Mume wangu ana kisirani

Mume wangu ana kisirani

mama la mama3

Member
Joined
Feb 19, 2018
Posts
11
Reaction score
8
Jamani mume wangu anakisirani yani ukimkosea kitu kidogo tu anaweza kununa hata miezi sita, hatakula nyumbani, atakublock kwenye mitandao ya kijamii yote na hakuna kitu kitaendelea cha maendeleo mpaka siku ataamua kuacha kununa ndo mtaendelea kuongea.

Yani hii tabia yake nahisi kuichoka natamani mnishauri niishije na Mtu wa namna hii
 
Ni mume wa ndoa? Pole. Mna watoto wangapi? Kama bado fungasha mapeeema la sivyo uamue kuishi hivyo maisha yako yote. Ni shida sana kuishi na mtu wa namna hiyo; hawabadilikagi. Mara nyingi hujiona wao wako sahihi na hawakoseagi. Sasa akijua unampenda umeoza ndo utakoma.
 
Ni mume wa ndoa? Pole. Mna watoto wangapi? Kama bado fungasha mapeeema la sivyo uamue kuishi hivyo maisha yako yote. Ni shida sana kuishi na mtu wa namna hiyo; hawabadilikagi. Mara nyingi hujiona wao wako sahihi na hawakoseagi. Sasa akijua unampenda umeoza ndo utakoma.
Ndiyo ni wa ndoa ,mtoto mmoja
 
Ndiyo ni wa ndoa ,mtoto mmoja

Sasa hapo kazi ni kwako kuchagua kusuka au kunyoa. wewe ndie unayepambana na hizo kero za kununiwa na zitakufanya usiwe huru hata kumhoji yuko wapi akichelewa kurudi hom hata akiongea na simu kiutata hutakiwi kuhoji. Maisha yasiyo na raha kila baada ya siku chache kununiana. Fikiria hayo ndio maisha yako hadi unaingia shimoni... once again...pole inakuhusu.
 
Sasa hapo kazi ni kwako kuchagua kusuka au kunyoa. wewe ndie unayepambana na hizo kero za kununiwa na zitakufanya usiwe huru hata kumhoji yuko wapi akichelewa kurudi hom hata akiongea na simu kiutata hutakiwi kuhoji. Maisha yasiyo na raha kila baada ya siku chache kununiana. Fikiria hayo ndio maisha yako hadi unaingia shimoni... once again...pole inakuhusu.
 
Jamani mume wangu anakisirani a.k.a gubu, yani ukimkosea kitu kidogo tu anaweza kununa hata miezi sita, hatakula nyumbani, atakublock kwenye mitandao ya kijamii yote, tendo la ndoa kama wanandoa hatotaka in short hatakugusa na kila ukikosea anahisi umemdharau.

Yani hii tabia yake nahisi kuichoka natamani mnishauri nifanyeje kwani makwazo madogo kwenye ndoa hayaepukiki, tired.

Kwa Uandishi wako tu huu uliojaa ' Ushangingi ' na ' Ushari ' tuliobobea katika Saikolojia ya Kimawasiliano tayari tumeshagundua kuwa Wewe una matatizo makubwa ambayo ukisema uyaweke katika Kontena basi ile Meli yote ya MSC ( Mediterranean Shipping Company ) itajaa hadi pomoni / juu.
 
Pole sana mama la mama. Japokuwa napata maswali yaso na majibu inamaana miezi sita yote anayokuwa kanuna unashindwa kumsemesha na kujua tatizo ni nini?

Hapo kosa sio la mmoja hata wewe mama la mama inatakiwa ujue namna ya kuishi na huyo mumeo mwenye gubu na sio kuyaacha hayo yote yatokeee.

Kanuna leo kesho muulize nini tatizo ili kama linatatulika mlitatuwe na sio kusubiri miezi halafu mwisho wa siku bado mnakaa chini yanakwisha.
 
Nadhani jf haitakusaidia lolote, nenda kawaeleze ndugu zake kuhusu hilo, mbona suala dogo tu
 
Kwa Uandishi wako tu huu uliojaa ' Ushangingi ' na ' Ushari ' tuliobobea katika Saikolojia ya Kimawasiliano tayari tumeshagundua kuwa Wewe una matatizo makubwa ambayo ukisema uyaweke katika Kontena basi ile Meli yote ya MSC ( Mediterranean Shipping Company ) itajaa hadi pomoni / juu.
Matatizo Gani umegundua?
 
Ndiyo ni wa ndoa ,mtoto mmoja
nini kinamfanya apate kisirani? naona umenyofoa bbaadhi ya contents ili upate support hapa JF. Kisirani kwa kinamama ndo mwake mwake tena mmefuzu kwa ngazi ya PhD mnakosea nyie mnataka kupotezea kwa kisirani chenu. Mwanaume akiwapotezea (kuepusha malumbano, maana kwa midomo wanawake mlio kwenye ndoa hamjambo) hapo ndo mnadai eti Mume ana Kisirani. pole though!
 
Back
Top Bottom