Dah! Ribosome mbona umekuwa mkali hivyo? Basi ntakulipa kwa kunieleleza, kiswahili kinanisumbua, anyways asante kwa mchango, ntatafuta the right word hapo.
Naombeni jamani tusaidiane hili. Mume wangu alikuwa masomoni nje ya nchi kwa muda wa miaka miwili, amerudi hivi karibuni. Aliporudi kanunua line ya Airtel ambayo ndio ninayoifahamu. Mie sikujua kumbe mwenzangu kanunua line ya tigo, ambayo hakunambia. Sasa siku moja usiku nashangaa msg inaingia:-
YEYE: Darling mambo vipi? Naona tangu jamaa yako arudi umenitosa
MIE: Mbona mie sikufahamu?
YEYE: Hee! kumbe tuko wengi tunaoiba? Njoo basi tukutane hapa Rose garden
Na mengine meeengiiiii.
Mie nkaushtukia mchezo hapo, ila nkasema wacha nione hii movie mwisho wake utakuwaje. Tukapanga hadi kukutana, bahati nzuri sikuwa na papara. ALHADULILAH! mara nafika eneo la tukio ni yeye huyooo!
Nilighafilika kwa kweli, ingawa hisia zangu zishantuma kuwa kama sio yeye basi ameweka watu wanitrace. Hivi ingekukuta wewe mwana JF mwenzangu, ungeliamuaje hili?
Inawezekana kweli eeh! Sasa kwa mfano ingekuwa kweli mie ni wale wale angefanyaje? dah hiyo trial mie sikuipenda bwana, bora hata angemtumia mtu mwingine.
Bahati nzuri huyo mume wa bombu siyo mimi, Kama ni mimi Power angekuja eneo la tukio angefikia kipondo kikali sana ambacho asingekisahau maisha yake yote.
Sasa wewe ulikwenda kufanya nini kama sio kuzini, maana hata aliyekuandikia meseji ulikuwa humjui, kufika tu hammadi!! mmeo kasimama anaku-observe, ame-confirm, eti?!
Ndoa za vijana ni kazi kweli kweli!!
Kwani huyo mwanamume alikuwa anampima mke wake mwenyewe ili iweje?
Hivi watu hawaamini kwamba kwenye ndoa watu tunaishi kwa kanuni ya imani?
Haya majaribio ya kuprove kwamba some is guilty ni hatari sana...
Heri yetu tunaoamini kuwa kila mtu ni msafi hadi tuuone uchafu wake!!
Babu DC!!
Sasa. . . . ?MKUBALIE.
Is this a true story Bombu?...if it is then am kind puzzled usiku wachat na mtu usiyemfahamu na anakuambia mkutane sehemu ya starehe nawe pasi hiyana waenda, binafsi nashindwa kuelewa lengo lako lilikua ni lipi haswa.