Mungu Haishi. Maana Si Kiumbe

Mungu Haishi. Maana Si Kiumbe

Mungu alaani mtu kwa kutomtolea sadaka wala nini japo tu utakosa baraka kutoka kwake
Sasa nikikosa Baraka kutoka Kwake kwa Kutompa Sadaka yeye anafaidikaje kwa Mimi kukosa Hizo baraka. Yaani ananikosesha Baraka Ili yeye Apate Nini wakati ndio kaniumba

Na Unaposema Mtu akikosa Baraka Maana Yake si Ndio Kama Amekulaani tu
 
Hata malaika na Majini yanazaliana kama Wewe na Mimi Mkuu ingawa Wewe huyaoni kwa Macho.

Mungu ameweka Mifumo yake Ya Uzalianaji hata Binadamu wa kwanza Kuumbwa Waliumbwa wakiwa na Vizazi ili wazae na Wakawekwa Duniani

MALAIKA nao hivyo hivyo Wakawekwa sehemu yao
Majini hivyo hivyo Wakawekwa sehemu yao

Hamaanishi kwa Vile wewe una Uhai basi na Mungu awe na Uhai. Jiwe halina Uhai ila Limeumbwa. Kwa Mantiki yako inatakiwa yule aliyeliumba Jiwe lazima asiwe Hai ili aweze umba Jiwe
Jiwe ni matokeo ya wheathering process halafu hao majini,malaika ni imani tu za kufikirika
 
Sawa mimi siyaoni kwa macho. Je wewe unayaona. Ikiwa hauyaoni umejuaje yanazaliana?

Kwani kwenye Vitabu si Wameandikwa. Hata Huko makanisani si yanatoa Ushuhuda kwamba Yamezaa na Waumini na Hayawezi kuwatoka kwa Sababu yanafamilia na Huyo yaliyemuingilia.

Kwani si Hata vitabu vimeandikwa kwamba Yesu aliyauliza yakasema Yana Majeshi

Ni swala tu la Kutumia Akili. Hata Vitabu vimeandika Majini na Mashetani yana Ufalme wake.

Viumbe Vinazaliana Maana ndivyo Mungu ameviumba

Hiyo ni imani yako na umeibeba ulimwengu wako wote unauona hivyo.

Mimi siyo imani yangu hiyo na siamini katika hayo yote na hayapo. Kwangu huo sio ukweli.

Hata Kama Siyo ukweli kwako haimaanishi kwamba Si UKWELI.. UONGO una Muda wake ukifika Unaisha watu wanajua Ukweli ila UKWELI hauna mwisho. Ukatae huo ndio ukweli ukubali utabaki kuwa ni Ukwlei
 
Acha kuwaza ujinga hakuna kitu kinachiitwa mbingu space ni infinity na ulimwengu unazidi kutanua kwa spidi ya mwanga .unayoiina juu sio mbingu bali ni mwisho wa upeo wa machi yako ,huko juu hakuna mwisho
Una uthibitisho gani kwa haya uyasemayo? Leta ushahidi au kaa kimya
 
Basi Mngekuwa mnaishi naye Mtaa Mmoja. Kama Atakuwa anaishi basi Ungejua Amepanga au Amejenga Sehemu fulani na Hizo Sadaka na Zaka msingekuwa mnapeleka Kanisani mngekuwa Mnampelekea Sehemu anayoishi.

Viumbe waovu wamewapotosha Sana




Viumbe ndio walitengeneza Uhai. Na Uhai una Mwisho maana Yake Kufa. Ukimuweka Mungu kwenye Sifa Hizo basi Mungu Kuna Siku Atakufa kitu ambacho najua Hukubaliani macho pia kwamba Mungu atakufa. Kama Hawezi kufa Basi Hana Uhai
Kwani unapozungumzia malaika uliwahi kuwaona nyumba waliopanga? Au mtaa wanaokaa?
 
Sasa nikikosa Baraka kutoka Kwake kwa Kutompa Sadaka yeye anafaidikaje kwa Mimi kukosa Hizo baraka. Yaani ananikosesha Baraka Ili yeye Apate Nini wakati ndio kaniumba

Na Unaposema Mtu akikosa Baraka Maana Yake si Ndio Kama Amekulaani tu
Mkuu naona safari yangu imeishia hapa byebye
 
Hakika kama Mungu aishivyo, akupe haki yako!
Umeona Mlivyo na Chuki. Sasa Mungu mwenye Vyote Hana Chuki na Wala hana Hisia za Chuki na Kiumbe chake. Ndio maana Mnaombeana Mabaya na Huko kanisani Mnaenda Kila Siku

Mmejaa Chuki Mioyoni mwenu Hasa Mkiambiwa kwamba Hamna Ukweli ndani Yenu. Kwa Mujibu wa vitabu Mungu ametuma Manabii, mitume na Watu kibao wameshindwa Kuirekebisha Dunia kwa Akili yako ya Kawaida Mungu angeamua Kutuma Kitu Kinaweza Shindikana Kweli

Kama Akituma Kitu kikashindikana Kurekebishika Basi Si Mungu mwenye Vyote huyo. Na mpaka anamtuma Mwanae wa Pekee mnamkataa
 
Ila kuna uwezekano pia miungu ilikuwepo na ikaumba binadamu. Ila kwa bahati mbaya kama ambavyo iliweza kuwepo ikawa haipo tena sasa kwa njia zilizo nje ya uelewa wa binadamu, miungu imetoweka. Hayupo hata Mungu mmoja tena🙏🏿🤔
Quran 23:91

Mwenyezi Mungu hana mwana yeyote, wala hanaye mungu mwengine. Inge kuwa hivyo basi kila mungu angeli chukua alivyo umba, na baadhi yao wangeli washinda wengine. Mwenyezi Mungu ameepukana na sifa wanazo msifu.


Quran 21:

22. Lau wangeli kuwamo humo miungu wengine isipo kuwa Mwenyezi Mungu basi bila ya shaka hizo mbingu na ardhi zingeli fisidika. Subahana 'Llah Ametakasika Mwenyezi Mungu, Bwana wa A'rshi (Kiti cha Enzi), na hayo wanayo yazua.


23. Yeye hahojiwi kwa ayatendayo, na wao ndio wanao hojiwa kwa wayatendayo.
 
Ila kuna uwezekano pia miungu ilikuwepo na ikaumba binadamu. Ila kwa bahati mbaya kama ambavyo iliweza kuwepo ikawa haipo tena sasa kwa njia zilizo nje ya uelewa wa binadamu, miungu imetoweka. Hayupo hata Mungu mmoja tena🙏🏿🤔
Quran 23:91

Mwenyezi Mungu hana mwana yeyote, wala hanaye mungu mwengine. Inge kuwa hivyo basi kila mungu angeli chukua alivyo umba, na baadhi yao wangeli washinda wengine. Mwenyezi Mungu ameepukana na sifa wanazo msifu.


Kauli zako zinajichanganya sana
 
Kwani unapozungumzia malaika uliwahi kuwaona nyumba waliopanga? Au mtaa wanaokaa?
Hao tunajua Wanaishi kama Yalivyo majini n.k Maana Wapo katika Sayari yao na Si Hii Tunayoishi sisi wangekuwa wanaishi hapa Kwetu tungejua Wapo Mtaa fulani
 
Kila Kiumbe kimeumbwa na Kuweka Mahali kilipo kwa Muda wake na Ikifikia Hatua kitakufa na Kupotea hata Dunia Hii ina Muda Wake itapotea Na Wewe pia Una Muda Wako ukifika utazeeka Na Kufa
Kwahiyo aliyeumba hivi viumbe alifanya hivyo akiwa HAI au AMEKUFA?

Nijibu tu hapo!!
 
Kwahiyo aliyeumba hivi viumbe alifanya hivyo akiwa HAI au AMEKUFA?

Nijibu tu hapo!!
Hana Sifa hizo unazotaka wewe mkuu. UHAI NA UFU ni sifa za Kiumbe. Mungu si Kiumbe kwahiyo Unaposema nikupe jibu unataka nikupe jibu kwamba Mungu ni kiumbe

Mungu ni Enzi ndio maana Mnamuita Mwenyezi Mungu hana Sina za Kiumbe wewe kiumbe ndio una sifa Za Uhai na UFU
 
Back
Top Bottom