Mume wangu hataki kuacha hela ya matumizi

Mume wangu hataki kuacha hela ya matumizi

Usimuwekee chakula, akale huko anakopelekaga chakula.
 
Very simple,jilie zako kabisa mgahawani,ukirudi nyumbani we Unakunywa maji tu,......dogo mbebee kwenye contena kidunchu
Atafanya haya mpaka lini?. Ndio atakuwa ametatua tatizo?. Mpeni mwenzenu permanent solution 😀.Mambo ya nyumba yanahitaji hekima sana, na wakienda jino kwa jino, jahazi halifiki bandarini lazima watagawana mbao.
 


Nadhani hii ndio ya yeye kutokuacha hela ya matumizi, na wewe simple tuu kula huko huko mgahawani kwako mkutane nyumban kulala
 
Ameshakwambia Hana hela,,,sasa ulitaka afanyaje,,kama wewe unayo tumia yako acha ubahili, ubinafsi na uchoyo, kipindi huna kazi kwani alikutangaza kama wewe unavyomtangaza huku mitandaoni, adabu huna vya kwake mtumie wote vya kwako unavionea uchungu hata kwa matumizi ya familia yenu, sasa unatafuta za nini?

Kama hutaki kushiriki kuhudumia familia yako??omba talaka kaishi na huyo utakae ona anafaa kukuachia hela!!!
 
Habari zenu?

Poleni na majukumu ya kila siku, swali langu ni kwamba je ni sahihi mwanaume kutokuacha hela ya matumizi nyumbani? Binafsi nina miezi miwili toka nifungue biashara...
Kwanini usingeolewa na tajiri ona sasa dada unavyotapa tapa au ulisindikiza mapenxi ya kweli sio eeh
 
Habari zenu?

Poleni na majukumu ya kila siku, swali langu ni kwamba je ni sahihi mwanaume kutokuacha hela ya matumizi nyumbani? Binafsi nina miezi miwili toka nifungue biashara ya mgahawa hata bado haijachangamka ila toka nifungue Mume wangu hataki kuacha hela ya matumizi kama mwanzo wakati mtaji wenyewe alikataa kunipa, nimekopa sahivi nina kazi ya kulipa madeni na kulisha familia, tuna mtoto mmoja.

Kwakweli hili swala linaniumiza sana akili, nikimuuliza anadai hali ni ngumu hana hela wakati kabla sijaanza hii biashara alikuwa kila asubuhi anaacha elfu 10 mezani. Naombeni msaada wenu vipi hili Jambo ni sahihi au siyo sahihi?
Weka mpesa namba tukuchangie
 
Huyo mtoto baba yake ni nani?
Ndoa yenu ni ya Church, nendeni kwa wasimamizi wa ndoa yenu au pastor.
 
Seems unamkubali sana huyo jamaa na msela mwenyewe ameshalijua hilo kwahiyo anaamua kukufanya anavyotaka coz anajua huwezi kumfanya chochote, aiseee pole sana.
 
Wewew njoo pm........maana mnasemaga hivyo hivyo kumbe hakuna cha mume wala BIASHARA sema ndio Una Nadi BIASHARA yako
 
Hivi wenzangu nyie Ndoani kwenu, Hela ni Kila siku inaachwa Asubuhi mezani ?.

Mimi Bajeti ya Chakula naifanya Kwa mwezi, na nikitoa naitoa jumla , sitoi Kwa mafungu mafungu .

Nachotaka Chakula kisikosekane Wala kelele za Sijui Hela vile Mara vile

Yes kama Mwanaume , Kuna Hela zile za hapa napale ambazo pia hunifanya Kila siku nikiwa narudi home niwe na kitu mkononi.

Siku Nikikuta Chakula hamna, au wagen wangu au Ndugu wangu hawajala,, itakua ndio tiketi ya kumpeleka kwao akufunfishwe tabia Kisha aolewe na mwanaume mwingine .
Mkuu,
Tupo matabaka mengi, hasa bongo hii. Kuna wanaweza kufanya bajeti ya mwezi na kuweka kila kitu mezani, mama atajua mwenyewe(kina nyie).

Kuna wanafanya bajeti, baba ananunua vitu kila mara na kumletea mama, haiachwi mia home.(kina wao).

Kuna wanaonunua kila siku kwa kuacha kodi ya mezani kutokana na kilichpatikana jana, kama nilipiga dei nikapata 15k, nampa mama 10k nabaki na 5k kibaruani(kina sie).

Kwa ground mambo sio rahisi namna hiyo.
 
Back
Top Bottom