe wao kwa Wao kupigania Mamlaka Fulani kama Sisi Tunavyopigana Huku duniani, Marekani anataka Kupigana na Urusi. Urusi anataka Kupigana na Ukraine. Tanzania na Uganda

Sasa Hawa Viumbe wakaja Huku wakawarubuni Binadamu na Kuandika vitabu na Kuiweka Hiyo Vita Kama Ni kwamba Shetani alikuwa anapigana na Mungu na Akamtupa Duniani halafu Huyo huyo Shetani akaenda Kupiga Stori na Mungu ili akamjaribu tena Ayubu ambaye ni Binadamu. Vitu ambayo kwa Akili timamu haviingii hakilini

Ukiendelea kusoma Vitabu hivyo utagundua kwamba Kuna baadhi ya Mambo Mungu anayezungumziwa kwenye Vitabu alikuwa akitumia MALAIKA wake wakifika eneo hilo wanashindwa. Sasa Unajiuliza hivi Mungu mwenye Vyote anaweza Tuma Jambo likashindikana kweli
Ndo apo sasa??
 
Wewe Umejuaje kama yanaishi kama yalivyo majini? Na hiyo sayari yao inaitwaje? Na kama umeweza kujua ya kwamba uthibitisho wa hao malaika kuishi hakujahusisha wewe kuona wakipanga mtaani kwako au kujua walikopanga asa ni vipi kuishi kwa Mungu unataka mpaka aonekane mitaani au kujulikana nyumba aliyopanga?
Kuna Elimu kubwa Hapa ndugu yangu

Malaika wanaonekana kwa Macho Na Majini pia yanaonekana kwa Macho. Wametoka sayari Yao kuja Duniani kimagendo

Refer Biblia yako kama Ww ni Muumini wa Huko Maria Aliyemzaa Yesu alisema Alimuona Malaika Gabrieli.. Wale walioenda kwenye Kaburi Pia Waliwaona Malaika Waliwaambia kuhusu Yesu

Refer pia Biblia yako kuhusu mji wa Sodoma na Gomora Wale Malaika wanajivika Miili Ya Binadamu tu
 
Basi Vitabu ni vya Waandishi si vya Mungu wala mtu asiseme mwandishi aliongizwa na Roho Mtakatifu kuandika kama Maamuzi anayo yeye mwandishi aandike ajuacho



Haya Ndio ukweli kwamba Vitabu vingi ni maamuzi ya Waandishi ndio maana Vitabu hivyo vinaupotoshaji mwingi. Unaambiwa Injili ni ya YOHANA ila Si Yohana aliyeandika. Kama Angekuwa ni Yohana basi Tungetakiwa kusikia kwamba Mm Yohana nilipanda Mlimani na Yesu nikamuoma Yesu akiongea na Musa na Elia
Ni kweli.
Miungu haijawahi kusema chochote.
Ni wakoloni waliotuletea hizi dini ndio wanaoendesha mawazo yetu na wala si miungu bali ni wakoloni.
 
Mtoa maada Mungu ambaye jina lake halisi ni Yehova sio kiumbe kwaSABABU HAJAUMBWA
 
Kuna Elimu kubwa Hapa ndugu yangu

Malaika wanaonekana kwa Macho Na Majini pia yanaonekana kwa Macho. Wametoka sayari Yao kuja Duniani kimagendo

Refer Biblia yako kama Ww ni Muumini wa Huko Maria Aliyemzaa Yesu alisema Alimuona Malaika Gabrieli.. Wale walioenda kwenye Kaburi Pia Waliwaona Malaika Waliwaambia kuhusu Yesu

Kwahiyo wewe reference yako ni biblia je unaamini vilivyomo kwenye biblia? Tunajadiliana kimaandiko au kwa uelewa wako? Kama kimaandiko basi biblia hiyo ambayo uliotumia kuniaminisha mimi kuwa malaika wanaonekana kwa macho si ndio hiyo hiyo iliyosema kuwa Mungu anaishi milele na ukakataa na kudai kuwa Mungu hana uhai? Sasa ninapokuuliza maswali na ukatumia reference ya kitabu cha dini kuniaminisha mimi, maanake hapo hatupo kwenye facts bali tupo ndani ya imani humo humo za kidini.
 
Kwahiyo hata Yale Mapepo aliyokuwa anatoa Yesu si ya kweli. Vitabu vyote ni Uongo
Nilipokuwa mdogo nilikuwa najua mawingu ndo Mungu, unadhani ningekuwa na uelewa huo Hadi Sasa ,nikaandika kitabu kumuelezea Mungu, unadhani ungeunga mkono mawazo ya kitabu changu?
 
Kwahiyo wewe reference yako ni biblia je unaamini vilivyomo kwenye biblia?
Nimekupa Reference hiyo ili uamini kwanza Kama Upo huko. Ningekupa Stori zingine tofauti usingeniamini na Ndivyo Vitabu vilivyoandikwa na Hao Malaika na Viumbe vingine

Tunajadiliana kimaandiko au kwa uelewa wako? Kama kimaandiko basi biblia hiyo ambayo uliotumia kuniaminisha mimi kuwa malaika wanaonekana kwa macho si ndio hiyo hiyo iliyosema kuwa Mungu anaishi milele na ukakataa na kudai kuwa Mungu hana uhai?

Nimekujibu hapo juu kwamba Nimetumia Hiyo kama Reference itakayo amini kwamba viumbe wengine pia wanaishi na Wana uhai.

Na Tunajadili kwa Kutumia Akili Timamu hatujadili kwa kutumia Maandiko. Viumbe hao Walikuwepo na Walikuwa wanaonekana kabla ya Kitabu chako hicho ndugu


Sasa ninapokuuliza maswali na ukatumia reference ya kitabu cha dini kuniaminisha mimi, maanake hapo hatupo kwenye facts bali tupo ndani ya imani humo humo za kidini.

Nikikuambia Mengine yanayotokea hapa Ulimwenguni utayaamini!? Maana Nataka kwanza Nikuambie Yale unayoyamini uliyoambiwa ukapotoshwa Halafu Baadae ndio uambiwe Yaliyo nje ya Vitabu.

Maana Malaika na Majini yanaonekana kwa Macho kitu ambacho kwenye Vitabu pia Ipo ingawa si kwamba Walianza Kuonekana pale kitabu chako kilipoandikwa walikuwa wanaonekana kabla ya Vitabu hivyo ndugu yangu
 
Mtoa maada Mungu ambaye jina lake halisi ni Yehova sio kiumbe kwaSABABU HAJAUMBWA
UPO SAHIHI

Ingawa Mungu hana hayo majina Mnayompa. Yehova.. Yire.. Yahe.. Allah.. Ukifuatilia kwa Makini hayo ni Majina ya Viumbe Wanaojipa Ukuu wa Mungu asili ya Majina Hayo mengi ni Miungu siyo Mungu
 
Back
Top Bottom