ukicheche wako ni pale ulipopanga kwenda kuonana na huyo jamaa bila kumshirikisha huyo mumeo. kama kweli ulikuwa una haja tu ya kuonana na huyo anayekusumbua si ungemwambia mumeo? na je ungekuta siyo mumeo ungefanyaje? swali litakuwa rahisi kama hujampenda, lakini je ungempenda?Eeh! We kaka/dada ukicheche wangu ni upi hapo jamani? Mie nlitamani tu kumjua huyo anaenitongoza kwa kudai kuwa mie ni mpenz wake. Na mind you huyu mtu alionekana kunifahamu vizuri. Sasa sijui kwa nini umenihukumu hivyo
huyu mumeo ni jinga kabisa!
na ingekuwa kweli unapigwa angefanyaje!
vtu vingine si vya kujalibu bwana!
Kweli mkuu, hapa alitakiwa amueleze mume wake hili jangaYani kama me ndio mumeo nakumwaga mazima unaonekana ni kicheche.
Wewe mwanamke ni miongoni mwa mambumbumbu wa chache kuwahi kutokeaNaombeni jamani tusaidiane hili. Mume wangu alikuwa masomoni nje ya nchi kwa muda wa miaka miwili, amerudi hivi karibuni. Aliporudi kanunua line ya Airtel ambayo ndio ninayoifahamu. Mie sikujua kumbe mwenzangu kanunua line ya tigo, ambayo hakunambia. Sasa siku moja usiku nashangaa msg inaingia:-
YEYE: Darling mambo vipi? Naona tangu jamaa yako arudi umenitosa
MIE: Mbona mie sikufahamu?
YEYE: Hee! kumbe tuko wengi tunaoiba? Njoo basi tukutane hapa Rose garden
Na mengine meeengiiiii.
Mie nkaushtukia mchezo hapo, ila nkasema wacha nione hii movie mwisho wake utakuwaje. Tukapanga hadi kukutana, bahati nzuri sikuwa na papara. ALHADULILAH! mara nafika eneo la tukio ni yeye huyooo!
Nilighafilika kwa kweli, ingawa hisia zangu zishantuma kuwa kama sio yeye basi ameweka watu wanitrace. Hivi ingekukuta wewe mwana JF mwenzangu, ungeliamuaje hili?