Mume wangu hataki kuacha hela ya matumizi

Mume wangu hataki kuacha hela ya matumizi

Habari zenu?

Poleni na majukumu ya kila siku, swali langu ni kwamba je ni sahihi mwanaume kutokuacha hela ya matumizi nyumbani? Binafsi nina miezi miwili toka nifungue biashara ya mgahawa hata bado haijachangamka ila toka nifungue Mume wangu hataki kuacha hela ya matumizi kama mwanzo wakati mtaji wenyewe alikataa kunipa, nimekopa sahivi nina kazi ya kulipa madeni na kulisha familia, tuna mtoto mmoja.

Kwakweli hili swala linaniumiza sana akili, nikimuuliza anadai hali ni ngumu hana hela wakati kabla sijaanza hii biashara alikuwa kila asubuhi anaacha elfu 10 mezani. Naombeni msaada wenu vipi hili Jambo ni sahihi au siyo sahihi?
Nakuonea huruma sana na hiyo ndoa yako, nimeandika gazeti nikalifuta maana kwa dakika nikaimagine kama ingekuwa mimi nategemeq faraja halafu watu wamiseme.

Kipenzi hiyo ndoa utakapoishia sio pazuri sisi hata tukushauri vipi wewe ndio mwamuzi wa mwisho ni kama ulivyoshauriwa kutokuingia katika ndoa na bado ukaolewa.
 
Huyo mtoto baba yake ni nani?
Ndoa yenu ni ya Church, nendeni kwa wasimamizi wa ndoa yenu au pastor.
Hata hili tatizo nalo akashitaki kwa wadhamini na kwa pastor seriously?. Yapo mambo mazito ya kupeleka huko, ila hili anatakiwa a solve unknowns. Alikuwa anatoa, akaacha kwanini?. Je kipato kipo, au hakipo?. Na kama kipo hatoi kwanini, na kama hustle haijakaa sawa ampe muda. In fact ni jambo la kukaa na mumewe kuzungumza sio kuli amplify kama ni bomu linalotaka kulipuka.
 
Hata hili tatizo nalo akashitaki kwa wadhamini na kwa pastor seriously?. Yapo mambo mazito ya kupeleka huko, ila hili anatakiwa a solve unknowns. Alikuwa anatoa, akaacha kwanini?. Je kipato kipo, au hakipo?. Na kama kipo hatoi kwanini, na kama hustle haijakaa sawa ampe muda. In fact ni jambo la kukaa na mumewe kuzungumza sio kuli amplify kama ni bomu linalotaka kulipuka.
Hizi sababu zinafanya watu kibao wanapelekana serikali za mtaa kutafuta suluhu, mwamba anaondoka hatching mia ndani, wife atajua mwenyewe nini afanye jamaa keshasepa kazini.

Hizi changamoto we ona tu hivi watu wanaishi, ni shida sana!!
 
Hizi sababu zinafanya watu kibao wanapelekana serikali za mtaa kutafuta suluhu, mwamba anaondoka hatching mia ndani, wife atajua mwenyewe nini afanye jamaa keshasepa kazini.

Hizi changamoto we ona tu hivi watu wanaishi, ni shida sana!!
Unachosema ni sahihi, lakini kama wao wawili wanashindwa kuyagenga unadhani hao serikali ya mtaa na wengine wanaweza leta permanent solution mkuu?.
 
Habari zenu?

Poleni na majukumu ya kila siku, swali langu ni kwamba je ni sahihi mwanaume kutokuacha hela ya matumizi nyumbani? Binafsi nina miezi miwili toka nifungue biashara ya mgahawa hata bado haijachangamka ila toka nifungue Mume wangu hataki kuacha hela ya matumizi kama mwanzo wakati mtaji wenyewe alikataa kunipa, nimekopa sahivi nina kazi ya kulipa madeni na kulisha familia, tuna mtoto mmoja.

Kwakweli hili swala linaniumiza sana akili, nikimuuliza anadai hali ni ngumu hana hela wakati kabla sijaanza hii biashara alikuwa kila asubuhi anaacha elfu 10 mezani. Naombeni msaada wenu vipi hili Jambo ni sahihi au siyo sahihi?

Hawa wanaume sijui mnawatoa wapi, muwe mnawarudisha mlikowatoa, labda ni Tandahimba..
 
Mpwayungu village anakuja msaidiane kudai hela ya kodi ya meza
 
Mkuu,
Tupo matabaka mengi, hasa bongo hii. Kuna wanaweza kufanya bajeti ya mwezi na kuweka kila kitu mezani, mama atajua mwenyewe(kina nyie).

Kuna wanafanya bajeti, baba ananunua vitu kila mara na kumletea mama, haiachwi mia home.(kina wao).

Kuna wanaonunua kila siku kwa kuacha kodi ya mezani kutokana na kilichpatikana jana, kama nilipiga dei nikapata 15k, nampa mama 10k nabaki na 5k kibaruani(kina sie).

Kwa ground mambo sio rahisi namna hiyo.
Nakua
Mkuu,
Tupo matabaka mengi, hasa bongo hii. Kuna wanaweza kufanya bajeti ya mwezi na kuweka kila kitu mezani, mama atajua mwenyewe(kina nyie).

Kuna wanafanya bajeti, baba ananunua vitu kila mara na kumletea mama, haiachwi mia home.(kina wao).

Kuna wanaonunua kila siku kwa kuacha kodi ya mezani kutokana na kilichpatikana jana, kama nilipiga dei nikapata 15k, nampa mama 10k nabaki na 5k kibaruani(kina sie).

Kwa ground mambo sio rahisi namna hiyo.
Mkuu nakuelewa, na ni kweli Maisha yana tabaka , ila Sasa Mkuu, ndio kwamba Ndani ya nyumba kikosekane kitu mpaka Usipoacha Hela , Basi wanafamilia walalamike ??

Mimi nakua, Mzee wetu alikua anahakikisha Amenunua Mchele kilo za kutosha , Unga wakutosha ( Ule wa kusaga wenyewe ) , Maharage, na mazaga yote yote ambayo hayaharibiki mafuta ya kupikia alinunua Ndoo ndoo , atanunua Chumvi pakiti za kutosha mwezi, atanunua Sukari ya kutosha ,Unga wa ngano , n.k

Atahakikisha kwenye Friza Kuna Nyama kilo Kadhaa, Samaki wabichi sato Kila Kadhaa n.k

Alafu Masuala ya Hela Kwa ajili ya Mengineyo anamalizana na Mke wake ...hapo ndo kama Leo mnataka Mle Ndizi, Sijui Tambi, na kubadilisha badilisha .


Hii kitu nimeibeba Mwenyewe, maana hata utokee umekwama, mambo yameingiliana, unakua na uhakika wa Chakula Ndani hata kama umetembelewa na Ndugu, Rafiki, jamaa.


Na Wife anajua, Nilishamwambiaa, Sitaki kwenye Chakula ulete Bajeti za kichoyo,in fact Moja ya Sababu Kumuacha mwanamke ,kwangu Mimi ni Suala la Chakula.


Nitoe Rai tu, Pamoja kwamba Maisha yetu yanahitaji utoe ulichopata Jana kwaajili ya Leo, Ni vema Kuhakikisha Ndani una Akiba ya Chakula, kuanzia Mafuta mpaka Dona.
 
Habari zenu?

Poleni na majukumu ya kila siku, swali langu ni kwamba je ni sahihi mwanaume kutokuacha hela ya matumizi nyumbani? Binafsi nina miezi miwili toka nifungue biashara ya mgahawa hata bado haijachangamka ila toka nifungue Mume wangu hataki kuacha hela ya matumizi kama mwanzo wakati mtaji wenyewe alikataa kunipa, nimekopa sahivi nina kazi ya kulipa madeni na kulisha familia, tuna mtoto mmoja.

Kwakweli hili swala linaniumiza sana akili, nikimuuliza anadai hali ni ngumu hana hela wakati kabla sijaanza hii biashara alikuwa kila asubuhi anaacha elfu 10 mezani. Naombeni msaada wenu vipi hili Jambo ni sahihi au siyo sahihi?
Kwa maelezo yako inaonyesha hiyo biashara ya mgahawa umeifungua bila makubaliano na mumeo.
 
Hizi sababu zinafanya watu kibao wanapelekana serikali za mtaa kutafuta suluhu, mwamba anaondoka hatching mia ndani, wife atajua mwenyewe nini afanye jamaa keshasepa kazini.

Hizi changamoto we ona tu hivi watu wanaishi, ni shida sana!!
baba anapokosa hela ya kuacha kwake wakwanza kujua ni mkewe, amwambie tu wife leo hali n mbaya tunafanyaje penye wawili hapakos neno, sitak kuamini hao wanandoa wanashindwa kukaa chini na kusolve matatizo yao halaf mnatakiwa mpaka mnaoana ujue mwenzio anaingiza sh ngap ujue namna gam mtasev msonge mbele
 
Back
Top Bottom