Sio kweli. Kujua mwisho wako haimaaniishi kuwa alipanga uwe hivyo. Kwani wewe unavyomuona mtu akinywa sumu si unaujua mwisho wake? Inamaanisha kuwa ulipanga anywe hiyo sumu?Siku ukiwa Mtunzi hata wa simulizi utaelewa ni Kwa namna gani Mungu ndiye anayepanga maisha yako, na anajua mwisho wa kila kitu
Kwa hiyo jinsi moyo wangu unavyokuwa na matamanio yake mimi ndio naamua huo moyo uwe hivyo ama mungu ndio huamua moyo wako uwe hivi ama vile?Hapana. Ishu ni kwamba anaziona njia zako, matendo yako, maamuzi yako, mfumo wa moyo wako na matamanio yake hivyo yeye kujua kuwa utabadilika au kuacha unachokifanya ni rahisi, huwezi kumfanyia suprice., mwisho wako anaujua.
Ni kama vile wewe unaangalia movie ambayo ulishaiona, unajua kabisa kitakachotokea sio kwa sababu umekifanya kitokee au umepanga ila ni kwa sababu unajua kitatokea sababu una uzoefu wa hiyo filamu.
Sasa MUNGU anaona matamanio ya moyo wako na anajua matokeo ya hayo matamanio siku zote ni nini kitafuata maana matendo ya binadamu ni yale yale tu hakuna jipya ambalo litakuwa suprice.
Kwahiyo wale panya roads hawakulelewa vizuri na wazazi wao?Hoja yangu ni kwamba kama mungu anajua ya kesho yako au maisha yako yatakavyokuwa hapa duniani basi hakuna haja ya kwepo kwa dhambi maana alishajua kwamba wewe utakuwa mizi
Na pia kama mungu anajua kesho yako basi
Bado hujanielewa vizuri ni hivi inamaana tunawaambia wattoto wetu wawe na bidii masomoni ili iweje, kama ni mungu alipanga mwanangu atakua mwalimu basi akae tu nyumbani
Pia tunawalea watoto wetu kwa maadili mazuri ili iweje maana mungu alishapanga kwamba atakuwa mwema, mtoto umleavyo ndio akuavyo mungu hapo anahusikaje
Ni training yako mwenyewe. Kama vile unavyotaka mwili wako uwe na misuli wenye afya au ujae sumu za sigara, shisha bangi. Ts all about you. Ni mwili wako, moyo wako, roho yako.Kwa hiyo jinsi moyo wangu unavyokuwa na matamanio yake mimi ndio naamua huo moyo uwe hivyo ama mungu ndio huamua moyo wako uwe hivi ama vile?
Acheni upumbavu, mbona hukanyagi moto ukuunguze mguu ilihali uwezo wa kuukanyaga unao?Na kama uwezo wa kutuzuia anao ila anaamua kutuacha maana yake anafanya uovu, kitaalam tunaita ‘Sadism’, yaani ni Sadist, ana-enjoy kuona mateso ya wengine, otherwise why uruhusu na unao uwezo wa kuzuia?
Ok kwa hiyo mimi ndio nikaamua moyo wangu uwe vipi kutokana na training yangu, so sio mungu anayeamua moyo wangu uwe na tamaa fulani, na sio mungu anayeamua wala kujua future yangu iwe vipi, sio?Ni training yako mwenyewe. Kama vile unavyotaka mwili wako uwe na misuli wenye afya au ujae sumu za sigara, shisha bangi. Ts all about you. Ni mwili wako, moyo wako, roho yako.
Mimi kuna issue flani nimezinote watu wenye roho mbaya, makatili na washenzi ndio naona wanafanikiwa huku duniani kuliko watu wema sijui hizi hesabu zimekaajeNi ukweli ulio wazi ila ni ngumu kukubalika hasa kwa watu waliokaririshwa imani,
Iko hivi Mungu angekuwa anaijua kesho yako kusingekuwepo na kitu kinachoitwa dhambi, kwa sababu, mfano mtu amechinjwa hapo hakuna dhambi maana tayari mungu alishapanga utachinjwa au huo uovu unaoufanya sasa ungekuwa sio dhambi maana mungu alishapanga.
Njia unayoipitia ndiyo hatima ya maisha yako.
Kuna watu wanamtumikia Mungu mpaka wanazeeka na pia wapo wanamtumikia shetani mpaka wanazeeka.
Pia wapo walikuwa wanamtumikia Mungu ila hawajauona hata ujana
Maisha ni kama simu tu utachagua uitumieje vile unaitumia ndiyo inakupa majibu unayoyataka wewe
Sasa unachanganya. Kuna tofauti ya kujua future yako na kuamua future yako. Anayeamua future yako ni wewe ila iyo future MUNGU anaijua kutokana na maamuzi yako na mambo yanayoumba matamanio yako ndani yako.Ok kwa hiyo mimi ndio nikaamua moyo wangu uwe vipi kutokana na training yangu, so sio mungu anayeamua moyo wangu uwe na tamaa fulani, na sio mungu anayeamua wala kujua future yangu iwe vipi, sio?
Kwa hiyo kama hiyo future yangu naamua mimi, so Mungu anajua nitakachoamua kabla hata sijaamua?Sasa unachanganya. Kuna tofauti ya kujua future yako na kuamua future yako. Anayeamua future yako ni wewe ila iyo future MUNGU anaijua kutokana na maamuzi yako na mambo yanayoumba matamanio yako ndani yako.
Kama wewe binadamu ukimuona binti anatamani kutembea na kila mwanaume unajua kabisa huyu ataishia kupata mimba na ukimwi yeye MUNGU ambaye anawatazama binadamu vizazi na vizazi atashindwaje kujua matokeo ya maamuzi yako? Kuna jambo gani jipya utakalofanya asijue litakapokupeleka? Kama anauwezo wa kuona ndani mawazo ya matamanio yako anashindwa vipi kujua huyu kutokana na hii tamaa atafanya nn?
Akinyofoa hiyo pumzi yako utatendaje huo upumbavu wako?Kwa hiyo ibilisi hapo ndio mwamuzi wa mwisho sababu ndio anaamua akuingize kwenye dhambi ama akuache sio? Na anapoamua Mungu hawezi kumzuia
Yani Mungu akuzuie kufanya maovu yako tu ndipo aonekane Mwema?Kwa hiyo ibilisi hapo ndio mwamuzi wa mwisho sababu ndio anaamua akuingize kwenye dhambi ama akuache sio? Na anapoamua Mungu hawezi kumzuia
maisha baada ya kifo unayatengenezaje wakati nayo pia yashapangwaYani hata usipoenda jua ndivyo ilivyopangwaaa 😀 😀 usidhani kwamba ukienda sijui kuna mpango utaubadilisha hapana ndo maana unaweza toka kanisani na still ukagongwa na gari ukafa... haubadilishi kitu ila hivyo ndivyo ilivyoandikwa juu ya maisha yako zaidi ukienda Kanisani unatengeneza maisha yako baada ya kifo.
Kwa mimi mafanikio ni kuwa na amani ya roho, tena sihitaji mijumba ya kifahari, mali wala mipesa mingi maana naona karibu asimilia kubwa ya vyanzo vya uovu ni ukwasi, kama ilivyokuwa kwa Mfalme Suleiman alipoomba hekima akazidishiwa na utajiri.Mimi kuna issue flani nimezinote watu wenye roho mbaya, makatili na washenzi ndio naona wanafanikiwa huku duniani kuliko watu wema sijui hizi hesabu zimekaaje
mwenye uelewa afafanue. Mimi ni mtu wa dini pia naamini Mungu yupo
Ni kama wewe unavyojua hili gari litakula mafuta kiasi fulani hata kabla hujaliendesha kwa sababu unafahamu mfumo wa cc zake na matokeo ya kuendesha gari lenye hizo cc.Kwa hiyo kama hiyo future yangu naamua mimi, so Mungu anajua nitakachoamua kabla hata sijaamua?
Lakini hilo gari linakua limeundwa hivyo ili kula hizo CC kwa umbali kadhaa, kwa hiyo unasema hata moyo wa mtu kuwa na matamanio fulani ni mungu anakua ameumba hivyo tangia mwanzo?Ni kama wewe unavyojua hili gari litakula mafuta kiasi fulani hata kabla hujaliendesha kwa sababu unafahamu mfumo wa cc zake na matokeo ya kuendesha gari lenye hizo cc.
MUNGU nae anaangalia matamanio yako anajua utakapoelekea. Hakunaga suprice katika maamuzi, lolote utakalolifanya palikuwa na maandalizi, yale maandalizi ndiyo MUNGU huyaona, ukijiandaa kughairi au kubadilika anaona unavyojiandaa kabla hata hujabadilika.
Hilo gari limeundwa ni mashine halina utambuzi, nimelitumia tu kama mfano uone katika kipengele cha kufahamu jambo kutokana na sifa za hilo jambo. Sifa za cc kubwa ni kula mafuta sijaongelea uhusika wa uumbaji wake.Lakini hilo gari linakua limeundwa hivyo ili kula hizo CC kwa umbali kadhaa, kwa hiyo unasema hata moyo wa mtu kuwa na matamanio fulani ni mungu anakua ameumba hivyo tangia mwanzo?
Uwezo wa mungu usiulinganishe na WA Binadamu.Unachosema ni kwamba binadamu hana uchaguzi, hayupo huru zaidi ya kufuata kilichopangwa jambo ambalo si kweli.
Mm nachoona hatufanyi mambo kwa sababu MUNGU amepanga ila MUNGU anajua tutakalofanya kutokana na tabia zetu za maamuzi na tamaa anayoiona ndani yetu.
Kama tu wewe unavyomtambua mwanao wa kiume kiasi kwamba unajua pamoja na kumuonya sana ila nikisafiri nikamuacha atavuta bangi. Wewe kujua kuwa atavuta bangi haimaanishi kuwa ulipanga avute bangi.